Hili ni tatizo linalomea matawi, na linatapakaa kila kona ya nchi. Janga la Kamari (Betting). Kila kona ya jiji la Dar-es-Salaam, Mwanza na Arusha, Mashine za kamari zimewekwa.
Majuzi kati nilikuwa Shinyanga vijijini, watoto waodogo umri wa shule wamejazana ndani ya kachumba kadogo wanacheza kamari badala ya kwenda shule.
Wawekezaji wa Kichina kabla ya saa sita mchana wanafika na kufungua mashine na kujibebea kitita cha fedha bila kujali ni fedha zilizotokana na nini. Hawa Wachina wapataje vibali kuweka hizi mashine za Kamari?
Haya madude yamesambazwa nchi ázima. Vijana wanaangamia kwani wanashinda siku zima wanacheza kamari.
Hebu tujadili hili suala kama taifa!
Majuzi kati nilikuwa Shinyanga vijijini, watoto waodogo umri wa shule wamejazana ndani ya kachumba kadogo wanacheza kamari badala ya kwenda shule.
Wawekezaji wa Kichina kabla ya saa sita mchana wanafika na kufungua mashine na kujibebea kitita cha fedha bila kujali ni fedha zilizotokana na nini. Hawa Wachina wapataje vibali kuweka hizi mashine za Kamari?
Haya madude yamesambazwa nchi ázima. Vijana wanaangamia kwani wanashinda siku zima wanacheza kamari.
Hebu tujadili hili suala kama taifa!