Kamanda John Mhozya tumaini jipya Kibaha

Kamanda John Mhozya tumaini jipya Kibaha

dedam

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
845
Reaction score
166
Kwa muda mrefu sasa tangu uchaguzi wa vyama vyingi uanze mwaka 1995 wana jimbo la Kibaha Vijijini hawajapata kamanda makini wa kuweza kuwakilisha maoni yao, mawazo yao, matatizo yao,bungeni lakini sasa Wanakibaha wanatajiwa kumpata kijana machachari, msomi, mwenye uwezo wa kujenga hoja,mzawa wa Kibaha Vijijini si mwingine bali ni kamanda mwanasheria JOHN MHOZYA.

Njoo tarehe 19.1.2013 siku ya Jumamosi viwanja vya stendi ya Mzenga Mlandizi umuone kijana huyu akiunguruma kwa mara ya kwanza viwanja vya nyumbani akiwa na makamanda wengine wa CHADEMA.

KARIBUNI SANA MAKAMANDA MLANDIZI
 
Pamoja sana wakuu, yule HABIBI wa masalia ndo mnazidi kumuongezea kina cha kaburi lake la kisiasa
 
Pamoja sana wakuu, yule HABIBI wa masalia ndo mnazidi kumuongezea kina cha kaburi lake la kisiasa

HABIB(masalia) yupo kibaha mjini kwa koka.kamanda wetu atakuwa kibaha vijijini kwa mbunge dhaifu HAMUD JUMAA.ni m4c mpaka kieleweke wana kibaha vijijini
 
HABIB(masalia) yupo kibaha mjini kwa koka.kamanda wetu atakuwa kibaha vijijini kwa mbunge dhaifu HAMUD JUMAA.ni m4c mpaka kieleweke wana kibaha vijijini

Ahsante kwa Ilmu mkuu
 
kwa muda mrefu sasa tangu uchaguzi wa vyama vyingi uanze mwaka 1995 wana jimbo la kibaha vijijini hawajapata kamanda makini wa kuweza kuwakilisha maoni yao, mawazo yao, matatizo yao,bungeni lakin sasa wanakibaha wanatajiwa kumpata kijana machachari, msomi, mwenye uwezo wa kujenga hoja,mzawa wa kibaha vijijini si mwingine bal ni kamanda mwanasheria JOHN MHOZYA. Njoo tarehe 19.1.2013 siku ya jumamosi viwanja vya stendi ya mzenga mlandizi umuone kijana huyu akiunguruma kwa mara ya kwanza viwanja vya nyumbani akiwa na makamanda wengine wa chadema. KARIBUNI SANA MAKAMANDA MLANDIZI

makamanda bila depo!!!!
 
kila la kheri kamanda na 2na amini 2nazalisha lissu mwingne,mwanzo mzuri na kaza buti kz ni nzito.
 
Kwa muda mrefu sasa tangu uchaguzi wa vyama vyingi uanze mwaka 1995 wana jimbo la Kibaha Vijijini hawajapata kamanda makini wa kuweza kuwakilisha maoni yao, mawazo yao, matatizo yao,bungeni lakini sasa Wanakibaha wanatajiwa kumpata kijana machachari, msomi, mwenye uwezo wa kujenga hoja,mzawa wa Kibaha Vijijini si mwingine bali ni kamanda mwanasheria JOHN MHOZYA.

Njoo tarehe 19.1.2013 siku ya Jumamosi viwanja vya stendi ya Mzenga Mlandizi umuone kijana huyu akiunguruma kwa mara ya kwanza viwanja vya nyumbani akiwa na makamanda wengine wa CHADEMA.

KARIBUNI SANA MAKAMANDA MLANDIZI

unanikumbusha RUVU SEC SCHOOL 2000, Mkuu nami nakuja kwa UDIWANI kata ya RUVU STATION nakuahidi ushirikiano lkn tatizo la wazaramo kule ni njaa na fikra MGANDO. Mtafute na Mselewa kwa kata ya VISIGA.
 
John Mnaku Mhozya ni classmate wangu,ni kijana mzuri na mweledi,kila la kheri kamanda!
 
kule KUBENEA huku MHOZYA we acha tu
 
Hee, Mhozya umeamua kuingia katika Mchezo huu? Poa Kijana,mdomo unauweza. Nakukumbuka pale Tabora school,nilikuwa kiongozi wako. Safi sana.
 
Wakili Msomi John Mnaku Bonaventure Mhozya ni mtu makini.Yeye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Shule Kuu ya Sheria(zamani Kitivo cha Sheria). Namfahamu Kamanda John M.B.Mhozya tangu mwaka 1998 nilipojiunga Kidato cha Kwanza Shule ya Sekondari ya Ruvu,yeye akiwa kidato cha tatu.

Kamanda Mhozya,ni mjenzi wa hoja.Yeye aweza kuzungumzia umaskini na kueleweka kwakuwa naye ameuishi na kupambana nao hadi sasa anakaribia kuutokomeza.

Kamanda Mhozya hatetereki katika maamuzi yake.Ni mwanachama hai wa CHADEMA anayejipambanua kimatendo hasa kushiriki katika kesi zinazowakabili viongozi na makada wa CHADEMA.

Kamanda Mhozya unahitajika Kibaha Vijijini. Ulikuwa wapi muda wote huo? Ukawatumikie waliokukuza,ukiwaonesha elimu,ujuzi,uzoefu na weledi wako wa uchambuzi wa mambo kwa maendeleo yao.

Kila la kheri Msomi mwenzangu na kaka yangu,Kamanda John M.B.Mhozya(LL.B.,LLM.(Dar))

cc UJANJAUJANJA Edmund
 
Last edited by a moderator:
Namkubali kijana. Si mtu wa kuyumbishwa yumbishwa. Ni mjenzi mzuri wa hoja.
Niliwahi kufanya naye kazi kama viongozi wakati bado tunatoa umande, najua hatowaangusha.
Labda kama amebadilika maana miaka imepita na ufisadi umeibuka pia ukiwemo wa kukalishwa kimya na kupisha wenye hela kufanya wanayoyataka. Anyway tutampima kwa utendaji wake.
 
Tuko pamoja wana Kibaha, lisongesheni mpaka kieleweke.
 
Namtakia kila la kheri Kamanda Mhozya, imekuwa jambo la busara sana amejitokeza mapema ili wapiga kura waanze kumtathmini kabla ya kumpigia kura 2015.
Na huu ni wito kwa makamanda wengine wenye nia ya kuingia kilingeni mwaka 2015 kuhakikisha wameanza "field service" angalau kuanzia sasa.
 
Back
Top Bottom