Nimekuwa nikimsikiliza huyu jamaa, akiwa anafanya mahojiano mbalimbali. Iwe na BBC, DW, na pia vyombo vya habari vya hapa nyumbani. Uongeaji wake huwa wanikosha sana.
Jamaa ametulia, anaongea 'point' tu, kila mtu hutamani kumsikiliza. Ninaamini haya matukio ya ujambazi Dar es Salaam yataisha kabla hakujacha.
Watu kama hawa tukiwa CCP walikuwa wana pass out angalau na kirungu kimoja, hususani cha ukakamavu.
Ukiwaacha Thobias Andengenye na Diwani Athumani, Sirro atakuwa Bonge la IGP.
Aliwahi sifiwa hadi na Gazeti la Mwanahalisi, kwa kuzima mapigano ya wakulima na wafugaji huko Ikwiriri.