Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,810
- 831,011
Tunapozungumzia hizi habari wengi wetu tutakimbilia kuwanyooshea vidole wanawake lakini kuna wanaume pia wana hizo tabia
Ndoa na mahusiano ni taasisi moja kubwa sana! Walioko kwenye mahusiano kwa sasa no matter mnapendanaje wengi wenu hamtaoana! Wakwenu wapo na wengine saa hii nao wakiota ndoto kama za kwenu
Ndoa bila kujali imani zetu ni kiunganishi cha kiroho kisihia na fikra za ndani kabisa, ndoa ni mwanzo wa msingi unaokuja kujengewa kuta imara
Kiroho ndoa yako ipo! Mtu wako yupo! Mahusiano yako yapo! Ambayo yatakuja kuwakutanisha bila kutumia nguvu na kulazimisha vitu au hata kutumia nguvu za giza.
Mabinti msibebe mimba kama sababu ya ndoa, wazazi na walezi msipange fumanizi ili kuhalalisha ndoa za mkeka, wandugu msitumie ushawishi wenu nguvu ya fedha na ahadi za kazi nk ili ndoa ifungwe
Kufungwa kwa ndoa ni jambo la kwanza na wanandoa kudumu kwenye ndoa na kuishi maisha ya mafanikio ni kitu kingine kabisa
Wala hakuna haja ya kupoteza muda na fedha kwenda kwa wanajimu wa nyota na watabiri ati kuona kama mtaweza kuishi pamoja.
Utabiri na unajibu hutoa majibu ya jumla tu kutokana na hesabu za nyota na majira ya nyakati, ni vitu vinavyobadilika kila wakati
Jipange na maisha huku ukijibidiisha na kazi, ukiwa na hakika kwamba wako sahihi uliyepangiwa atakuja katika muda sahihi uliopangwa na nguvu iliyo juu yetu sote
Ndoa nyingi zimevurugika na kuharibika kabisa kwa sababu ya kulazimisha mambo...!!!ndoa imeonekana ni taasisi ngumu kwa ajili ya kulazimisha mahusiano...! Kila jambo lina mahali pake Mtu wake na wakati wake!
Soon tutapata couples zilizokutana/kutanishwa na JF! Utashangaa na kujiuliza imekuwaje? Makutano ya mtandaoni! Ni kwa vile ndivyo ilivyopangwa iwe! Tuwaombee, nawe waombee pia! Wako pia hayuko mbali ni muda tu haujafika kama hayuko JF au pale kazini kwako, yuko mahali pengine kona ya mabibo! Vumilia yuaja...! Nakuombea

nielewe tu nilichoandika katika uhalisia wake
