Kama Wananchi Hawajui Katiba, Basi Serikali na Rais ni Batili

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,077
Kama Watanzania hawaijui katiba, basi hakuna haja ya kuwa na Serikali, hakuna haja ya kuwa na Bunge wala hakuna haja ya kuwa na Mahakama. Turudi kwenye utawala wa jadi ambao haukuwa na katiba.

Kama wananchi hawajui katiba, Serikali, Bunge na mahakama vinapatikana kwa njia gani? Au ndiyo maana wanajipa Urais, wanajipa ubunge na udiwani bila ya kuchaguliwa na wananchi?

Serikali na Rais, Bunge na wabunge, mahakama na majaji, wote upatikanaji wake umeelekezwa na katiba. Kama wananchi hawajui katiba, hakuna haja ya kuwa na uchaguzi, wala hakuna haja kuwa na Rais, Serikali, Bunge, Mahakama, Polisi wala wala mahakama. Wale machifu wa kale, warudishwe kuongoza makabila yao. Wazee wenye hekima, warudishwe kuwahukumu wanaokosea.

Haiwezekani useme wananchi hawaielewi katiba, halafu wewe Urais wako uwe halali. Kama wananchi hawaelewi katiba, na wewe uliyetakiwa kupatikana kwa maelekezo ya katiba, huwi halali, unatakiwa kuondoka au kuondolewa. Ina maana umetumia ujinga wa wasioelewa katiba, kujipa madaraka na mamlaka.
 
Kasahau Yale ya kwenye kiofisi kichafu na meza chakavu na mic moja sijui ilitoka media gani kule Tanga! Kasahau usaidizi wa Mabeyo kwamba alirisk maisha yake kuhakikisha anayazima Yale mapinduzi haramu ya ccm wenzake!
Ama kweli binadamu sisi wasahaulifu mno!
 
Kama Watanzania hawaijui katiba, basi hakuna haja ya kuwa na Serikali, hakuna haja ya kuwa na Bunge wala hakuna haja ya kuwa na Mahakama. Turudi kwenye utawala wa jadi ambao haukuwa na katiba...
Si lazima kila mwananchi aijue katiba na haitawezekana.kwani katiba iliyopo watanzania wangapi wanaijua?

Kwanza wengine hawana hata muda wa kuijua hiyo katiba kwani haiwasaidii.wao wanachokijua ni wale na washibe hayo mengine hayawahusu.

Kwani hivi iliyopo mtanzania gani alihusishwa au alijitolea maoni? Nimemshangaa sana mkuu wa nchi anapoongea vitu vya kufikirika tena nimepatwa na hofu na uwezo wake.
 
Yaani kwakweli hii ni kali ya mwaka kwamba wananchi hawaijui katiba??! Kwa mantiki hiyo hata Uraisi wake wananchi hawatambui dah kweli leo wame muingiza chaka😂😂😂😂
 
Kama Watanzania hawaijui katiba, basi hakuna haja ya kuwa na Serikali, hakuna haja ya kuwa na Bunge wala hakuna haja ya kuwa na Mahakama. Turudi kwenye utawala wa jadi ambao haukuwa na katiba...
Mimi hofu yangu badala ya wananchi kuelemishwa kuhusu maudhui ya Katiba iliyopo kuna hatari ya watu wengine wakorofi kutumia fursa hiyo kuwaelemisha wananchi kuidai Katiba mpya kwa nguvu. Ikawa tofauti na matarajio ya serikali.. tusiache mwanya huo. Rais ashauriwe vizuri, machawa wasimwingize kwenye matatizo.
 
Kwa Kifupi alichokisema

Yeye ndi mwenye Uelewa.

Kweli hayo?

Muda utaeleza, 2025 sio mbali ataelewa maana yake.
 
Kama Watanzania hawaijui katiba, basi hakuna haja ya kuwa na Serikali, hakuna haja ya kuwa na Bunge wala hakuna haja ya kuwa na Mahakama. Turudi kwenye utawala wa jadi ambao haukuwa na katiba...
Mm nakwambia ndugu yangu watu hawajui wanaongea nn,wako madarakani na hawajui walikwendaje pale walipo,tukiwaambia hawaijui nchi wanakasirika na wanakuja na mipasho ya pwani wakidhani nchi inaongozwa kwa mipasho.

Kusema watanzania hawajui katiba ni MATUSI makubwa yy Mama SAMIA SULUHU HASSAN kama haijui katiba ni Uzembe wake lkn asijumuishe kutokujua kwake katiba basi watanzania wote hawajui katiba.

Watanzania wameshasema na wanaendelea kusema kila siku juu ya namna wanavyotaka nchi yao iongozwe.Kuijua Tanzania na watanzania ni muhimu sana unapokuwa kiongozi wa nchi.
 
Kama Watanzania hawaijui katiba, basi hakuna haja ya kuwa na Serikali, hakuna haja ya kuwa na Bunge wala hakuna haja ya kuwa na Mahakama. Turudi kwenye utawala wa jadi ambao haukuwa na katiba.

Kama wananchi hawajui katiba, Serikali, Bunge na mahakama vinapatikana kwa njia gani? Au ndiyo maana wanajipa Urais, wanajipa ubunge na udiwani bila ya kuchaguliwa na wananchi?

Serikali na Rais, Bunge na wabunge, mahakama na majaji, wote upatikanaji wake umeelekezwa na katiba. Kama wananchi hawajui katiba, hakuna haja ya kuwa na uchaguzi, wala hakuna haja kuwa na Rais, Serikali, Bunge, Mahakama, Polisi wala wala mahakama. Wale machifu wa kale, warudishwe kuongoza makabila yao. Wazee wenye hekima, warudishwe kuwahukumu wanaokosea.

Haiwezekani useme wananchi hawaielewi katiba, halafu wewe Urais wako uwe halali. Kama wananchi hawaelewi katiba, na wewe uliyetakiwa kupatikana kwa maelekezo ya katiba, huwi halali, unatakiwa kuondoka au kuondolewa. Ina maana umetumia ujinga wa wasioelewa katiba, kujipa madaraka na mamlaka.
Akili kubwa sn
 
Mamlaka yanatoka kwa wananchi wasiyojua walivyoyatoa.
Je inabidi wayachukue kwanza , halafu waweke utaratibu wa kuyatoa upya? Au wananchi wamenyang'anywa kwa sababu ya ujinga?
Tunahitaji watu wenye uwezo wa kuishauri serikali itoe hoja zenye mantiki na kueleweka wakati wote. Ukila na kipofu usimshike mkono.
 
Kwa Kifupi alichokisema

Yeye ndi mwenye Uelewa.

Kweli hayo?

Muda utaeleza, 2025 sio mbali ataelewa maana yake.
Watu wenye uwezo mdogo wakipewa mamlaka huamini kwa kupewa mamlaka, wameongezewa na akili.
 
Nadhani hoja ya C D Msuya kuhusu kujibu hoja za CDM ni ya kuzingatiwa na sisi CCM ili kwenda na kasi ya sasa hali ya kisiasa
 
Back
Top Bottom