Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Nijuavyo mimi, kampeni rasmi za Urais na Ubunge, zitaanza rasmi Tarehe 20 mwezi ujao. Katika pita pita yangu huku na kule, nimetua mjini Dodoma na kushuhudia mji mzima wa Dodoma, umeshehenezwa na mabango rasmi ya CCM yenye picha kubwa za JK na ujumbe mbalimbali ukihimiza Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Mabango haya ni mabango rasmi, yaani sio kazi ya bahati mbaya na yamebandikwa mji mzima hali inayopelekea kufuatwa kwa sheria taratibu zote na kanuni zinazotawala uchaguzi.
Swali langu ni jee hii sio CCM inacheza rafu?. Kama ni rafu hivi kweli CCM inaweza kucheza rafu namna hii wazi wazi huku tume ya uchaguzi imewanyamazia?.
Japo nina interest kubwa na harakati za kisiasa humu nchini, natamani sana siasa za fair playing ground, hivyo hiki kinachofanywa na CCM, na kunyamaziwa na Tume ya Uchaguzi, nadhani sio fair play.
Nauliza nini kifanyike au kinaweza kufanyika ili CCM licha ya kushika mpini, lakini pia isicheze rafu?.
Nijuavyo mimi, kampeni rasmi za Urais na Ubunge, zitaanza rasmi Tarehe 20 mwezi ujao. Katika pita pita yangu huku na kule, nimetua mjini Dodoma na kushuhudia mji mzima wa Dodoma, umeshehenezwa na mabango rasmi ya CCM yenye picha kubwa za JK na ujumbe mbalimbali ukihimiza Chagua CCM, Chagua Kikwete.
Mabango haya ni mabango rasmi, yaani sio kazi ya bahati mbaya na yamebandikwa mji mzima hali inayopelekea kufuatwa kwa sheria taratibu zote na kanuni zinazotawala uchaguzi.
Swali langu ni jee hii sio CCM inacheza rafu?. Kama ni rafu hivi kweli CCM inaweza kucheza rafu namna hii wazi wazi huku tume ya uchaguzi imewanyamazia?.
Japo nina interest kubwa na harakati za kisiasa humu nchini, natamani sana siasa za fair playing ground, hivyo hiki kinachofanywa na CCM, na kunyamaziwa na Tume ya Uchaguzi, nadhani sio fair play.
Nauliza nini kifanyike au kinaweza kufanyika ili CCM licha ya kushika mpini, lakini pia isicheze rafu?.