Wakuu, hawa jamaa kuaniza tarehe 28.01.2014 bila taarifa yoyote:-
Wamefunga ofisi zao za makao makuu pale Masaki na kubakiza wafanyakazi wasiozidi wanne tu, nadhani wanalinda linda baadhi ya mali zilizosalia kabla ya kutokomea.
Ofisi yao inafunguliwa baada ya saa 5 asubuhi.
Simu zao zote za huduma kwa wateja na zinazoonekana kwenye mtandao wao http://www.sasatel.co.tz/contact-us.html hazipatikani.
Wafanyakazi waliosalia wamewajibu wateja kuwa wana matatizo ya umeme na wangerekebisha ndani ya siku tatu tu lakini ni zaidi ya wiki sasa hakuna huduma ya internet.
Kinachoumiza zaid wamechukua malipo yangu ya bundle ya internet ya miezi miwili kwa ajili ya kibanda changu cha internet na hakuna dalili ya kurudi huduma yao. Ni zaidi ya kurudishana nyuma wakuu.
TCRA tusaidieni katika hili.
Wamefunga ofisi zao za makao makuu pale Masaki na kubakiza wafanyakazi wasiozidi wanne tu, nadhani wanalinda linda baadhi ya mali zilizosalia kabla ya kutokomea.
Ofisi yao inafunguliwa baada ya saa 5 asubuhi.
Simu zao zote za huduma kwa wateja na zinazoonekana kwenye mtandao wao http://www.sasatel.co.tz/contact-us.html hazipatikani.
Wafanyakazi waliosalia wamewajibu wateja kuwa wana matatizo ya umeme na wangerekebisha ndani ya siku tatu tu lakini ni zaidi ya wiki sasa hakuna huduma ya internet.
Kinachoumiza zaid wamechukua malipo yangu ya bundle ya internet ya miezi miwili kwa ajili ya kibanda changu cha internet na hakuna dalili ya kurudi huduma yao. Ni zaidi ya kurudishana nyuma wakuu.
TCRA tusaidieni katika hili.