BONGOLALA
JF-Expert Member
- Sep 14, 2009
- 16,511
- 11,913
Pamoja na kwamba nimesikitishwa na kifo cha kikatili cha ndugu Mawazo lakini sikubaliani na hii tabia ya kupeana tuhuma. Wananchi wengi tunahisi huenda kifo cha mawazo kimesababishwa na mgogoro wa dhulma humo humo ndani ya CHADEMA; Wengine wanasema huenda ni migogoro binafsi kati yake na jamaa zake. CHADEMA mnasema kifo chake kimepelekewa na green guard kumvamia marehemu na wengine mnasema polisi ndio wamemuua. Sasa tushike lipi!?
Aidha, mbona kifo cha Chacha Wangwe hatukuona watu kuguswa hivi!? Wakati kilijaa giza zito na hadi leo haieleweki nini kimemuua Chacha Wangwe. Ndugu Lema kama unajua kuhusu Wangwe tugusie kidogo. Huenda ikatoa mwanga wa kujua kuhusu kifo cha Mawazo. Natazama kwa jicho la tatu tu.
RIP Mawazo
Kazi ya polisi ni nini?