Kamati ya Ngwilizi yawatia hatiani Prof. Muhongo na Eliakim Maswi, yawasafisha Zitto na wenzake!

Yaani yule Mh. GF wa Muhando alivyokuwa anatuzungukia tumtetee Muhando na kumkandamiza Maswi si la kweli? Yaani Mh. Kabwe alivyohamasisha wanakamati na wanabodi kupinga Muhando alichukuliwe hatua si kweli?
Sote tunakutana huko mjengoni siku hiyo: Tuna akili timamu na hakuna haja ya kuoneana haya kuwalinda mafisadi na kuwachafua viongozi wachache ambao hakika tunaona wanajitahidi kuajibika kwa nafasi walizopewa.

Swali la msingi ni hili: Ni namna gani bila kuacha mashaka yoyote (approach & methodological) kamati ilijilidhisha kuwa hakukuwa na jaribio au utoaji au upokeaji wa rushwa wowote. Kumbuka kuwa kamati ilikuwa inafanya kazi yake baada ya tukio kufanyika na kwamba rushwa hutolewa au hujaribiwa kutolewa katika mazingira ya usiri. Kama ni kutokana na mahojiano tu, Je mlitegemea kuwa Mbuge mwizi, fisadi au kuwadi wa mafisadi aje kwenu aseme mimi nilipokea rushwa kama alinyamaza kimya Bungeni siku hiyo? Kama watu wananyea kazi lakini hakuna anayestep down mwenyewe utategemea mla rushwa afike kwenye Kamati na kujisema mwenyewe? You have got to stop being naive!

1. Kama kweli kamati ilitakiwa kufanya kazi ya uchunguzi wa jinai, mlitakiwa kuangalia na kuchambua kwa undani juu ya mazingira, mfano: Wizara imemkuta CEO wa TANESCO na ukiukaji mkubwa wa kiuendeshaji na kwa kupitia Bodi yake imeamliwa asimame kazi kupisha uchunguzi halafu anakuja mwenzetu Mh. Kabwe anajitahidi kwa nguvu zote kuzuia hilo akishilikiana na mpenzi wa Mhando je hilo nayo ni siri? Je kamati ilikwenda deep kujiuliza wale Waarabu na wahindi waliokatiwa ulaji na ufisadi wa kusuply mafuta waliojaa Dodoma na wakawa wanazunguka na baadhi ya wabunge na ilipokaribia siku ya bajeti ya Nishati na Madini wakawa restless ni kwa nini?

2. Je kamati iliwasiliana na makampuni ya simu na kujaribu kutrack jinsi mazungumzo yalivyokuwa siku hizo kati ya CEO TANESCO- Mwenyekiti wa Bodi- wale wabunge wawili (dada zangu na wengine walitajwa humu) akiwemo Mh. Kabwe?

3. Kwa vile kamati ilikuwa inashughulikia jambo nyeti ambalo lingekuja kuleta ubishi kama ambavyo tunaona sasa, kwa nini hamukuhusisha makachero wenye uzoefu wa ku- interrogate watu wenye tuhuma za jinai hata wangekuwa ni wa kutoka nje ili kazi hiyo iwe independent nay a uhakika kweli. Kuwa na Wanasheria t u haitoshi tena kama ni wa aina ya Gosbert Blandes ambaye alisemwa toka mwanzo kuwa si msafi kimaadili mlitegemea tushangae matokeo ya kuwalinda mafisadi?

Mnafikiri ingemfaa nini mtu kama huyu Prof. Sospeter mwenye hadhi yake na kusifika duniani ambaye ndio kwanza ameteuliwa uwaziri na Rais na ni kikao chake cha kwanza aamuwe tu kuwazushia Wabunge au kuwadanganya juu ya jambo ambalo halikuwepo. Na ikimbukwe kuwa hata kabla ya kutoa hotuba yabajeti ya Wizara, hawa viongozi (Maswi na Wizara kwa ujumla walipokelewa vyema kwa kushangiliwa na wabunge wengi wakati wa utambulisho na wakati Waziri anakwenda kusoma hotuba.

Siamini haya yanayosemwa mpaka nishuhudie mwenyewe Spika akisoma maneno hayo kwamba Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara ndiwo ‘wamekutwa na hatia’ tuone. Maana hii itathibisha hakika kuwa nchi yetu ina mtandao mkubwa wa kutaka mafisadi waendelee kupeta na yeyote anayejaribu kupambana nao lazima ageuziwe kibao. Nina wahakaishia kuwa hakika Bunge litagawanyika, tutakuwepo tusiokubali kutumika kuwakuwadia mafisadi kutuibia rasilimali zetu.

Nami nakubaliana na aliyetoa wazo kuwa Waziri asikubali kabisa kuomba msamaha kwa jambo ambalo hana kosa. Sisi tunasema Wizara iendelee kuboresha miundo mbinu umeme usikatike katike (mnakumbuka hao mafisadi walitabiri kuwa baada tu ya bajeti nchi yote ingeingia gizani lakini sasa tumeona hakuna mgao isipokuwa TANESCO wakikaza butu kufanya matengenezo yanayopaswa tutapata umeme wa uhakika.
 
hii inchi imeshafilisika kimaadili, mfano reli iliyotakiwa kuanza usafirishaji dar es salaama mpaka sasa hakuna taarifa zake, na mnasema mwakyembe sio mzembe, ukishakuwa ccm we ni tatizo, hata dr. slaa akihamia ccm atakuwa kama wao tu
 
Bunge letu ni bunge la kishabiki,wabunge wengi wanauwezo mdogo sana wa kufikiri na kutafakar mambo na walichoamua sasa ni kuwa na chuki binafsi na wabunge wenye upeo mkubwa kama akina Zitto Kabwe ili kulazimisha akili za kina zitto zifanane na zao.
 
Tanganyika ya wadanganyika, hizo nguzo zinazotolewa na kupelekwa Mombasa na kurudi nazo wamezingelea au wameishia kubwabwaja tu kuhusu kanuni na sheria za manunuzi? Tangu mwanzo tulijua kuwa walikiuka hizo kanuni za kifisadi lakini kwa maslahi mapana ya umma. Bei ya kulipia nguzo moja ya umeme ilikuwa shilingi ngapi kabla ya Maswi na Profesa kuingia wizarani na sasa ni shilingi ngapi?
Kamati ya Ngwilizi, huyu ambaye ana hekaru kule Lushoto pamoja na Ben? I will be the last to trust them.

zats gud, kama na we umegundua hilo mkuu. Tulia vivyo hivyo kuna "mdau" atakuja "kutililika" humu hivi karibuni labda abaniwe na mods.
Ts a matter ov collecting data.
 
Me nilijua ZITTO kama kapiga pesa kama baadhi ya WANACDM walivyo dai kumbe ZITTO kaibuka kidedea!
 
Twende nyuma, twende mbele, yaani twende kotekote, kupindisha sheria ya manunuzi kwa maslai ya nchi siyo kitu mbaya. Mbaya ni ile kuzingatia sheria kwa maslai binafsi, wapi yule fisi mtoto zzk?
 
Hivi hakuna mgongano wa maslahi kwa wabunge kuwa wajumbe wa kamati inayochunguza tuhuma dhidi ya wabunge wengine wa bunge hilohilo? Hii kisheria imekaaje? Haki inaweza kutendeka au kuonekana kuwa imetendeka katika mazingira kama hayo?

nimependa comment yako hakika katika katiba mpya hili naomba litizamwe ili kuepusha mgongano wa kimaslahi.
 
Haya magazeti nayo siku hizi hayaaminiki. Yanaandika habari za mtaani. Mfano vyombo vingi vya habari vya Kenya viliweka habari ya balozi wa Tanzania kufukuzwa Malawi

Hata hivyo kusema ukweli nimeanza kumstukia prof Muhongo. Alitoa ahadi ya wiki mbili kufanya mapitio ya mikataba kisha umma ujulishwe. Mwezi unaisha bila bila

Kaaazi kweli kweli!
 
Ndugu zangu niliandika hapa jukwaani jinsi William lukuvi kwa kusaidiana na maswi walitengeneza zile tuhuma ili kuondoa concentration ya nini kijadiliwe kwenye bajeti ya nishati, na walifanikiwa sana, ni kweli kuna wabunge wanafanya biashara na tanesco wapo, taarifa imewataja na Bahati nzuri,wote ni ccm. Kamati haijathibitisha rushwa yeyote na badala yake inayeonekana alikula rushwa ni maswi , kwa nini aliondoka akaenda mlango wa nyuma akaipa zanuni kampuni ya puma kisa Ina bei ndogo bila kuziuliza kampuni zingine ukizingatia kuwa hapo awali puma alibid kwa bei kubwa? Sasa wameumbuka wakiwamo waliotaka kushambulia Akina zitto kisa tu wanasema sheria ifuatwe, nimeongea na j Mushi , nitaiweka hiyo taarifa ya bunge hapa wiki hii.

Acha Kuzunguka Mbuyu wewe!!!! Huyu Dogo Fisadi Tu hata ukeshe kumuombea.
 
babykailama,
Mheshimiwa spika alivunja kamati ya mNishati na madini kwa sababu ya maelezo ya Mh.waziri ambaye yeye ndiye aliwatuhumu wabunge hao kuchukua rushwa. Ilikuwa ni kazi yake kuwa na ushahidi kuonyesha ama kuelekeza Rushwa imetolewa wapi. na ikumbukwe pia hata hapa JF mlikuja mapema sana kabla hata bajeti haijasomwa na kutuambia tusimkubali Mhando.. ushawishi huu ulitokana na nini haswa ikiwa kuna uchunguzi unafanyika.. Kwa nini mlitaka tuwasikilize nyie na kumuunga mkono waziri kabla hata bajeti haijasomwa. Ina maana mlijua najet haitapita na inakutana na watu watakao ipinga sasa kwa nini mssisubiri nasi tuione tuisome na tusikie wanapinga kwa sababu gani maana sisi sote hapa tulikuwa hatujui kilichomo..

Kwa hili nitakuwa upande wa Zitto maana tayari tumesha yaona madudu ya waziri Muhongo na sera zenu za kuuza nchi. Swali dogo sana Zitto aliwauliza, kuna sheria ya kodi ilokweisha pendekezwa na kamati ya Bomani toka mwaka 2008 kwa nini haijatumika?..Na kwa nini wizara haijafuata ushauri ule.

Swala la Tanesco, unaposema waziri amekuta CEO wa Tanesco ana makosa makubwa ya ukiukaji ktk kiuendeshaji na kwa kupitia Bodi yake. Mnamsimamisha wa nini ili kupisha uchunguzi badala ya kumpeleka mbele ya sheria. Sema alikuwa mkisiwa, na hivyo uchunguzi unafanywa ili ku prove kama tuhuma hizo zina ukweli na yeye anahusika..Unapomkamata mwiz unampeleka mbele ya sheria moja kwa moja..
 
Last edited by a moderator:
Hapa nina waiswasi CCM wanakwepa yafuatayo kwa kuliweka sintofahamu hili la Wabunge-WAPIGA dili:
1. Mauaji ya Mwangosi yakitawala Bunge hili la mwezi wa 11 na ripoti zake Serikali itakua uchi zaidi.Hivyo ni vema kuwahamishia Wabunge kwenye hili la Tanesco maana halina madhara kwa watu wa kada ya chini
2.Vurugu za kidini Mbagala na uchomaji makanisa
 
Nonsense, huu ule muendelezo wa hadithi za mbio za kinyonga kujipanga barabarani eti baadaye aitwe mshindi. Hakuna asiyejua kuwa Muhando alikuwa mwizi hakuna asiyejua kuwa akina Kigeugeu Zitto walikuwa wanamtetea huyo mwizi. Mbona hata wabunge wenyewe walikubali kuwa kuna wabunge walikuwa wanatembeza mshiko na wakawa wanashangilia na kusema watajwe hadharani?

Wajaribu kuwasafisha tu lakini walioshika mpini ni wananchi na tunawasubiri majimboni. Huyu Zitto ni mtu mnafiki sana ndiye mpikaji wa michezo yote hii michafu ili Lissu aonekane muongo pia na mjadala uzuke kuwa hata CHADEMA nao ni waongo. Kwa mchezo anaocheza wa kuwa double Agent Zitto anastahili kufungiwa jiwe kubwa shingoni na kushushwa ziwa Tanganyika!

Kama kweli haya ndivyo yatakavyokuwa, mimi ningemshauri Waziri Prof. akatae ushenzi huo tuone watamfanya nini? Rais aliyemteua amtoe tuone maana huwezi kuwa na Waziri anayejitahidi kurekebisha Taasisi na kuleta mabadiliko kwa ajili ya Wananchi halafu tena ninyi mnaanza kumchora na kumfanya kama mtoto eti kamati imemkuta na hatia-ipi??

Ebu waombeni watu wa TV warudie kuwaonyesha mkanda wa siku hiyo muone jinsi kila lilipotamkwa suala la wabunge kuzunguka usiku kucha na hongo wabunge wote walivyokuwa wananyanyuka kwa hisia na kushangilia kuwa watajwe watajwe! Watu wenye heshima na uelewa wao kama wabunge wazushiwe jambo ambalo halipo la kipumbavu na kudhalilishwa wangebehave hivyo?

Sasa sheria na kanuni zifuatwe: Hakuna Mbunge anaye mwajibisha Waziri; wabaki watoe ushauri kwa Serikali, la kama double dealer Zitto halidhiki kama kawaida yake tunamkumbusha achukuwe tena karatasi kama alivyotumwa wakati ule ajipange nje kutishia kumpigia kura isiyo na imani na waziri Mkuu lakini Mtu Msomi na mwadilifu kama Prof. Muhongo wala Maswi wala Naibu Waziri yeyote wa Nishati na madini asiombe msamaha wowote kwa mafisadi!!!
Acha chuki za kichawi.
Kilichotokea, kwa nia mbaya au nzuri sheria imevunjwa
 
Wabuge wa Tanzania ni watu wa ajabu sana!

Iweje kamati ya Bunge ichunguze Wabunge wake?

Kwa nini wabunge wajichunguze wenyewe? Iko wapi misingi ya utawala bora? Kamati hii ina tofauti ipi na ile ya Nchimbi?

Au ya Polisi kuchunguza Polisi wanaotuhumiwa kumpiga Ulimboka?

Hivi ni vituko tu na kufanya watu hawana akili. Hakuna anayeweza kuamini matokeo ya kamati za dizaini hii.

Ni usanii mtupu, kama kawaida yenu, muwalaumu watendaji wakati mapungufu yenu mkiyaficha.

Kupitisha watu wawaite waheshimiwa yalikuwa makosa makubwa mno, matendo yenu hayastahili title hiyo.
 
he! sasa umeshaambiwa chanzo ni gazeti la nipashe, kanunue gazeti au azima then ndo ujue ukweli, sasa kuniita mkuda kwan i miye ndo nilikuwa mwanakamati? tatizo mnataka kuambiwa uongo,sasa ngwilizi kaupata ukweli hamuamini. siku mtakaposikia kuwa magufuli ni mla rushwa namba wani kupitia taasisi za umma kama SUMAJKT, TBA NDO HAMTAAMINI KABISAAAAA

Unavyoandika hapa mkuu inaonekana wazi kabisa wewe ni fisadi au mmoja wa waathirika wa mbano ambao Maswi na Muhongo wameuleta hapo TANESCO. Pole maana biashara yako ya kuiibia nchi imedoda. Lol!
 
Hii ndiyo wizara ya matatizo hata kama utakuwa mr.clean ukikanyaga tu wizara hiyo lazima uchafuke tu penda usipende
 
Its very open kwamba Muhongo na maswi walipindisha utaratibu.. swali ni, Je walipindisha utaratibu kwa manufaa ya Uma au kwa manufaa ya wanyonyaji wachache? kamati ilitakiwa kujibu hili swali na sio kushadadia upindishaji wa utaratibu

I still stand for Muhongo and Maswi japokua sipendi kabisa MaCCM
 
Rushwa huwa haina mazingira rasmi ya kupeana yanayoweza kuthibitika haraka/kirahisi.hawa wabunge kwa kuwa waliomba mlungula kwa mlango wa nyuma wanajiona wajanja kwa kukosekana ushahidi lakini sio wasafi hatta kidogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom