Uchaguzi 2020 Kampeni za mwaka huu zitaiachia nchi nyufa za chuki, ubaguzi, dharau kwa dini na viongozi wake, hasira. Tunahitaji muafaka wa kitaifa

Hawezi kuwa jiwe kwa sababu sifa ya jiwe ni kutokubadilika. Liko hivyohivyo enzi na enzi!!
 
Baada ya kufuatilia kampeni za mwaka huu hususan za Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuangalia serikali na Tume wanavyochezesha mchezo huu wa kampeni nashuhudiwa ndani ya nafsi yangu kuwa iwapo CCM itashinda au CHADEMA tutakuwa na miaka mitano iliyojaa

1. Chuki baina ya Wananchi na Serikali na Wanachama wa vyama vikubwa vya siasa. Chuki hii inaletwa na upendeleo wa wazi dhidi ya CCM na kuzuia watu kutoa hasira zao waziwazi badala yake wanaweka vinyongo moyoni

2. Ubaguzi. Maadili ya Uchaguzi yanakataza matumizi ya lugha za makabila wakati wa kampeni. Bahati Magufuli anajua lugha za makabila mengi ya kanda ya ziwa na ameishi au kufanya kazi mikoa hiyo kwa wakati fulani. Sasa kampeni zake kanda ya ziwa ni kisukuma, kihaya n.k halafu yuko live TBC. Anawaonyesha kuwa yeye ni mwenzao ni mtoto wao. Hili ni ubaguzi na Mwl. Nyerere alisema hii ni sawa na kula nyama ya mtu. Magufuli, Bashiru, Polepole n.k wote kanda ya ziwa.

3. Dharau kwa Dini na viongozi wake. Kugombea kwa Askofu Gwajima na sala na dua wanazotoa viongozi wa dini kwenye kampeni za CCM ambazo ziko live kila siku zinafanya wananchi wengi tunawadharau matokeo yake tutadharau dini na mwisho wa siku kikinuka hatutakuwa na wa Kumsikiliza maana dini na viongozi wake tutaziona kama vyama tu.

Aidha hakuna kiongozi wa dini hata mmoja ambae amekemea au kuonyesha sympathy na Tundu Lissu hadharani dhidi ya shambulio lake la September 2017. Matokeo yake viongozi wa dini wanaelemea upande wa wawashukiwa wa tukio.

4. Hasira ipo dhidi ya uonevu. Itazidi sana wakati wa kutangaza matokeo na itachochewa sana na walioshindwa.

5. Kupoteza imani na sheria na vyombo vinavyoisimamia. Kama unaongea kwa lugha za makabila, unapiga simu kuagiza barabara zitengenezwe wakati uko kwenye kampeni kinyume na sheria inavyotaka na hatua yoyote inayochukuliwa hata ya onyo na wewe ndio Mkuu wa nchi maana yake unawaonyesha watu kuwa sheria haina maana au ni ya wale sio yako hali ya kuwa wakati huu wenzako nao wanakuchukulia uko kama wao ni shida.

Sioni kwa sasa katika serikali, dini au kwenye vyama mtu anayeweza kuzungumza na Taifa kwa umoja wetu. Tukiendelea hivi naona miaka 5 ya mivutano bila kufanya maendeleo. Tunahitaji Muafaka wa Kitaifa wakati huu wa kampeni kabla ya Kura na kabla ya Matokeo. Sioni upendo kati ya Magufuli na Lissu. Mafahali wawili wakivutana nyasi ndio zitaumia.

TUNATAKA MUAFAKA WA KITAIFA BARA NA ZANZIBAR KABLA YA SIKU YA KURA. JUKWAA LA WAHARIRI WAMEANZA KWA KUWAKUTANISHA CHADEMA NA TBC SERIKALI NAYO IFUATE KUPITIA TDC
Policcm na Neccm ndio watakaovunja amani ya nchi hii , ng'ombe atachinjwa jinsi alivyolala ,hakuna kumpeleka kibla!! Policcm na nec wakitenda haki hakuna vurugu itkayotokea ila wakileta uhuni watapata wanachokitaka.

Viongozi wa Chadema ngazi ya jimbo washatoa tamko eg misungwi kwamba kuna vituo na wapiga kura hewa,kwahiyo janja ya NEC ishajulikana ,kila jimbo NEC watoe nakala ya matokeo kwa kila kituo na jumla yake ya jimbo iliflect kwenye nakala za mawakala yakienda tofauti lazima kinuke!! Hakuna upuuzi tena,tunatumia zaidi ya bil 600 kufanya uchaguzi halafu kumbe matokeo yapo mfukoni mwa NECCM si upuuzi huo? hizo b 600 si zingefanyie vitu vingine kama hamtaki uchaguzi huru? Mwaka huu mtajua hamjui,hakuna JANJA JANJA tena.
 
Nilisema na nitarudia...kwa namna ile ile Magufuli alivyosukumiziwa madaraka yaliyomzidi kimo, toka awali kabisa hakuona umuhimu wa kuwaomba radhi Watanzania kwa ushiriki wake katika kulifikisha taifa lilipofikia mwaka 2015.

Sio tu kwamba hakuona umuhimu wa kufanya hivyo, kwa kiburi cha ajabu alijifananisha na malaika aliyeshushwa tu kutoka sayari nyingine na kulikuta taifa lililopinda na lililo katika hali ya kusikitisha likihitaji mtu wa kulikomboa kama yeye.

Hakuishia hapo tu aliapa pia kuwalinda wote alioshirikiana nao kwa kipindi chote cha miaka zaidi ya ishirini kulifikisha taifa katika hali hiyo ya kusikitisha akiwataka walale bila hofu ya kuwajibishwa huku akidai kulinyosha taifa hilo.

Hakutaka ushiriki wala mapatano na wazalendo wa kweli ambao kwa miaka hiyo yote walikuwa wakipiga kelele wakati yeye pamoja na hao alioshirikiana nao wakineemeka kwa kutapanya rasilimali za taifa kama vile hazima mwenyewe.

Kwa miaka mitano aliyokaa madarakani alihakikisha anawanyamazisha wazalendo wote ambao hasa ndio walikuwa wahanga wakiteseka kwa hujuma zilizokuwa zikifanyika dhidi yao na genge lililotamba kuwa na hatimiliki ya taifa hili.

Katika miaka hiyo mitano kulikuwa kikundi kisicho rasmi cha wasiojulikana kilichotumika kuteka, kutesa na kuwapoteza wananchi ambao walikataa kuunga mkono juhudi hizo za kilaghai zilizoendeshwa kikatili kwa kivuli cha hapa kazi tu.

Na leo, kama vile kazinduka...

Katika wale waliolaghaiwa na hivyo kushawishika kuunga mkono juhudi hizo ovu, anatokea moja na bila hata kuwaomba radhi Watanzania waliopitia mateso makubwa ndani ya taifa lao, anatutaka tutafute muafaka na genge hilo...Benson Mramba, upo?
 
Tukubali tu kuwa mzee ndio anaanzisha hizi rafu wenzake wanamalizia.

Mzee anajisahau sana inapokuja swala la sheria na taratibu na kanuni mbali mbali za nchi. Kama viongozi wote wangekuwa na ujeuri wa kufanya vile wanavyojiskia bila kuheshimu au hata ka'aibu fulani kwenye sheria za nchi then sidhani kama taifa letu lingekuwa limesimama kama hivi.

Hili ni vema likazungumzwa na kukemewa wazi wazi pasipo kupiga chenga. Kwann tunakuwa ni watu wa kuonea haya au aibu kiongozi anapocheza na misingi ya taifa letu?!


Hebu tukemee hili na tukemee wazi wazi.
 
Usinilishe maneno. Mimi nilikuwa napingana na Mbowe na kikundi chake namna ya uendeshaji wa Chama. Wanachama walinielewa. Sasa habari za Mbowe nimefunga. Niko na agenda nyingine.
Mkuu, wewe si miongoni mwa walioshadadia kukamatwa kwa watu wanaovaa nguo iloandikwa "pray for Lissu"??
 
Baada ya kufuatilia kampeni za mwaka huu hususan za Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuangalia serikali na Tume wanavyochezesha mchezo huu wa kampeni nashuhudiwa ndani ya nafsi yangu kuwa iwapo CCM itashinda au CHADEMA tutakuwa na miaka mitano iliyojaa

1. Chuki baina ya Wananchi na Serikali na Wanachama wa vyama vikubwa vya siasa. Chuki hii inaletwa na upendeleo wa wazi dhidi ya CCM na kuzuia watu kutoa hasira zao waziwazi badala yake wanaweka vinyongo moyoni

2. Ubaguzi. Maadili ya Uchaguzi yanakataza matumizi ya lugha za makabila wakati wa kampeni. Bahati Magufuli anajua lugha za makabila mengi ya kanda ya ziwa na ameishi au kufanya kazi mikoa hiyo kwa wakati fulani. Sasa kampeni zake kanda ya ziwa ni kisukuma, kihaya n.k halafu yuko live TBC. Anawaonyesha kuwa yeye ni mwenzao ni mtoto wao. Hili ni ubaguzi na Mwl. Nyerere alisema hii ni sawa na kula nyama ya mtu. Magufuli, Bashiru, Polepole n.k wote kanda ya ziwa.

3. Dharau kwa Dini na viongozi wake. Kugombea kwa Askofu Gwajima na sala na dua wanazotoa viongozi wa dini kwenye kampeni za CCM ambazo ziko live kila siku zinafanya wananchi wengi tunawadharau matokeo yake tutadharau dini na mwisho wa siku kikinuka hatutakuwa na wa Kumsikiliza maana dini na viongozi wake tutaziona kama vyama tu.

Aidha hakuna kiongozi wa dini hata mmoja ambae amekemea au kuonyesha sympathy na Tundu Lissu hadharani dhidi ya shambulio lake la September 2017. Matokeo yake viongozi wa dini wanaelemea upande wa wawashukiwa wa tukio.

4. Hasira ipo dhidi ya uonevu. Itazidi sana wakati wa kutangaza matokeo na itachochewa sana na walioshindwa.

5. Kupoteza imani na sheria na vyombo vinavyoisimamia. Kama unaongea kwa lugha za makabila, unapiga simu kuagiza barabara zitengenezwe wakati uko kwenye kampeni kinyume na sheria inavyotaka na hatua yoyote inayochukuliwa hata ya onyo na wewe ndio Mkuu wa nchi maana yake unawaonyesha watu kuwa sheria haina maana au ni ya wale sio yako hali ya kuwa wakati huu wenzako nao wanakuchukulia uko kama wao ni shida.

Sioni kwa sasa katika serikali, dini au kwenye vyama mtu anayeweza kuzungumza na Taifa kwa umoja wetu. Tukiendelea hivi naona miaka 5 ya mivutano bila kufanya maendeleo. Tunahitaji Muafaka wa Kitaifa wakati huu wa kampeni kabla ya Kura na kabla ya Matokeo. Sioni upendo kati ya Magufuli na Lissu. Mafahali wawili wakivutana nyasi ndio zitaumia.

TUNATAKA MUAFAKA WA KITAIFA BARA NA ZANZIBAR KABLA YA SIKU YA KURA. JUKWAA LA WAHARIRI WAMEANZA KWA KUWAKUTANISHA CHADEMA NA TBC SERIKALI NAYO IFUATE KUPITIA TDC

Kwanza ni kujua hali yako,maneno haya ni ukweli mtupu na hua mwanzo wa kutengeneza utengano wa kitaifa, hasa kama hakuta kuwa na matayarisho ya kukumbatiana.

Ila mnaniangusha Kilimanjaro, hasa Rombo, Hai na Vunjo safari hii mmeamua kuungama, nini kipya tena? Bi mkubwa nikizungumza nae na uncles wananiambia Lwamungo Sinde ya kijani. Nipashe kama kuna mpya.

Kila nikipata taarifa za huko napungukiwa ufahari na kuutingisha ujasiri wangu. Karibu sana na siku njema.
 
Mungu ashukuriwe kwa wewe kurudiwa na akili timamu umeongea jambo la msingi sana.

Tunaofahamu undani kidogo huyu yupo sawa tuu, ila Kaka alimpiga kofi la keleb akateleza, hivi anajitafuta tuu anarudi huyo, na mabadiliko yeyote ya juu kuna nondo za ukweli tutaungana kwa kurudi nyumbani. Siasa hizo ni suala la muda tuu.
 
Back
Top Bottom