Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Jana nilimsikia kupitia kituo cha Television cha ITV Msemaji(ovyo) wa Simba (Mabingwa wa soka wa Tanzania Bara) Bwana Ezekiel Kamwaga akiujulisha uma wa watanzania hatua wanazojiandaa kuchukua kama team dhidi ya watumia mitandao ya kijamii wote wanaochangia hoja ambazo pengine hazimfurahishi yeye,Viongozi wenzake,na team anayoitumikia kwa ujumla.
Lazima niseme kama ilivyo siku zote jana Kamwaga ameendelea kuongeza shauku yangu ya kutaka kumjua vizuri background yake,elimu yake na mambo kadhaa yanayoweza kujenga weredi wa mtu, Kamwaga aliyekuwa aki'respond to swali la Mwandishi wa habari aliyetaka kujua maoni yake kuhusiana na Haruna Moshi "Boban" baada ya kumchezea rafu iliyoonekana kuwa mbaya mchezaji wa Yanga Kelvin Yondani,aliishia kulaumu watu wanaomshutumu Boban kwa mchezo ule na kumtolea maneno aliyoyaita makali kwenye mitandao ya Kijamii huku akitoa ahadi ya kuwashughulikia, nanukuu "..Simba sasa tunajiandaa kuwashughulikia wale wote wanaomtolea maneno makali mchezaji wetu Haruna Moshi,tumeshaongea na Mwanasheria wetu na tutachukua hatua...." mwisho wa kunukuu.
Kwanza sijajua hivi huu "utumbo" anaouongeaga mara ka mara Msemaji(ovyo) wa hii team huwa ni official taarifa za Club au ni matamshi yake binafsi? Binafsi nafikiri hili ni tatizo kama si la Kamwaga binafsi basi ni la safu nzima ya uongozi wa mabingwa hawa,haiwezekani wawe na mahaba yaliyopitiliza kwa baadhi ya Wachezaji wao kiasi cha kutoona matatizo yao hata pale yanapojionyesha wazi, issue ya utovu wa nidhamu kwa Haruna Moshi "Boban" siyo ya kwanza,aliwahi kumkung'uta ngumi mchezaji mwenzake mbele ya wachezaji wenzake na baadhi ya viongozi na hakufanywa kitu,haya juzi kamvunja mfupa gani sijui beki tegemeo wa team ya Taifa wakati mwenyewe Haruna Moshi akijutia suala lile na kunukuliwa na vyombo vya habari mbalimbali uongozi wa Simba kupitia Msema(ovyo) huyo wanaona ndo kwanza mchezaji wao anaonewa,mi nilitegemea uongozi wa Simba ungekuwa wa kwanza kukaripia tukio lile kwani licha ya kumsababishia matatizo mchezaji wa team ya Taifa lingeweza hata kuigharimu team yake kama Mwamuzi angekuwa fair,je huku si kuficha maradhi ambapo mwisho wake kila mtu anaujua?
Anyway mambo ya Ngoswe namwaachia Ngoswe mwenyewe lkn ninachotaka kumshauri Bwana Kamwaga huu ni wakati wa kuitumia nafasi hii ya kuwa Mwajiriwa wa team ya Dar-es-salaam kwa kuongeza elimu kidogo ili aweze kuongeza weredi wake,elimu ni factor muhimu sana katika kuongeza upeo wa mtu kuelewa,Dsm kuna centre nyingi sana anaweza ku'reseat kama alikuwa hajamalizana na NECTA issue za Credit na mambo mengine ya namna hiyo au kama alikuwa ameshasogeasogea kwenye level ya mbele mathalani Certificate zao zile za Journalism si vibaya akaanza mchakato wa kuitafuta Diploma na kuendelea mbele zaidi, hii itamsaidia kuongeza ufahamu wa yeye kama Msemaji wa team anatakiwa aisemee nini team yake na nini asiisemee,asiangalie umri Wahenga walisema elimu haina mwisho.
Nawasilisha!
Lazima niseme kama ilivyo siku zote jana Kamwaga ameendelea kuongeza shauku yangu ya kutaka kumjua vizuri background yake,elimu yake na mambo kadhaa yanayoweza kujenga weredi wa mtu, Kamwaga aliyekuwa aki'respond to swali la Mwandishi wa habari aliyetaka kujua maoni yake kuhusiana na Haruna Moshi "Boban" baada ya kumchezea rafu iliyoonekana kuwa mbaya mchezaji wa Yanga Kelvin Yondani,aliishia kulaumu watu wanaomshutumu Boban kwa mchezo ule na kumtolea maneno aliyoyaita makali kwenye mitandao ya Kijamii huku akitoa ahadi ya kuwashughulikia, nanukuu "..Simba sasa tunajiandaa kuwashughulikia wale wote wanaomtolea maneno makali mchezaji wetu Haruna Moshi,tumeshaongea na Mwanasheria wetu na tutachukua hatua...." mwisho wa kunukuu.
Kwanza sijajua hivi huu "utumbo" anaouongeaga mara ka mara Msemaji(ovyo) wa hii team huwa ni official taarifa za Club au ni matamshi yake binafsi? Binafsi nafikiri hili ni tatizo kama si la Kamwaga binafsi basi ni la safu nzima ya uongozi wa mabingwa hawa,haiwezekani wawe na mahaba yaliyopitiliza kwa baadhi ya Wachezaji wao kiasi cha kutoona matatizo yao hata pale yanapojionyesha wazi, issue ya utovu wa nidhamu kwa Haruna Moshi "Boban" siyo ya kwanza,aliwahi kumkung'uta ngumi mchezaji mwenzake mbele ya wachezaji wenzake na baadhi ya viongozi na hakufanywa kitu,haya juzi kamvunja mfupa gani sijui beki tegemeo wa team ya Taifa wakati mwenyewe Haruna Moshi akijutia suala lile na kunukuliwa na vyombo vya habari mbalimbali uongozi wa Simba kupitia Msema(ovyo) huyo wanaona ndo kwanza mchezaji wao anaonewa,mi nilitegemea uongozi wa Simba ungekuwa wa kwanza kukaripia tukio lile kwani licha ya kumsababishia matatizo mchezaji wa team ya Taifa lingeweza hata kuigharimu team yake kama Mwamuzi angekuwa fair,je huku si kuficha maradhi ambapo mwisho wake kila mtu anaujua?
Anyway mambo ya Ngoswe namwaachia Ngoswe mwenyewe lkn ninachotaka kumshauri Bwana Kamwaga huu ni wakati wa kuitumia nafasi hii ya kuwa Mwajiriwa wa team ya Dar-es-salaam kwa kuongeza elimu kidogo ili aweze kuongeza weredi wake,elimu ni factor muhimu sana katika kuongeza upeo wa mtu kuelewa,Dsm kuna centre nyingi sana anaweza ku'reseat kama alikuwa hajamalizana na NECTA issue za Credit na mambo mengine ya namna hiyo au kama alikuwa ameshasogeasogea kwenye level ya mbele mathalani Certificate zao zile za Journalism si vibaya akaanza mchakato wa kuitafuta Diploma na kuendelea mbele zaidi, hii itamsaidia kuongeza ufahamu wa yeye kama Msemaji wa team anatakiwa aisemee nini team yake na nini asiisemee,asiangalie umri Wahenga walisema elimu haina mwisho.
Nawasilisha!