Kamanda Mawazo ameuawa na Mfumo wa Jeshi la Polisi - Lema

Kamanda Mawazo ameuawa na Mfumo wa Jeshi la Polisi - Lema

mkuu Lema, kwanza pole sana kwa msiba huu mzito.

but nataka kufanya rejea kidogo...hivi yale mauaji ya Soweto Arusha, mhabarishaji Mwangosi, nk, nk... yameishia wapi?

maana kama hakuna kilichofanyika kwa hayo ya nyuma, ni kipi kipya tukitegemee kwa hili la kamanda Mawazo?

nawaza kwa sauti tu...
 
Apumzike kwa amani. . . Pole sana kaka mkubwa godless J Lema

Ni wakati muafaka wa kutafakari vitendo vya aina hii. . . . .
Ni wakati wa wananchi kuangalia kitu hiki kwa jicho la tatu. . . .
 
Last edited by a moderator:
Jamani Mbona hakuna anayeeleza kisa cha yeye kuvamiwa? Yeye kama mwananchi anaweza tenda kosa kwahiyo msikimbilie kwenye nafasi yake bila kueleza mkasa mzima.

Kwan mwananchi akitenda kosa anatakiwa auwawe ??? Kwel tunasafar ndefu ya kuelimisha watu huyu bwana alikuwa ametoka kwenye mkutano wa kampeni kumnadi mgombea udiwani.......ametenda kosa lip asifikishwe mahakaman ameuawa.....
 
Pamoja na kwamba nimesikitishwa na kifo cha kikatili cha ndugu Mawazo lakini sikubaliani na hii tabia ya kupeana tuhuma. Wananchi wengi tunahisi huenda kifo cha mawazo kimesababishwa na mgogoro wa dhulma humo humo ndani ya CHADEMA; Wengine wanasema huenda ni migogoro binafsi kati yake na jamaa zake. CHADEMA mnasema kifo chake kimepelekewa na green guard kumvamia marehemu na wengine mnasema polisi ndio wamemuua. Sasa tushike lipi!?

Aidha, mbona kifo cha Chacha Wangwe hatukuona watu kuguswa hivi!? Wakati kilijaa giza zito na hadi leo haieleweki nini kimemuua Chacha Wangwe. Ndugu Lema kama unajua kuhusu Wangwe tugusie kidogo. Huenda ikatoa mwanga wa kujua kuhusu kifo cha Mawazo. Natazama kwa jicho la tatu tu.

RIP Mawazo
 
Ushahidi wa uongo sio mzur,uko dar huko umejifichavnyuma ya keybord unajiandikia tu unachohisi then anatoa ushuhuda,acheni siasa huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine

Uhalifu uliofanywa na .....geenguard
 
Maneno haya hameniumiza sana kwa kweli, nenda kamanda Mawazo Nenda.

Acha porojo zenu , achana na siasa za upuuzi , hapa Nazi tu hakuna mwenye shida na magwanda yenu
 
Hii haikubaliki ....hii lazima ifike mwisho ....
 
Kuna mijitu humu ilichekelea sana mwenyekiti wa ccm mkoa wa mwanza alivyouliwa kule kisesa, sasa hayohayo eti yanalaani,

nilidhani mtampongeza kuwa kafa kishujaa, munafuga ugonjwa wenyewe sasa munaota matende, tulishasema hii biashara sijui kulinda kura sijui green guard iko siku itawatokea puani.

Leo lema kamwona mawazo hao wengine hajawaona? Au kwa kuwa hajawapa magwanda?
 
maneno ya kichochezi kama haya ktk uzi huu yapingwe. Kuanzia ya Lema na wachangiaji wengine, kila aandikaye "anadhani" waliotenda hivyo ni akina fulani pasipo chembe ya uhakika...... MTACHIMBA SHIMO NA MTATUMBUKIA WENYEWE
 
Na nyie viongozi wa ukawa mmekaa kimya sana , toeni tamko kieleweke sio kulia lia kwenye social media,

Wanaboa sana brother wangu chama utafikiri hakuna wanaume!! Kuheshimiana hapa ni t for tat.
 
Tunahitaji viongozi wa kisiasa wenye uwezo wa kujenga hoja na sio wenye kuijaza chuki jamii...!

Wako baadhi ya wenye dhamana ya ulinzi wa jamii wakishirikiana na wanasiasa au wafanyabiashara wa madini wanaendesha mauaji ya kikatili dhidi ya jamii mfano albino.

Hili ni tatizo msingi linalotakiwa kushughulikiwa.Nilidhani Lema unaliongelea hili.

Maoni yangu ni kuwa na utulivu na uvumilivu wa hali ya juu kama kiongozi kwani ubaya hulipwa kwa wema zaidi...!!!
 
Kamanda Mawazo kauawa na Polisi na inajulikana,najiuliza hivi hawa Polisi wetu ni Watanzania?na kama ni Watanzania wanapigania nini?nasema wazi watatumaliza wote ili wabaki wenyewe,lakini kabla hawajatumaliza haki itachukua mkondo wake na ndipo Taifa langu Tanzania litainuka kutoka kwenye mavumbi,Mungu M;laze pema Kaka yangu Kamanda Mawazo!

Una ushahidi juu ya ushiriki wa Polisi? ...kama hauna ushahidi ni bora ukae kimya maana ujumbewako unaweza kuchochea uhasama..
 
Pamoja na kwamba nimesikitishwa na kifo cha kikatili cha ndugu Mawazo lakini sikubaliani na hii tabia ya kupeana tuhuma. Wananchi wengi tunahisi huenda kifo cha mawazo kimesababishwa na mgogoro wa dhulma humo humo ndani ya CHADEMA; Wengine wanasema huenda ni migogoro binafsi kati yake na jamaa zake. CHADEMA mnasema kifo chake kimepelekewa na green guard kumvamia marehemu na wengine mnasema polisi ndio wamemuua. Sasa tushike lipi!?

Aidha, mbona kifo cha Chacha Wangwe hatukuona watu kuguswa hivi!? Wakati kilijaa giza zito na hadi leo haieleweki nini kimemuua Chacha Wangwe. Ndugu Lema kama unajua kuhusu Wangwe tugusie kidogo. Huenda ikatoa mwanga wa kujua kuhusu kifo cha Mawazo. Natazama kwa jicho la tatu tu.

RIP Mawazo

We mjinga kweli wewe, unapinga kutuhumu halafu mwenyewe unatuhumu, Lofa sana wewe
 
Taarifa ya polis I unaiamini sana?? utasikia amepigwa na kitu kizito! aliyemteka Ulimboka ni mkenya, hakuna cha kusubiri taarifa ya polisi ,

Pamoja na mapungufu hayo unayoyasema, hii taarifa pia haitolewi kwa ukamilifu
1. Alikuwa anatoka wapi na saa ngapi?!
2. Alikuwa na nani??!!
3. Alitekwa au alishambuliwa hapo alipokuwepo??!!!
4. Huwa anatembea mwenyewe??!! Hata kipindi hiki??!!
5. Marafiki na watu wa chama mkoa/wilaya walikuwa wapi siku hiyo ya kampeni (alikuwa anatoka kwenye kampeni)??!!!!
6. Chaguzi nyingi zimeisha, chama kina magari yalikuwa yanafanya kazi gani mpaka kiongozi anatekwa akitokea kwenye kampeni(???!!!) au kwenye shughuli za chama??! Au alifikishwa nymbani akatoka mwenyewe??!!!

Taarifa bado haijajaa kiasi cha kutosha

Inabaki kuwa kafanyiwa kitendo kisicho cha kibinaadamu na ni changamoto kwa serikali mpya na Rais mpya
 
Lema, i think kwa hili umewahi sana kutoa tamko.... Bado hujawa mbunge and anything can be done to stop you contesting

jaribu kubana pumzi kidogo tu ili upate nguvu zaidi ya kusukuma gurudumu
 
Siku hizi neno "amani" sitaki hata kulisikia maana linatumika kinafiki sana kupumbaza watu.
 
Ni masikitiko sana kupoteza binadamu ambaye nchi bado inahitaji mchango wake.

Mungu akuweke pema peponi Kamanda Mawazo.

Nashangaa umeanza kutoa tuhuma mapema kabla hata ya uchunguzi haujafanyika. Nadhani Mtu ambaye aliwahi kuwa Mbunge atakuwa anafahamu maana ya sheria.


Na wewe Lema ni kati ya wanasiasa wanaosaidia wauwaji wasifahamike na waendelee kuwepo mitaani!

Kama mmoja wa viongozi wa CHADEMA walivyoueleza ulimwengu, kwa sasa una mkanda ambao unaonyesha watu waliofanya mauwaji katika mkutano Arusha kwenye viwanja vya Soweto! Kinachoshangaza na kusikitisha ni kuendelea kukaa na mkanda wa video badala ya kuvipa vyombo vya habari ili vihabarishe dunia kuhusu wauwaji hao kwa sababu kuna uwezekano wanaendelea kufanya maovu wakati una mkanda unaonyesha sura zao.

Inaeleweka Vyombo vya habari ni muhimili mwingine wa nchi na taasisi zake zinafanya kazi kubwa ya kuelimisha na kupasha habari. Nchi kama Uingereza wananchi wanatumia vyombo vya habari kama BBC kuhabarisha jamii kuhusu watenda maovu walionaswa kwenye video (Crimewatch).

Kama hamuwezi kuwapa polisi/serikali huo mkanda, vipeni vyombo vya habari ili viwafichue watenda maovu.

Kuna familia mpaka sasa hazifahamu kilichotokea mpaka kupotelewa na ndugu, jamaa na marafiki. Kwa familia hizi kufahamu nani aliyetenda maovu ni njia ya kuponya makovu ya masikitiko.

Maisha ya binadamu ni zaidi ya siasa. Hata kuwafahamu kwa sura wauwaji ni moja ya justice kwa familia. Wapeni haki ndugu, jamaa na marafiki.
 
Wanaboa sana brother wangu chama utafikiri hakuna wanaume!! Kuheshimiana hapa ni t for tat.

Mku inauma sana watoe tamko juu ya uchaguzi uliopita ,watoe tamko juu ya haya mambo ya kishenzi yanayoendelea ,watoe tamko kwanini HRLC ilivamiwa na polisi, siku chache mbele Helen K Bisimba akapata ajali ,huu ukimya wao hata kama unajenga ifike sehemu watoe maamuzi
Watoe tamko juu ya yanayo endelea ZANZIBAR
 
Back
Top Bottom