Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 40,000
Nimeeleza kwenye ile mada nyingine kuwa haya yote ni mazingaombwe. Bado naamini hivyo. Ninaamini mazingaombwe haya ni kamili (complete illusion) kwa sababu kamati teule iliyoundwa na Spika Makinda kuchunguza tuhuma hii kimsingi imepewa jukumu lisilowezekana. Kamati hii inaongozwa na Hassan Ngwilizi (CCM) na wajumbe wake wengine wakiwa ni: John Chiligati (CCM), Said Arfi (CHADEMA), Riziki Omar Juma (CUF), na Gosbert Blandes (CCM).
Nani aliomba rushwa na aliombaje?
Kazi kubwa ya kuweza kuthibitisha hili inaanzia hapa. KT inapaswa kupata ushahidi usiokinzana wa kuonesha nani aliomba rushwa TANESCO na aliomba rushwa hiyo vipi. Ni rahisi - kwa kiasi - kuweza kutaja majina ya walioomba rushwa lakini kuweza kuonesha waliomba "vipi" rushwa hiyo ikawa ni kazi. Kama mbunge aliomba rushwa kwa mtendaji wa TANESCO na wakati anafanya hivyo walikuwa wawili tu ni kwa kiasi gani maneno ya mtendaji wa TANESCO yataweza kuaminika bila ya ushahidi mwingine wowote wa nje (mawasiliaoni ya simu, email, video au vimemo)?
Kumbe haitoshi kusema tu "fulani aliomba rushwa" kwani hilo peke yake bila ushahidi wa nje wa uombaji huo ni maneno dhidi ya maneno.
Nani alipokea rushwa?
Sasa inawezekana kuwa ni vigumu kuonesha ni vipi rushwa iliombwa; lakini ni rahisi kwa kiasi chake kuonesha kama rushwa ilipokelewa. Kama rushwa haikutolewa na hakuna ushahidi wa kuonesha kuwa rushwa imepokelewa madai kuwa kuna mtu aliomba rushwa yanaweza kuonekana ni masimulizi tu. Kama rushwa ilipokelewa ni wazi basi kuna mtu aliitoa. Huyu aliyetoa ni nani? na kama alitoa ni kwanini alitoa bila kujaribu kuwasiliana na TAKUKURU kuwanasisha wataka rushwa hawa?
Hili linatudokeza lile la kwangu la "mazingaombwe". Kama mtu alitoa rushwa bila kushirikisha vyombo vya usalama ili kumnasa mtoa rushwa mtu huyo naye anashtakika kwa mashtaka ya kutoa rushwa! Ikumbukwe katika sheria yetu mtoa rushwa na mpokea rushwa wote wanashtakika! Ushahidi wa kuwa mtu kapokea rushwa ni pamoja na kukutwa na rushwa. Ina maana akaunti za wabunge WOTE wanaotuhumiwa kupokea rushwa (siyo kuomba tu) ni LAZIMA zipitiwe na kamati teule na pamoja na akaunti hizo ni zile za JAMAA NA NDUGU WA KARIBU na kulinganisha mtiririko (flow) ya fedha katika siku ambazo viongozi wanadaiwa kuomba rushwa.
Uchunguzi huu hauwezi kukamilika bila kueleza wazi kuwa akaunti za wabunge watuhumiwa na jamaa zao wa karibu zilikuwa au hazikukutwa na kiasi cha fedha kinachodaiwa kutolewa. Naamini wataangalia pia 'movement' ya fedha kutoka akaunti hizo baada ya tarehe ya sakata kulipuka bungeni.
Itakuwaje kama hakuna ushahidi wa kiforensiki wa rushwa?
Sasa, swali hili liko katika kiini cha nani anasema kweli. Kama hakuna ushahidi wa rushwa kutolewa au kupokelewa na wala hakuna ushahidi wa rushwa kuombwa ni kwa vipi watu waliweza kusimama BUNGENI na kudai kuwa kulikuwa na rushwa? Je tunakumbuka (au tumesahau) jinsi sakata la Jairo lilivyodai kuwa kuna "rushwa" ilitolewa kwa wabunge na wengine tulipinga vile vile kwani hakukuwa na ushahidi? Na ni kweli walipochunguza "hawakukuta" rushwa hiyo? Sasa kama hakuna ushahidi wowote kuonesha kama rushwa iliombwa, ilitolewa au ilipokelewa hawa wabunge wanaosimama kudai kuna rushwa wanapata wapi taarifa hizo?
Lakini kama wapo wabunge wanaopokea rushwa (wakiomba au wasipoomba) na wanaweza kuficha rushwa hiyo kiasi kwamba haiwezi kuonekana kwa vyombo vya usalama je hii ina maana gani? Je tuna uhakika gani kuwa kila wanapoulizwa "wale wanaokubali waseme ndiyo" wanasema ndiyo na "wale wanaokataa waseme hapana" halafu "waliosema ndio wameshinda" wanafanya hivyo wakiwa na mulungula mfukoni au kwenye vyungu vyao? Lakini, kama ni kweli wabunge wanaweza kuhongwa kwa ajili ya kufanya mambo fulani Bungeni na hakuna mtu ambaye ameweza kuwanasa ina maana kuwa tuna mfumo mbovu kabisa wa kupigana na rushwa? siyo?
Kwamba wabunge wenyewe wanajuana nani mpokea rushwa na nani anapenda kuomba omba rushwa lakini wabunge hawa walioapa kuilinda, kuitetea na kuihifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hakuna hata mmoja wao ambaye ameweza kusaidia vyombo vya dala kuwanasa wenzie wala rushwa?
Lakini swali la ugomvi ni kuwa: KAMA kweli Bungeni wala rushwa wapo, wanajuana na kulindana na wakikasirikiana wanatajana ni kwa kiasi gani tunaweza kuamini wanavyozungumza kwa jazba, kumwaga data na hata kuonekana ni wazalendo? Na kama wabunge wala rushwa hawawezi kupatikana tunaweza vipi kuliamini Bunge hili lote?
Swali zaidi ambalo sitaki kufikiria maana yake ni kuwa ITAKUWAJE KAMA KAMATI TEULE ITAKUTA KUWA NI KWELI WAPO WABUNGE WAMEKULA RUSHWA? Ikumbukwe agizo la Spika Makinda ni kuwa wakimaliza kina Ngwilizi wamshauri nini cha kufanya! Hakuwapa agizo la kusoma ripoti yao BUNGENI. Kwanini wabunge wasimtake Spika kutaka Kamati Teule isome ripoti yake Bungeni moja kwa moja ILI BUNGE LIAMUE NINI CHA KUFANYA BADALA YA YEYE MTU MMOJA?
Nani aliomba rushwa na aliombaje?
Kazi kubwa ya kuweza kuthibitisha hili inaanzia hapa. KT inapaswa kupata ushahidi usiokinzana wa kuonesha nani aliomba rushwa TANESCO na aliomba rushwa hiyo vipi. Ni rahisi - kwa kiasi - kuweza kutaja majina ya walioomba rushwa lakini kuweza kuonesha waliomba "vipi" rushwa hiyo ikawa ni kazi. Kama mbunge aliomba rushwa kwa mtendaji wa TANESCO na wakati anafanya hivyo walikuwa wawili tu ni kwa kiasi gani maneno ya mtendaji wa TANESCO yataweza kuaminika bila ya ushahidi mwingine wowote wa nje (mawasiliaoni ya simu, email, video au vimemo)?
Kumbe haitoshi kusema tu "fulani aliomba rushwa" kwani hilo peke yake bila ushahidi wa nje wa uombaji huo ni maneno dhidi ya maneno.
Nani alipokea rushwa?
Sasa inawezekana kuwa ni vigumu kuonesha ni vipi rushwa iliombwa; lakini ni rahisi kwa kiasi chake kuonesha kama rushwa ilipokelewa. Kama rushwa haikutolewa na hakuna ushahidi wa kuonesha kuwa rushwa imepokelewa madai kuwa kuna mtu aliomba rushwa yanaweza kuonekana ni masimulizi tu. Kama rushwa ilipokelewa ni wazi basi kuna mtu aliitoa. Huyu aliyetoa ni nani? na kama alitoa ni kwanini alitoa bila kujaribu kuwasiliana na TAKUKURU kuwanasisha wataka rushwa hawa?
Hili linatudokeza lile la kwangu la "mazingaombwe". Kama mtu alitoa rushwa bila kushirikisha vyombo vya usalama ili kumnasa mtoa rushwa mtu huyo naye anashtakika kwa mashtaka ya kutoa rushwa! Ikumbukwe katika sheria yetu mtoa rushwa na mpokea rushwa wote wanashtakika! Ushahidi wa kuwa mtu kapokea rushwa ni pamoja na kukutwa na rushwa. Ina maana akaunti za wabunge WOTE wanaotuhumiwa kupokea rushwa (siyo kuomba tu) ni LAZIMA zipitiwe na kamati teule na pamoja na akaunti hizo ni zile za JAMAA NA NDUGU WA KARIBU na kulinganisha mtiririko (flow) ya fedha katika siku ambazo viongozi wanadaiwa kuomba rushwa.
Uchunguzi huu hauwezi kukamilika bila kueleza wazi kuwa akaunti za wabunge watuhumiwa na jamaa zao wa karibu zilikuwa au hazikukutwa na kiasi cha fedha kinachodaiwa kutolewa. Naamini wataangalia pia 'movement' ya fedha kutoka akaunti hizo baada ya tarehe ya sakata kulipuka bungeni.
Itakuwaje kama hakuna ushahidi wa kiforensiki wa rushwa?
Sasa, swali hili liko katika kiini cha nani anasema kweli. Kama hakuna ushahidi wa rushwa kutolewa au kupokelewa na wala hakuna ushahidi wa rushwa kuombwa ni kwa vipi watu waliweza kusimama BUNGENI na kudai kuwa kulikuwa na rushwa? Je tunakumbuka (au tumesahau) jinsi sakata la Jairo lilivyodai kuwa kuna "rushwa" ilitolewa kwa wabunge na wengine tulipinga vile vile kwani hakukuwa na ushahidi? Na ni kweli walipochunguza "hawakukuta" rushwa hiyo? Sasa kama hakuna ushahidi wowote kuonesha kama rushwa iliombwa, ilitolewa au ilipokelewa hawa wabunge wanaosimama kudai kuna rushwa wanapata wapi taarifa hizo?
Lakini kama wapo wabunge wanaopokea rushwa (wakiomba au wasipoomba) na wanaweza kuficha rushwa hiyo kiasi kwamba haiwezi kuonekana kwa vyombo vya usalama je hii ina maana gani? Je tuna uhakika gani kuwa kila wanapoulizwa "wale wanaokubali waseme ndiyo" wanasema ndiyo na "wale wanaokataa waseme hapana" halafu "waliosema ndio wameshinda" wanafanya hivyo wakiwa na mulungula mfukoni au kwenye vyungu vyao? Lakini, kama ni kweli wabunge wanaweza kuhongwa kwa ajili ya kufanya mambo fulani Bungeni na hakuna mtu ambaye ameweza kuwanasa ina maana kuwa tuna mfumo mbovu kabisa wa kupigana na rushwa? siyo?
Kwamba wabunge wenyewe wanajuana nani mpokea rushwa na nani anapenda kuomba omba rushwa lakini wabunge hawa walioapa kuilinda, kuitetea na kuihifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hakuna hata mmoja wao ambaye ameweza kusaidia vyombo vya dala kuwanasa wenzie wala rushwa?
Lakini swali la ugomvi ni kuwa: KAMA kweli Bungeni wala rushwa wapo, wanajuana na kulindana na wakikasirikiana wanatajana ni kwa kiasi gani tunaweza kuamini wanavyozungumza kwa jazba, kumwaga data na hata kuonekana ni wazalendo? Na kama wabunge wala rushwa hawawezi kupatikana tunaweza vipi kuliamini Bunge hili lote?
Swali zaidi ambalo sitaki kufikiria maana yake ni kuwa ITAKUWAJE KAMA KAMATI TEULE ITAKUTA KUWA NI KWELI WAPO WABUNGE WAMEKULA RUSHWA? Ikumbukwe agizo la Spika Makinda ni kuwa wakimaliza kina Ngwilizi wamshauri nini cha kufanya! Hakuwapa agizo la kusoma ripoti yao BUNGENI. Kwanini wabunge wasimtake Spika kutaka Kamati Teule isome ripoti yake Bungeni moja kwa moja ILI BUNGE LIAMUE NINI CHA KUFANYA BADALA YA YEYE MTU MMOJA?