Kanda ya Ziwa ni Lowassa

Kanda ya Ziwa ni Lowassa

Mkuu unaongelea hiyo mikoa iwe chini ya UKAWA baada ya uchaguzi au hivi sasa?
Tafadhali jaribu kufuatilia habari za huko upepo wa kisiasa uko vipi maana hali ni mbaya kwa CCM.

Hii ndio mikoa iliyotia mizizi ya CCM.
 

Best yale mafuriko yalinitisha, halafu mimi mtoto wa kike siwezi kumudu ile hali.
Ila tuombe Mungu taifa nitaenda tena nitawahi ili nipate kiti.
 
Last edited by a moderator:
Ndg wanabodi, salaam!

Baada ya jana kupitia uzi fulani wa maandalizi ya kumpokea ENL Jijini Mwanza - taarifa kuwa Magufuli hakubaliki katika kanda yake sikuiamini. Imenichukua muda wa masaa kadhaa kufanya utafiti mdogo ili kujiridhisha na nani kati ya Edward Lowassa na Dkt. John Magufuli anakubalika. Mwanza niliongea wa watu watano (5) kwa nyakati tofauti na haya ndiyo maswali ya msingi niliyouliza:


  • Mwanza Jiji ikitokea watu kumi (10) wakienda kuchagua rais wagombea wakiwa Magufuli na Lowassa hvi wangapi kati yao watachagua Magufuli na wangapi watampigia Lowassa?


Nilijibiwa: Mtu wa 1: Lowassa anaweza kupata sita au saba

Mtu wa 2: Lowassa anaweza kupata 5 au 6

Mtu wa 3: Lowassa anaweza kupata 6

Mtu wa 4: Lowassa anaweza kushinda (hakutaka kuweka takwimu)

Mtu wa 5: Lowassa atapata kura 5 na Magufuli 5.


  • Katoro nimeuliza watu wawili (2): ikitokea watu kumi (10) wakienda kuchagua rais wagombea wakiwa Magufuli na Lowassa hvi wangapi kati yao watachagua Magufuli na wangapi watampigia Lowassa?
Nilijibiwa: Mtu wa

1: Lowassa anaweza kupata 7
Mtu wa 2: Lowassa anaweza kupata 5


  • Ushirombo nimeuliza watu wanne (4): ikitokea watu kumi (10) wakienda kuchagua rais wagombea wakiwa Magufuli na Lowassa hvi wangapi kati yao watachagua Magufuli na wangapi watampigia Lowassa?


Nilijibiwa: Mtu wa 1: Lowassa anaweza kupata 6

Mtu wa 2: Lowassa anaweza kupata 5

Mtu wa 3: Lowassa anaweza kupata 4

Mtu wa 4: Lowassa anaweza kupata 5

Baada ya kuuliza maswali kwa njia ya simu na kupata majibu haya nimeona ni vizuri niwaletee ili kama kuna waccm wanahitaji ushindi kanda ya ziwa basi waweke mkakati wa kubaini kwa nini kundi la watu fulani halimpendi Dkt. Magufuli badala yake linampenda Edward Lowassa. Aidha, kwa wale wa kundi la Lowassa utafiti huu mdogo uwasukume kuongeza jitihada za kumnadi ili ajulikane zaidi. Mimi sina kinyongo na mgombea yeyote hivyo kwa msomaji mwenye mashaka na findings hizi basi afanye utafiti wake na atuletee humu.

VIVA TANZANIA, 2015 CHAGUA RAIS UMPENDAYE MWENYE UWEZO WA KUTUVUSHA WATANZANIA
 
magufuli oyeeee soma hapa AJALI iliyotokea eneo la Changarawe, Mafinga
Jumatano iliyopita, bado ndiyo habari yenye
kuendelea kujadiliwa kila kona ya Mkoa wa Mbeya.
Ni ajali iliyoua watu 50, leo hii ni vilio kila kona ya Jiji
la Mbeya. Ni wazi itaendelea kubaki katika
kumbukumbu za wakazi wa mikoa ya Mbeya, Iringa
na Njombe kwa miaka mingi ijayo.
Watu wengi waliofariki katika ajali hiyo ni wakazi wa
Jiji la Mbeya, lakini wenye kutoka maeneo
mbalimbali ya mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya
yenyewe.
Siku za Ijumaa, Jumamosi na hadi Jumapili zilikuwa
na pilikapilika za kusafirisha miili ya marehemu na
mazishi, kutoka Mafinga hadi Mbeya na baadaye
kwenye maeneo mbalimbali ya mikoa hiyo kwa ajili
ya mazishi.
Nini hasa sababu ya ajali?
Ni swali lenye kuumiza vichwa vya wakazi wa Jiji
la Mbeya na ndilo lililotawala mazungumzo ya
wakazi wa jiji hilo, tangu kutokea kwa ajali hiyo.
Mengi yamezungumzwa kuhusiana na ajali hiyo,
wapo wenye kuamini kuwa imesababishwa na
ushirikina, wakiamini kuwa ni ajali iliyohusishwa na
utoaji kafara. Hawa yawezekana ni kutokana na
kutoamini kwamba yawezekana kutokea kwa ajali
kama ile, yenye kuteketeza watu wengi kwa wakati
mmoja kutokea.
Lakini zipo sababu za kisayansi zenye kutumika
kuielezea ajali ile, zikiwemo mwendo kasi, ubovu wa
barabara na uzembe. Hata hivyo, sababu kuu
iliyozungumzwa zaidi ni ubovu wa barabara,
kwamba ajali ilisababishwa na dereva wa lori
alipolazimika kulikwepa shimo kwenye eneo hilo la
barabara.
Miongoni mwa wenye kusimamia sababu ya ubovu
wa barabara ni pamoja na Kamanda wa Jeshi la
Polisi mkoani Iringa, Ramadhan Mungi, ambaye
alinukuliwa akisema: “Hapa tusitafute mchawi,
katika hii ajali chanzo kikubwa ni ubovu wa
barabara, hivyo ni jukumu la mamlaka husika
kurekebisha.”
 
Kweli. Nina rafiki yangu yuko Mwanza ni mwanasheria kwa taaluma na ni mtu asiyeegemea upande wowote wa siasa, kaniambia kwa hali ilivyo Mwanza, n dhahiri Lowassa anashinda kwa kishindo dhidi ya Magufuli. Pia hata Mbeya ambako wapenzi wa chadema awali walisononeka Lowassa kukaribishwa na kupewa bendera ya chama, sasa wamejidhatiti kuitoa ccm. Kubea zaidi ni jinsi watu wasio na vyama walivyoipokea Ukawa kwa mikono miwili. Ccm wana kazi ngumu sana, nadhani ni maradufu kuliko viongozi wa ukawa wangeamua vinginevyo khs mgombea urais
 
Mateso ya CCM, - Nilizungumzia kanda ya ziwa sasa labda fanya utafiti iringa kisha utuletee nini umekipata tukijadili pamoja!
 
Mkafred
Tunakushukuru kwa juhudi zako za kufanya utafiti lakini siku nyingine jaribu kuboresha utafiti kwa kupata taarifa za moja kwa moja. Ingependeza zaidi kama hao uliowapigia simu ungewauliza wao wenyewe wanamtaka nani kati ya Magufuli na Lowassa na baadaye ukakokotoa mwenyewe kupata asilimia. Au ungejaribu kuwauliza zaidi na kupata sababu ni kwa nini wanapanga kumpigia huyu wanayemtaka
 
Ushauri wangu kwa UKAWA kampeni ziwe matata sana wahakikishe kila anapokanyaga MUUZA NYUMBA ZA SERIKALI lowassa nae anapita.
 
Mkafred
Tunakushukuru kwa juhudi zako za kufanya utafiti lakini siku nyingine jaribu kuboresha utafiti kwa kupata taarifa za moja kwa moja. Ingependeza zaidi kama hao uliowapigia simu ungewauliza wao wenyewe wanamtaka nani kati ya Magufuli na Lowassa na baadaye ukakokotoa mwenyewe kupata asilimia. Au ungejaribu kuwauliza zaidi na kupata sababu ni kwa nini wanapanga kumpigia huyu wanayemtaka

Asante,
 
Kuna watu wanasema eti CCM mwaka huu wana kazi kubwa mi naona wala hawana kazi kwani kushindwa unahitaji ufanye kazi
Ipi
 
"Mimi Edward Ngoyayi Lowassa , naapa kwamba nitaitetea , nitailinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , nitayatekeleza majukumu yangu ya Urais kwa uwezo wangu wote ......................
Ewe Mwenyezimungu nisaidie"
Then
(makofi , vigeregere , mizinga 21)
Hichi ndicho nachosubiria kukisikia ! Na si vinginevyo .
 
Back
Top Bottom