Siku zingine jitahidi uwe unatumia vyema Akili zako hasa ukija hapa The Home of Great Thinkers tafadhali. Hilo ambalo unadhani limefanywa tu na huo Mtandao ambalo umekuja nalo kwa Mhemko hapa pia huwa linafanya hata na Mitandao mingine mikubwa kama Tigo na Airtel na Mifano yake ipo wazi isipokuwa tatizo Kubwa la Watanzania si Wafuatiliaji wazuri wa mambo, hamjui Kutunza Kumbukumbu na ni Watu wanaopenda Kukurupuka na si ajabu ndiyo maana huko nje tunadharaulika mno na waliotuzidi Akili.
Ungekuwa unajua ya kwamba haya Makampuni yote ya Simu nchini yapo chini ya Serikali na kwa Msaada mkubwa wa Kiudhibiti kutoka TCRA wala usingekuja na huu Uzi wako ulio na Hoja Nyepesi kama siyo ya Kipuuzi. Halafu msisahau ya kwamba kuna hatua zingine zinaweza zikawa zinachukuliwa dhidi ya Mtu kwa ajili ya Usalama wa Taifa letu na hata Sisi Wananchi wake ila bahati mbaya sasa hivi kila Jambo la Muundo huo kama uliomtokea huyo Mtu likitokea haraka sana lawama zenu mnazielekeza katika Mamlaka ila huwa hamtaki Kujua ya upande wa Pili.
Namalizia tu kwa Kukuambia kuwa KUNA UNAYOYAJUA NA YALE USIYOYAJUA na msije Kuona Watu wanakurupuka tu.