Kampeni ya kuikataa Vodacom

We tongoza yule binti ya Jiwe Jeska uone.
 
Kususia kwako hakuna athari zozote ni sawa na kutishia kuchota ndoo moja ya maji kwenye bahari eti utaikausha bahari.
 
Mimi voda waliniibia tuzo point zaidi ya 3,400 nikaona hawa jamaa sasa wamezidi. Nikarekodi kwenye simu nyingine taarifa zangu zote. Nikawapigia mara 3 nakuwapa ushahidi hata hawakunisaidia. Baada ya kuchukia nikawambia nitapeleka suala hili kwa MD wenu asiponisaidia nitaenda tcra. Wakanijibu usiende huko tutakurudishia hela yako jumatatu maana niliwapigia jumapili. Ile jumatatu badala ya kurekebisha wakafuta taarifa zangu zote wakidhani wameniweza bila kujua taarifa nimezihamishia kwenye simu nyingine! Sasa nafikiri kampuni imeajiri vijana wasio waaminifu wanao idharirisha. Mimi mambo haya hayajaisha, sema naishi mbali, siku nikija dar nakuja na ushahidi wangu kwa wahusika hadi kieleweke! Hawa watu msiwaamini sana, muwe nanyinyi mnarekodi taarifa zao bila hivyo mtapigwa changa la macho; 0756 426247.
 
Kuna mambo unaweza kuwa unayajua na kuna mambo unaweza kuwa hauyajui,
Kuna personal matter na public matter,
Pia kuna kufikiri kabla ya kutenda,
Pia kuna kujutia maamuzi,

Nakushauri jaribu sana kuangalia tatizo ulilonalo kwa undani zaidi kabla haujajihesabia haki
 
yajayo yanafurahisha je uko tayari?
 
Lazima mjue Rostam karudi nchini na ni mwanaccm.
Voda tanzania inamhusu.
La msingi ni kuomba msaada wa kisheria kuishtaki kampuni ya vada Tz kwa mmiliki mkuu kanda ya afrika.
Ni makosa sana kumwamini fisi kulinda bucha.
 
KANUNI NA MASHARTI YA MTUMIAJI WA VODACOM

6.3 Vodacom haisambazi taarifa zako binafsi zozote kwa upande wa tatu isipokuwa kama tumeombwa nawe au imetakiwa kisheria kufanya hivyo na kwa amri ya serikali. Kwa ajili ya kuepuka shaka na kufanya kazi kwa uwazi, Vodacom inaweza kutakiwa kuonyesha taarifa binafsi kukidhi mahitaji yoyote ya kisheria au udhibiti wa sheria zilizopo.
6.4 Vodacom ina haki ya kurekebisha au kubadilisha taarifa hii ya Usalama na Usiri wakati wowote ili kuendana na sheria mpya ya usiri.
6.5 Kusimamia au kurekodi mawasiliano yako kama vile miito au ujumbe mfupi wa maandishi kunaweza kufanyika kama inavyotakiwa kisheria au kwa madhumuni ya kikazi katika kiwango kinachoruhisiwa kwa agizo la sheria. Hata hivyo, katika hali hizi, hatutaonyesha taarifa ambazo zingeweza kutumika kukutambulisha.
 
Mkuu naomba kueleweshwa tafadhari. Mimi situmi msg toka jana usiku mpaka sasa ila calls napokea nashindwa kuelewa shida nini. Usikute linahusiana na hiki ulichosema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…