#COVID19 Kamati ya Kuchunguza Covid-19 iwe makini sana na hadidu rejea

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,162
10,890
Kamati iliyoahidiwa na mheshimiwa Rais Samia Suluhu ya kuchunguza corona inabidi iweke hadidu rejea zake kwa umakini bila kupendelea upande wowote.Mambo yafuatayo ni muhimu kuyaweka kwenye utafiti wao.

Jinsi corona inavyoambukiza watu wa rika tofauti na sababu zake?

Je, dawa za kiasili zinasaidia kupunguza ugonjwa huo kwa kiasi gani?

Je, ni kweli chanjo zinazotolewa zinazui corona?

Ni chanjo ipi bora zaidi kutumiwa kati ya zile za Uiengereza, Marekani, China na Urusi.

Na ni yepi madhara ya muda mrefu yatokanayo na chanjo wakati utafiti umefanyika muda mfupi.

Baada ya kujadili vitu hivyo na vyengine vingi watakavyoviingiza hapo ndipo nchi ichukue maamuzi bila kufuata shinikizo la taifa lolote na bila kupuuza baadhi ya misimamo iliyochukuliwa na hayari Rais Magufuli.

Zaidi ya hivyo hapo itakapoonekana kuna umuhimu wa Tanzania kutojitenga kama kisiwa kuhusiana na ugonjwa wa corona basi nchi yetu isikubali kupokea chanjo za bure kupitia Covax. Tanzania inunue chanjo kwa pesa zake kwani sisi si miongoni mwa mataifa masikikini tunaopaswa kupokea chanjo za bure.

Zinunuliwa chanjo chache kabisa na isiwe lazima kuchanja. Anayetaka au atakayehitajika kuchanjwa aruhusiwa kufanya hivyo na wote wengine wasilazimishwe chanjo wala kuvaa barakoa.
 
Ushauri Mzuri, Lakini Hapa Mama amefeli, Walanguzi wataanza kumletea mbinu za Mataifa ya nje na Kumshauri kuhusu chanjo, Akijiloga akakubali tutashuhudia Ufisadi mkubwa sna Katika Historia ya TZ. Hii Corona Imetumika Kama fursa ya Kibiashara Kwa Wanasiasa wengi sana Wa Africa Haswa Kenya (Rejea KEMSA Scandal Juu ya COVID-19). Kwenye Mambo kama Haya ndipo nilipokua nayakubali Maamuzi ya Chuma.
 
Sio kwamba NIMR walikuwa hawafanyi tafiti za Covid-19, ishu ni kwamba haikuwa ikijulikana kama ambavyo mama kaona bora iwe wazi ili walimwengu watusome.

Na pia matokeo ya tafiti zao yawe wazi.
 
Hapa Mama amefeli, Walanguzi wataanza kumletea mbinu za Mataifa ya nje na Kumshauri kuhusu chanjo, Akijiloga akakubali tutashuhudia Ufisadi mkubwa sna Katika Historia ya TZ. Hii Corona Imetumika Kama fursa ya Kibiashara Kwa Wanasiasa wengi sana Wa Africa Haswa Kenya (Rejea KEMSA Scandal Juu ya COVID-19). Kwenye Mambo kama Haya ndipo nilipokua nayakubali Maamuzi ya Chuma.
Si umeona juzi raisi wa Gabon akimdunda kwa makonde waziri wake kuhusiana na pesa za corona.
 
Chanjo zimekuwa zikisikika kuwa Na madhara!

Yatuepuke hayo kwa kweli jamani.
Kabisa bwana!
Iwapo tumepita mawimbi na mawimbi ya maambukizi na bila chanjo.Itakuwa akili gani hiyo kuogopa sasa na kujiingiza kwenye mambo yenye shaka na gharama nyingi.Wao wameshachanja na kila siku habari ni hiyo hiyo maambukizi yemeongezeka maradufu.
 
ANayetaka au asiyetaka kuchanjwa iwe hivyo
Ndio hivyo.Kwani huko tuendako chanjo zitalazimishwa kimataifa.Anayetaka kuchanjwa asafiri sawa lakini hapa kwetu kila mtu na hiyari yake.
 
Ushauri Mzuri, Lakini Hapa Mama amefeli, Walanguzi wataanza kumletea mbinu za Mataifa ya nje na Kumshauri kuhusu chanjo, Akijiloga akakubali tutashuhudia Ufisadi mkubwa sna Katika Historia ya TZ. Hii Corona Imetumika Kama fursa ya Kibiashara Kwa Wanasiasa wengi sana Wa Africa Haswa Kenya (Rejea KEMSA Scandal Juu ya COVID-19). Kwenye Mambo kama Haya ndipo nilipokua nayakubali Maamuzi ya Chuma.
Dah! Kama yule mrembo wa kizungu wa amazingpolly.net yuko sahihi, basi msimamo wa Mama juu ya covid19 uko wazi kabisa. Tujiombee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshaurini Mh SSH Mimi niwemi kwenye hiyo Kamati.Kuna mambo yanahitaji sometimes kuweka makaratasi pembeni na kuiruhusu akili ya asili ifanye kazi.Ndio utauona mchezo wa Corona.
 
Ushauri Mzuri, Lakini Hapa Mama amefeli, Walanguzi wataanza kumletea mbinu za Mataifa ya nje na Kumshauri kuhusu chanjo, Akijiloga akakubali tutashuhudia Ufisadi mkubwa sna Katika Historia ya TZ. Hii Corona Imetumika Kama fursa ya Kibiashara Kwa Wanasiasa wengi sana Wa Africa Haswa Kenya (Rejea KEMSA Scandal Juu ya COVID-19). Kwenye Mambo kama Haya ndipo nilipokua nayakubali Maamuzi ya Chuma.
Hebu nyie Mataga yale mawazo mwitu ya marehemu pombe bakini nayo wenyewe na familia zenu.

Wataalam wakija na maoni ya kisayansi lazima tuyafate ila kama wewe unataka kuishi kienyeji kama Musukuma nenda ukajifungie kwenye lile tanuru lake ujifuze na kutembea kifua mberee kama marehemu pombe.
 
Hapa walete tu iyo chanjo ila mtu awe huru kuamua km anataka kuchanjwa au la. tusilazimishane.
 
Hebu nyie Mataga yale mawazo mwitu ya marehemu pombe bakini nayo wenyewe na familia zenu.

Wataalam wakija na maoni ya kisayansi lazima tuyafate ila kama wewe unataka kuishi kienyeji kama Musukuma nenda ukajifungie kwenye lile tanuru lake ujifuze na kutembea kifua mberee kama marehemu pombe.

Endeleeni kumshukuru Mungu na kina JPM. Tangu mwaka Jana mwezi March. Kumekuwa na Lockdowns mbali mbali. Na Sasa Pia. Lakini wazungu wamechoka na hawafuati masharti. Mzungu anaambiwa unavaa Mara moja. Then kama haijalowa unairudia baada ya siku 6. Lakini huku mtaani unaona kabisa wanavaa chafu na za muda mrefu. Ili wasilipishwe tu Faini. Results Ni kwamba corona badala ya kupungua ndo inazdi. Watu wamechoka na ndoa zinavunjika. Depressions. Ajira nk.

Leo mama akiambiwa na wataalamu kuwa muwe na lockdown. Mtarudi hapa kutukana na kuomba JPM afufuke. Jilinde uwezavyo. Lakini kwa aina ya maisha yenu. Nyumba za kupanga. Familia nne nk nyumba moja na vyoo 2 . Kwenu lockdown haina mana. Masks Ni hizi za kununua. Hata wazungu wanashindwa. Je wewe mtz. Mavitambaa haya huku ulaya hawaruhusu tena. Corona Ni Hatari kwa uchumi wako kuliko afya.
 
Back
Top Bottom