Kampuni 4 za mafuta zapewa masaa 24.

Kampuni 4 za mafuta zapewa masaa 24.

kampuni za oilcom,cameloil,bp na engen zimepewa masaa 24 kusitisha mgomo wao na kuanza kuuza mafuta kwa bei rasmi iliyotangazwa na ewura.endapo watakaidi amri,ewura imetishia kuziburuza mahakamani.wakati huo huo mheshimiwa zito kabwe ameshauri endapo kampuni hizi zitaendeleza mgomo,jwtz iingilie kati kwa kuvamia vituo vya mafuta kinguvu na kuuza mafuta kwa wananchi.
hapa ni nguvu ya umma tu ndio suluhisho basiiii
 
Mh. Mnyika kasema ana ushahidi unaothibitisha kwamba maafisa wa serikali wamehongwa. Leo muongozo kuhusu uthibitisho hakuna? Au asilimia kubwa ya waheshimiwa wabunge na mawaziri wa miongozo ya spika wanahusika?
Ushahidi wa Mnyika ni muhimu sana hasa hasa kwa jambo nyeti kama hili lililotikisa taifa.
 
pigeni kelele sisi twafuturu huku magogoni na mgeni wetu maaaalim kutoka somalia
 
Wenye vituo vya mafuta wana bahati wanaomiliki magari wastaarabu kidogo wanabaki kuongea tu ingekuwa ni Machinga vituo vyote vingechomwa moto au kuvamiwa. Lakini pale daladala ambazo sasa zimepungua barabarani zitakapoishia wengi wetu tutashindwa kuvumilia na machingas watashindwa kwenda sehemu zao za kazi - moto utawaka wauza mafuta waogope nguvu za umma! Wakati wao wanang'angania kukusanya shilingi zetu sisi tunasweat kuipata hiyo shilingi. Wandelee kugoma na serikali iache kuwanyang'anya leseni kwa lile tunalojua wapo ndani yao wenye interest zao - nguvu ya umma itachukua hatua, kaeni chonjo tunakuja.......
 
Sikubaliani na Zitto hiyo ni temporary soln, kifupi serikali ijipange nayo kupitia kampuni yake tuone nini kitatokea.
Hoja ya zito ina msingi wake hasa matumizi ya jeshi kwenye dharura. Pitia kwa kina majukumu ya jeshi (kama una fursa ya kujua) kisha jiulize maswali kwa nini rais ni amiri jeshi kama hakuna uhusiano wa jeshi na maisha ya raia. baada ya temporary solution then we tune to durable solution.
 
Sisi WADANGANYIKA ni MAFALA sana... Am sorry to say that!! Sirikali imeshachemka tunaona kabisaa na tunakaa tunaulizana eti why imekaa kimya while tunajua imekaa kimya kwanini(SABABU inawaaogopa wafanyabiashara wenzao wa Mafuta). TAfakari..... Chukua Hatua! Kunyoa au Kusuka! Boss yeye anatoa misaada ya Misosi tu! Futari/Mahindi!
 
Kampuni za OILCOM,CAMELOIL,BP na ENGEN zimepewa masaa 24 kusitisha mgomo wao na kuanza kuuza mafuta kwa bei rasmi iliyotangazwa na Ewura.Endapo watakaidi amri,Ewura imetishia kuziburuza mahakamani.Wakati huo huo mheshimiwa Zito Kabwe ameshauri endapo kampuni hizi zitaendeleza mgomo,JWTZ iingilie kati kwa kuvamia vituo vya mafuta kinguvu na kuuza mafuta kwa wananchi.

Vipi TPDC mbona wao hawaagizi na kusambaza, na hii TPDC tunajuwa wazi na ya Serikali ya Muungano (JMT). Je Serikali haioni hapo kuwa inakwepa majukumu yake na kuyakabidhi kwa watu binafsi?

WaTanzania lazima sasa mfikiri out of the box. Mtategemea uhisani mpaka lini?
 
Hoja ya zito ina msingi wake hasa matumizi ya jeshi kwenye dharura. Pitia kwa kina majukumu ya jeshi (kama una fursa ya kujua) kisha jiulize maswali kwa nini rais ni amiri jeshi kama hakuna uhusiano wa jeshi na maisha ya raia. baada ya temporary solution then we tune to durable solution.

BRAVO!! 100% Atamtoto akichelewa nyumbani au akiiba Unapiga kwanza then Unakaa nae na kuanza mpa somo la LIFE!
 
Mh. Mnyika kasema ana ushahidi unaothibitisha kwamba maafisa wa serikali wamehongwa. Leo muongozo kuhusu uthibitisho hakuna? Au asilimia kubwa ya waheshimiwa wabunge na mawaziri wa miongozo ya spika wanahusika?
Ushahidi wa Mnyika ni muhimu sana hasa hasa kwa jambo nyeti kama hili lililotikisa taifa.

kama ana ushahidi pasi na shaka kwanini asipeleke kwenye vyombo husika ili taratibu za hatua zichukue mkondo wake.

kama alisema kweli sio kutaka kujipandisha chati
 
naihurumia Tanzania inayouzwa kwa wanyonyaji huku tukiiona kwa kisingizio cha uwekezaji itakufa masikini na watu wake.

Hao wanyonyaji /wawekezaji wenye rangi nyeupe, ambao si ajabu kuwakuta pia wakijiita watanzania huku wakiwa na pasi za TZ na za mataifa mengine waliishaona TZ ndio jalala, shamba la bibi na ni nchi ambayo mgeni anaweza kuamua kufanya chochote atakacho kwa kisingizio cha uwekezaji huku selikali ikimtazama kwa kuwa serikali yetu haina meno yalishang'olewa yote enzi za mwalimu imebaki kibogoyo kutafuna haiwezi.

ingekuwa serikali ina meno unafikiri wangethubutu kugoma si wangejua tu siku wanayogoma kesho asubuhi hawana seseni ya kufanya biashara aghalabu na kutakiwa kuondoka inchini.

Pole Tanzania, Pole Watanzania. ukiangalia nchi nyingi ziliizoendelea serikali pia inafanya bishara kwa maslahi ya wananchi wake.
 
Back
Top Bottom