Kampala - London - Brussels: Tumejifunza nini kama Taifa?

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
1,093
1,726
Juma hili linalomalizika, serikali ya Uganda Chini ya Rais Museveni imepata wakati mgumu mbele ya mabunge mawili - Bunge la Uingereza na Bunge la Ulaya.

Vyombo vya habari na mitandao imeonyesha mijadala motomoto ikiishutumu serikali ya Uganda kwa yafuatayo:
-Kukiuka haki za binadamu
-Kuwakamata na kuwatesa wapinzani
-Kuzuia uhuru wa kujieleza, kukusanyika na kutoa maoni
-Kutumia bunge vibaya kwa kutunga sheria zinazopingana na katiba
-Kutesa, kuua na kufanya ukatili

Hitimisho lao likawa ni:
-Uganda iko chini ya mfumo wa kidikteta rasmi
-Hali hiyo haikubaliki na jumuia ya kimataifa
-Wito wa kuiondoa madarakani kwa njia zozote.

Sipendi nchi za Magharibi kuingilia uhuru wa nchi za Kiafrika, lakini sipendi zaidi viongozi wa nchi za kiafrika kuwatesa watu hao kuliko walivyoteswa na wakoloni. Tanzania tumejifunza nini?

Kwanza nikiri wazi, yanayosemwa kutendwa na serikali ya Uganda kwa wananchi wa Uganda, hayafikii nusu ya yale tunayotendewa na serikali yetu hapa Tanzania. Mbunge Lusinde ameyaanika vizuri katika kampeini za Monduli na Ukonga. Hatuhitaji ushahidi kuonyesha kuwa serikali inaliendesha bunge; inatesa wapinzani, inaua wapinzani, na kusimamia ukiukwaji wa haki za binadamu. Hayakusemwa na wapinzani, yamesemwa na Mbunge wa CCM akiwatumia Spika, waziri Mkuu na mawaziri kama mashahidi wake.

Kinachoonekana kukosekana Tanzania ni utashi wa wanasheria wetu kuyapeleka haya katika vyombo vya kimataifa ili yafahamike. Vyama vya upinzani, wana harakati, na media zetu, ama hawana uwezo, au hawana utashi na uthubutu wa kuyafanya waliyofanya watu wa Uganda. Kuna tweet inazunguka kwenye mitandao kuwa Washington imemfutia visa Museveni na mawaziri wake, na kijana wake anayesoma hapa anarudishwa Kampala. Sipendi haya yatufike. Nimemsikia balozi wetu mmoja wa nchi za Magharibi akisema "wamechoka" kutetea mambo yasiyokuwa na msingi!
 
.
IMG-20180914-WA0097.jpg
 
Haraka haraka hazina baraka, uzuri wa mambo yanavyoendelea hayana kificho. Ule uchaguzi wa Kinondoni hata Ubalozi wa Marekani ulikiri kuwa haukuwa halali.

Yale ya Korogwe ni aibu tupu, na sasa hivi Vitisho vinaendelea kuhakikisha Waitara anatangazwa mshindi Ukonga.

Dunia inafahamu ni kwanini Tundu Lissu yuko Ubeligiji na viongozi wa upinzani wana kesi ya mauwaji ya Akwilina.
Time is getting closer
 
Baija Bolobi ,

..labda CDM nao wakashitaki kwa nchi wahisani.

..bila CCM kufinywa kidogo na nchi wahisani nina wasiwasi hakuna kitakachobadilika.

..kama ni misaada ya kimaendeleo inaweza kuletwa kupitia TAASISI ZISIZO ZA KISEREKALI / NGO.
 
Baija Bolobi ,

..labda CDM nao wakashitaki kwa nchi wahisani.

..bila CCM kufinywa kidogo na nchi wahisani nina wasiwasi hakuna kitakachobadilika.

..kama ni misaada ya kimaendeleo inaweza kuletwa kupitia TAASISI ZISIZO ZA KISEREKALI / NGO.
===

Joka Kuu

Nasita kukubaliana nawe kuwa CDM wakashtaki kwa nchi wahisani. Hili suala ni zaidi ya CDM na CCM. Haki zinazokiukwa ni za watanzania. Mimi siyo CDM na wala CCM. Chama changu ni Tanzania. Nimekuwa nawe Joka Kuu kwa muda mrefu na ninaweza kukutetea kuwa wewe si CCM wala CDM. Viangazi na masika vimepita vingi nikikuona hivyo hata kama unaweza kuwa una kadi yako mfukoni!

Uchama unaoendelea hapa nchini kwa sasa ni wa hatari kuliko utumwa na ufisadi tunaodai tunapigana nao. Kwa jina la chama, watu wanaiba, wasio raia wanatutawala, biashara chafu inaendelea, na maovu yote yanavumiliwa ikiwa mtu ni wa chama fulani. There is ideological cleansing and literal genocidal manifestation. Ni suala letu, si la CDM. Kuna siku CDM wanaweza kushika dola wakafanya haya haya.
 
Kinachoonekana kukosekana Tanzania ni utashi wa wanasheria wetu kuyapeleka haya katika vyombo vya kimataifa ili yafahamike. Vyama vya upinzani, wana harakati, na media zetu, ama hawana uwezo, au hawana utashi na uthubutu wa kuyafanya waliyofanya watu wa Uganda. K
Mimi nadhani vyama vya upinzani hapa kwetu vinahitaji mbinu mpya. Sasa hivi ni kama wameishiwa nguvu kabisa, na wala hawajui wafanye nini.
Walipoambiwa sasa siasa basi hadi uchaguzi mwingine, na kupewa misukosuko kadhaa, wakanywea kabisaa.
Mabaya wanayofanyiwa, na wao wasijue namna ya kuyatangaza yafikie wananchi na dunia, wanapoteza fursa ya kuyamlika hayo mabaya na kuyatumia kwa manufaa yao na nchi kwa ujumla.
Nakumbuka waliwahi kwenda ubalozi wa Ulaya wakati fulani. Hatujui waliambiwa nini huko! Labda waliambiwa hawataki kuwaona huko tena au kusikia lolote linalowahusu.
Tunavyokwenda sasa ni kama tunaelekea kwenye uchaguzi wa 2020 utakaomaliza uwepo wa vyama hivi. Sijui kama wao hawaamini hivyo na kwa sababu gani wasiamini hivyo. Nikama wamedungwa sindano ya ganzi, jinsi wanavyokwenda sasa.
 
Uchama unaoendelea hapa nchini kwa sasa ni wa hatari kuliko utumwa na ufisadi tunaodai tunapigana nao. Kwa jina la chama, watu wanaiba, wasio raia wanatutawala, biashara chafu inaendelea, na maovu yote yanavumiliwa ikiwa mtu ni wa chama fulani. There is ideological cleansing and literal genocidal manifestation. Ni suala letu, si la CDM. Kuna siku CDM wanaweza kushika dola wakafanya haya haya.
Absolutely brother, these are Great Thinker's analytical thoughts! Hii para niliyo ku quote imebeba points muhimu sana juu ya tatizo letu halisi na hatri tunayopitia kama nchi kwa sasa.You have rightly and precisely phrased it! Kinachoendelea kwenye medani ya siasa is purely ideological cleansing

Watu waliopo ndani ya mfumo hawalioni hili? Seriously!? Tetesi kua wasio raia wanatuongoza na wengine wamepenyezwa katika sehemu sensitive za mifumo yetu kiulinzi zinasikika kila mahali ingawa binafsi siziamini sababu sina ushahidi wa hilo.Lakini kama kutakua na chembe ya ukweli katika hilo then hiyo ni patriotc suicidal na itakua kunashida katika muundo, mafunzo na sheria zinazoongoza taasisi zilizopewa jukumu la kuhakikisha very existence of our nation as a sovereign state
 
Absolutely brother, these are Great Thinker's analytical thoughts! Hii para niliyo ku quote imebeba points muhimu sana juu ya tatizo letu halisi na hatri tunayopitia kama nchi kwa sasa.You have rightly and precisely phrased it! Kinachoendelea kwenye medani ya siasa is purely ideological cleansing

Watu waliopo ndani ya mfumo hawalioni hili? Seriously!? Tetesi kua wasio raia wanatuongoza na wengine wamepenyezwa katika sehemu sensitive za mifumo yetu kiulinzi zinasikika kila mahali ingawa binafsi siziamini sababu sina ushahidi wa hilo.Lakini kama kutakua na chembe ya ukweli katika hilo then hiyo ni patriotc suicidal na itakua kunashida katika muundo, mafunzo na sheria zinazoongoza taasisi zilizopewa jukumu la kuhakikisha very existence of our nation as a sovereign state

Ndugu yangu wala siyo siri tena. Siku hizi mtu yeyote aliye na uraia tata, biashara chafu, deni baya na kitapeli kwa benki, anakimbilia kwenye chama chenye kinga. Wachafu wote wamehama toka kote walikokuwa na kuhamia kwenye chama chenye kinga. Ukiona aliye kwenye chama chenye kinga anatumbuliwa ujue hicho ni kisasi hakuunga mkono mambo fulani. Bila kujua, CCM imevisafisha vyama vingine na watu wenye mambo tata.

Pili, ukweli uko wazi, mawaziri wawili si raia wa Tanzania. Walijadiliwa katika kamati ya ulinzi na usalama ya bunge, na baadaye kamati ikapigwa STOP likaisha. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara si raia na uhamiaji walichunguza na kuthibitisha. Walipigwa STOP likaisha. Wabunge watatu kutoka Manyara, Kagera na Shinyanga si raia. Uhamiaji walipigwa STOP wasigusie jambo hilo. Tuna wanajeshi na polisi kadhaa wa vyeo vya juu na wengine ni waambata katika balozi zetu, si raia hawaguswi. Katibu Mkuu wa Chama chenye kinga uraia wake unalalamikiwa mpaka na mkewe!

Badala yake, watu wenye mawazo huru kama mmoja wa wamiliki wa mtandao huu, ndio wanaohojiwa uraia wao.
 
Mimi nadhani vyama vya upinzani hapa kwetu vinahitaji mbinu mpya. Sasa hivi ni kama wameishiwa nguvu kabisa, na wala hawajui wafanye nini.
Walipoambiwa sasa siasa basi hadi uchaguzi mwingine, na kupewa misukosuko kadhaa, wakanywea kabisaa.
Mabaya wanayofanyiwa, na wao wasijue namna ya kuyatangaza yafikie wananchi na dunia, wanapoteza fursa ya kuyamlika hayo mabaya na kuyatumia kwa manufaa yao na nchi kwa ujumla.
Nakumbuka waliwahi kwenda ubalozi wa Ulaya wakati fulani. Hatujui waliambiwa nini huko! Labda waliambiwa hawataki kuwaona huko tena au kusikia lolote linalowahusu.
Tunavyokwenda sasa ni kama tunaelekea kwenye uchaguzi wa 2020 utakaomaliza uwepo wa vyama hivi. Sijui kama wao hawaamini hivyo na kwa sababu gani wasiamini hivyo. Nikama wamedungwa sindano ya ganzi, jinsi wanavyokwenda sasa.
===

Ndugu Kalamu

Kwisha kwa upinzani ni kwisha kwako na mimi tunaoandika haya. Unandika kana kwamba hili ni tatizo la vyama vya upinzani. Hili si lao ni letu kama taifa. Kimsingi hata CCM hili ni lao kwa sababu CCM ya sasa si ya wanachama tena, ni ya Mwenyekiti na Katibu wa Itikadi Polepole. Nashauri tuache kuona kuwa hili ni la wapinzani waliopigwa ganzi au watakaokwisha mwaka 2020. Kwisha kwa upinzani ni kwisha kwa fikra huru katika taifa. Taifa lisilofikiri au lisilo na uhuru wa kufikiri, hakuna anayelitamani.
 
Ndugu yangu wala siyo siri tena. Siku hizi mtu yeyote aliye na uraia tata, biashara chafu, deni baya na kitapeli kwa benki, anakimbilia kwenye chama chenye kinga. Wachafu wote wamehama toka kote walikokuwa na kuhamia kwenye chama chenye kinga. Ukiona aliye kwenye chama chenye kinga anatumbuliwa ujue hicho ni kisasi hakuunga mkono mambo fulani. Bila kujua, CCM imevisafisha vyama vingine na watu wenye mambo tata.

Pili, ukweli uko wazi, mawaziri wawili si raia wa Tanzania. Walijadiliwa katika kamati ya ulinzi na usalama ya bunge, na baadaye kamati ikapigwa STOP likaisha. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara si raia na uhamiaji walichunguza na kuthibitisha. Walipigwa STOP likaisha. Wabunge watatu kutoka Manyara, Kagera na Shinyanga si raia. Uhamiaji walipigwa STOP wasigusie jambo hilo. Tuna wanajeshi na polisi kadhaa wa vyeo vya juu na wengine ni waambata katika balozi zetu, si raia hawaguswi. Katibu Mkuu wa Chama chenye kinga uraia wake unalalamikiwa mpaka na mkewe!

Badala yake, watu wenye mawazo huru kama mmoja wa wamiliki wa mtandao huu, ndio wanaohojiwa uraia wao.

Mkuu humu jukwaani ndio sehemu ya kuweka mambo wazi, kama unaogopa kutaja jina la mtu taja hata nafasi yake. Mfano waziri wa wizara fulani, mbunge wa jimbo fulani. Hii tabia ya kukalia kimya haya mambo ni hatari. Mfano umetaja katibu mkuu wa chama chenye kinga wote tumeelewa. Huku mitandaoni ndio mahali tunaweza kujadili kwa uwazi kuliko sehemu yoyote kwa sasa hapa nchini.
 
Ndugu yangu wala siyo siri tena. Siku hizi mtu yeyote aliye na uraia tata, biashara chafu, deni baya na kitapeli kwa benki, anakimbilia kwenye chama chenye kinga. Wachafu wote wamehama toka kote walikokuwa na kuhamia kwenye chama chenye kinga. Ukiona aliye kwenye chama chenye kinga anatumbuliwa ujue hicho ni kisasi hakuunga mkono mambo fulani. Bila kujua, CCM imevisafisha vyama vingine na watu wenye mambo tata.

Pili, ukweli uko wazi, mawaziri wawili si raia wa Tanzania. Walijadiliwa katika kamati ya ulinzi na usalama ya bunge, na baadaye kamati ikapigwa STOP likaisha. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara si raia na uhamiaji walichunguza na kuthibitisha. Walipigwa STOP likaisha. Wabunge watatu kutoka Manyara, Kagera na Shinyanga si raia. Uhamiaji walipigwa STOP wasigusie jambo hilo. Tuna wanajeshi na polisi kadhaa wa vyeo vya juu na wengine ni waambata katika balozi zetu, si raia hawaguswi. Katibu Mkuu wa Chama chenye kinga uraia wake unalalamikiwa mpaka na mkewe!

Badala yake, watu wenye mawazo huru kama mmoja wa wamiliki wa mtandao huu, ndio wanaohojiwa uraia wao.
Ikiwa hayo usemayo ni kweli mkuu then the future of our nation is so dull! Hizo orders za kupiga stop uchunguzi wa mambo ya msingi na nyeti kama kweli zipo basi zitakua zinatolewa na ama kikundi cha watu wachache sana au pengine mtu mmoja tu! Ni akina nani hao!?

Haiwezekani mambo hayo (nasisitiza tena kama yapo) yana blessings za Chama Tawala kama taasisi au 'The System'. Inawezekana watu wanamuaminisha Kiongozi/Mtawala wa ngazi fulani kua nguvu zake baada ya Mungu ni yeye! Labda watu fulani wa mfumo wanamuaminisha au ndio kanuni za utumishi wa nafasi yake kwamba kama vile akitakacho Mungu ndio kinakua na yeye kwenye nchi ni hivyohivyo, akitakacho ndio kitafanyika kiwe kizuri au kibaya, kiwe sahihi au makosa na wala hahojiwi!

Na kama ni kanuni au mfumo ndio uko hivo, hapa tatizo ni kubwa zaidi kuliko kulaumu personalities. Kama kuna kiongozi ambaye sheria kanuni na taratibu zimempa nafasi ya uungu basi tunayoyapitia ni matunda ya maamuzi hayo maana kila kitu kinafanyika kwa discretion yake kwa mandate aliyopewa na sheria hizo. Inamaana hata siku akija mtawala kutoka chama kingine anaweza kufanya the same kama hatutabadilisha angalau mifumo yetu (maana kubadilisha katiba ni mfupa mgumu)
 
Mkuu humu jukwaani ndio sehemu ya kuweka mambo wazi, kama unaogopa kutaja jina la mtu taja hata nafasi yake. Mfano waziri wa wizara fulani, mbunge wa jimbo fulani. Hii tabia ya kukalia kimya haya mambo ni hatari. Mfano umetaja katibu mkuu wa chama chenye kinga wote tumeelewa. Huku mitandaoni ndio mahali tunaweza kujadili kwa uwazi kuliko sehemu yoyote kwa sasa hapa nchini.
Naunga mkono hoja
 
Mleta mada umesema yanayofanyika Uganda kwa Tz hata nusu hayafiki,alafu kwenye hitimisho unaomba tena tusifikwe na yanayomkuta Mseveni.
 
Mkuu humu jukwaani ndio sehemu ya kuweka mambo wazi, kama unaogopa kutaja jina la mtu taja hata nafasi yake. Mfano waziri wa wizara fulani, mbunge wa jimbo fulani. Hii tabia ya kukalia kimya haya mambo ni hatari. Mfano umetaja katibu mkuu wa chama chenye kinga wote tumeelewa. Huku mitandaoni ndio mahali tunaweza kujadili kwa uwazi kuliko sehemu yoyote kwa sasa hapa nchini.
==

Mkuu Mwakijembe, nikitaja majina nakuhakikishia uzi huu utafungwa mara moja. Hata kwa haya niliyosema, uzi huu unafungwa hivi punde. Naenda kusali, nikirudi nitakuta ama umefungwa au au hakuna anayechagia. Diabolic indeed.
 
Mleta mada umesema yanayofanyika Uganda kwa Tz hata nusu hayafiki,alafu kwenye hitimisho unaomba tena tusifikwe na yanayomkuta Mseveni.
==

Yeah umenisoma vizuri. Yanayofanyika huko ni madogo kuliko ya kwetu lakini hatua anazochukuliwa Mseveni ni kubwa kuliko anayofanya ukilinganisha na ya kwetu. Siombei yatufike kwa sababu hapa tuna tabaka kubwa la watu wasiojua wala kuota namna ya kuishi nje ya madaraka. Taifa litakumbwa na kihoro. Ni sawa na kuwa na mtoto mtundu, lakini yakimpata makubwa unasikitika kama mzazi.
 
==

Yeah umenisoma vizuri. Yanayofanyika huko ni madogo kuliko ya kwetu lakini hatua anazochukuliwa Mseveni ni kubwa kuliko anayofanya ukilinganisha na ya kwetu. Siombei yatufike kwa sababu hapa tuna tabaka kubwa la watu wasiojua wala kuota namna ya kuishi nje ya madaraka. Taifa litakumbwa na kihoro. Ni sawa na kuwa na mtoto mtundu, lakini yakimpata makubwa unasikitika kama mzazi.
Upo sawa
 
Kinachoonekana kukosekana Tanzania ni utashi wa wanasheria wetu kuyapeleka haya katika vyombo vya kimataifa ili yafahamike. Vyama vya upinzani, wana harakati, na media zetu, ama hawana uwezo, au hawana utashi na uthubutu wa kuyafanya waliyofanya watu wa Uganda. Kuna tweet inazunguka kwenye mitandao kuwa Washington imemfutia visa Museveni na mawaziri wake, na kijana wake anayesoma hapa anarudishwa Kampala.
Si utoke uyaseme hayo unayoyajua dhidi ya utawala wa Tanzania? Unadhani ni nani atasikiliza hisia tu na madai yako ya kufkirika? Watu (akina Ansert Ngurumo na wenzake) wanakaa nyuma ya keyboard na kuzalisha uongo wakifikiri hizo ndio siasa za kuimarisha upinzani kumbe bure kabisa. Wamepotea! Tanzania is the heaven of peace.
 
Back
Top Bottom