Kama Uchaguzi Mkuu Ungefanyika Leo...

maggid,
just curious, Umeamua kubandika hii tena?

Na Maggid Mjengwa,

HUU ni mjadala niliouanzisha kule kwenye jukwaa la Jamii (www.jamiiforums.com). Nauendeleza hapa ili uwafikie wengi zaidi.
Ni tathimini yangu. Ni mtazamo wangu huru. Katika kuishi kwangu kuna chaguzi nilizozishuhudia kwa macho na nilizosoma vitabuni. Hivyo, ninachoandika kinatokana na uzoefu wangu wa kufuatilia kwa karibu mienendo ya chaguzi zetu.
 
Mwafrika,

Tofauti na nilichoandika huku nikifikiri kwenye Jamii Forums, hayo ni mawazo niliyoyaweka sawa kwenye karatasi na kisha kuyachapa na kuyatuma gazetini. Ni mwendelezo wa fikra. Na lengo hapa ni kupata mawazo tofauti kutoka kwa watu tofauti. Kutakuwa na cha kujifunza. Naamini.
 
Mwafrika,

Tofauti na nilichoandika huku nikifikiri kwenye Jamii Forums, hayo ni mawazo niliyoyaweka sawa kwenye karatasi na kisha kuyachapa na kuyatuma gazetini. Ni mwendelezo wa fikra. Na lengo hapa ni kupata mawazo tofauti kutoka kwa watu tofauti. Kutakuwa na cha kujifunza. Naamini.

Fair enough
 
jasusi,
ahsante sana. Nimefuatilia kwa karibu kampeni za mwaka huu tangu agosti 28 na kipindi kabla ya kampeni. Tunaelewa kuwa takribani asilimia 79 ya wapiga kura wa tanzania wako maeneo ya mashambani. Na huko ndiko ccm inapotegemea sana kuchota kura zake. Ndio maana ya kuandika; kwa chama au vyama vya upinzani kufanikiwa kukiondoa chama kilicho madarakani katika nchi zetu hizi , ni lazima wafike iliko mizizi ya wapiga kura wake. Nina bahati ya kutembea vijijini. Ukweli huko vijijini hali ni tofauti na sehemu za mijini. Na nilichoandika ni kama uchaguzi mkuu ungefanyika leo. Bado tuna mwezi na nusu umebaki. Katika siasa lolote laweza kutokea.

ndio maana mzee makamba akajitoa katika midahalo ya kwenye tv!.. Akawaachia wanachadema
 
Ulishaweka hizo findings zako za kijiweni zikapingwa.Umezirejesha tena ukidhani zitaaminiwa au ndio katika kuhalalisha ujira wa kumkampenia Alhaji Kikwete?
 
Mbinu pekee inayoweza kuifanya ccm kuanguka ni kwa wapinzani kuungana na kugawana majimbo kulingana na nguvu walizonazo. kwa mfano cuf wangepewa mikoa ya kusini, pwani na zanzibar, chadema mikoa ya kaskazini na magharibi na mingineyo halafu mkoa wa shinyanga ingeachiwa UDP. Hii ingewasaidia sana wapinzani kwanza kwa kuokoa kiasi kikubwa cha fedha na muda mwingi wa kuzunguka nchi nzima na pia itawawezesha kuwashambulia ccm kirahisi kwa sababu itawabidi CCM wajikute wanazunguka nchi nzima kupambana na wapinzani na pia hawatokuwa na muda wa kujikita sehemu moja kwani watakuwa wakipigwa kutoka pande zote za nchi. faida nyingine kubwa ni kwamba mgombea kuwa mmoja wa upinzani na JK , hii inawapunguzia wananchi kazi na pia inakuwa rahisi kwani mgombea huyo atakuwa anafanyiwa kampeni na vyama vyote vya upinzani kwahiyo hii itampunguzia mgombea wa upinzani gharama kubwa ktk kuwafikia wananchi. hii itasaidia wapinzani kupata majimbo mengi na hata kuweza kushinda kiti cha urais.
 
Maggid,

Kwanza nikushukuru kwa article yako ambayo imegusia mambo mengi kuhusu siasa za nchi yetu. Nimefurahi kwamba umeileta hapa jamvini; kwa hiyo, wanabodi watapata nafasi ya kukujibu bila ya mawazo yao kuchujwa tofauti na kwenye Blog yako.

Kwenye article yako umezungumzia nguvu na mapungufu ya vyama mbali mbali kijuujuu (superficially) sana. Ni kweli CCM imejenga mpaka vijijini, lakini hii haitokani na ugenious wa viongozi wake bali historia ya nchi yetu. Chama hiki kimebahatika kwa kuwa kwa muda mrefu kwa kuwa nchi yetu ilikuwa ni chama kimoja, ni katika kipindi hiki tuliamini ya kuwa Chama kimeshika hatamu. Katika makosa ambayo Mwl. Nyerere aliwahi kuyafanya ni kujenga chama ambacho kilikuwa na nguvu sana, kuanzia kwenye shina,tawi ,mkoa ....Kutokana na hili, Mwl. Nyerere hakutoa kipaumbele katika kujenga strong instututions (mahakama, Bunge n.k) ambazo zingekuwa independent na zingeweza kumkomboa mwananchi.

Ni katika kipindi hiki cha chama kimoja, watanzania wengi walilazimishwa kuchangia chama hiki. Nani asiyejua viwanja kama vya Jamhuri Dodoma, Kirumba Mwanza vilijengwa kutumia resource za serikali na michango ya wananchi? Maggid, kwa nini ujagusia hiyo unfair advantage kwenye article yako? Hivi ni vitu ambavyo Mwandishi yeyote makini angegusia. Kwa maana nyingine CCM ina vyanzo vingi vya vipato ambavyo ni mali ya watanzania.

Pia umeshindwa kugusia ni jinsi gani katiba yetu ilivyo incompatible na siasa ya vyama vingi. Katiba hii imempa Rais uwezo wa kuchagua tume ya uchaguzi as well as Msajili wa vyama vya siasa vitu ambayo JK anatumia katika supress upinzani. Ni juzi tuu wananchi wa Arusha waliamriwa kufunga biashara kwa sababu Kikwete anafanya mkutano wa kampeni. Upinzani hauwezi kukua wakati uwanja wa kuchezea mpira hauko sawa!


Mwisho, katika mapungufu ya CCM sijaona ukizungumzia kuhusu ubadhirifu na ufisadi uliokithiri! Ni nani asiyejua ya kuwa mabilioni ya shilingi yallibiwa benki kuu chini ya serikali ya ccm, mikataba mibovu ya madini inayowanufaisha wageni na kuwaacha mamilioni ya watanzania under abject poverty ilisimamiwa na serikali ya CCM. Ni nani asiyejua ya kuwa mashirika muhimu kama TRC yaliyokuwa silaha ya wanyonge yameuwawa na serikali ya ccm ?


Maggid, Nashindwa kuelewa unapojifanya kuwa impartial wakati true color zako zinaonyesha ya kuwa unaishangilia ccm blindly.
 
With all due respect Mjengwa, sikubaliani na findings zako. Kigezo gani ulichotumia kufikia hiyo conclusion kuwa ccm watashinda? Hii ni ccm ya JK siyo CCM ya JKN. Kama watanzania hawajaona hilo, basi ni kuhalalisha ccm itawale milele. Hii ni ccm iliyofuta Azimio la Arusha, iliyoondoa misingi yote ya baba wa Taifa, kuwa cheo ni dhamana, rushwa ni audi wa haki, na binadamu wote ni sawa. Hii ni ccm tunayoambiwa kuwa elimu kutolewa bure haiwezekani. Wote tunafahamu, tukiwemo wewe na mimi, na JK na mawaziri wake wengi ambao tulikuwa nao mashuleni na vyuoni enzi za Mwalimu, kuwa tulisoma bure kuanzia shule za msingi mpaka chuo kikuu. Hatukulipa ada, hatukulipia vitabu, wala madawati. Na hatukuwa na tuition ya baada ya shule. Waalimu wetu waliwajibika ipasavyo, mitihani haikuibiwa na wanafunzi walifaulu kwa kiasi kikubwa. Iliwezekana wakati ule, haiwezekani leo. Wakati kila mmoja wetu anafahamu kuwa Tanzania ya leo imeendelea zaidi kuliko wakati ule, nadhani hata kirasilmali na uwezo wa kuzitumia kwa makini zaidi sasa tunaweza zaidi. Tanzania ya leo inao wataalamu wengi zaidi wa kila fani, hata wa kuweza kuishauri serikali vizuri zaidi tunao. Wataalamu wazawa, sio wa kigeni wapo kwenye kila fani. Kama bado tunaifagilia ccm, pamoja na kuwa upeo wetu umeendelea kuliko miaka mitano iliyopita, ni kuisaliti nchi yetu. Watu wa vijijini wanaweza kuwa hawafahamu kama ccm siyo CCM. Lakini ni jukumu letu wewe, mimi na yule kuwaeleza hivyo, ili wafanye uamuzi wenye busara, utakaoweza kuikomboa nchi yetu. Mwalimu aliwahi kusema, CCM sio baba yangu wala mama yangu. Mtu yeyote anayefikiria ccm ni baba yake au mama yake ni msaliti wa watanzania. Mjengwa una nafasi nzuri sana ya kuwaelimisha watanzania kupitia blog yako. Unaweza kuwaelimisha hata watu walioko huko vijijini ambako mara nyingi huwa unatuletea picha za matukio mbalimbali. Kwa maoni yangu unachokifanya hapa ni kupigia debe mafisadi na washirika wao, ambao hawaitakii mema nchi yetu.
 
Maggid, katika makala zako nne ama tano za mwisho katika Raia Mwema umekuwa ukionyesha waziwazi kuipigia sana debe CCM na mgombea wake JK. Ni haki yako kimsingi lakini fanya kwa uwazi kwamba wewe ni mshabiki/mwanachama wa CCM na JK bila kujificha ficha. Makala moja ya nyuma kidogo ulidai'...kuona wananchi wakisimama barabarani kuzunguka redio ama Tv kusikiliza/kuangalia hotuba ya JK ni ishara ya kukubalika JK kwa wananchi' iliniacha hoi.
Kuna makala nyingine uliwalaumu sana baadhi ya waandishi wanaoandika makala zao kwa dhihaka ama kutumia kejeli hasa pale walipokuwa wanamzungumzia JK.
Mimi ninaamini kuwa hukupaswa kuwahukumu waandishi wenzio kwa kuwataka watumie aina fulani ya lugha kwa vile tu walielekea kumkejeli JK.
Kila muandishi ana haki ya kutumia aina yake ya uandishi kufikisha ujumbe wake kwa jamii aliyoilenga ilimradi tu havunji sheria. Mwenye kutumia kejeli na atumie, mwenye kuandika ngonjera na aandike, wa vibonzo achore. wa maigizo na aigize, wa nyimbo na aimbe na wa ngoma acheze ili kuwaelemisha wananchi wetu kuhusu haki yao ya kimsingi ya kumchagua raisi atakayewafaa. Ukiona raisi umpendaye anakejeliwa usikasirike na kuwataka waandishi wenzako kuandika aina ya uandishi unaotaka wewe.
 
Maggid? ninaanza kukuelewa. kwa nini unawadhihaki Chadema kwa kukosa pesa? nadhani bila pesa tutashinda, ndio maana ya peoples power.
 
Maggid, katika makala zako nne ama tano za mwisho katika Raia Mwema umekuwa ukionyesha waziwazi kuipigia sana debe CCM na mgombea wake JK. Ni haki yako kimsingi lakini fanya kwa uwazi kwamba wewe ni mshabiki/mwanachama wa CCM na JK bila kujificha ficha. Makala moja ya nyuma kidogo ulidai'...kuona wananchi wakisimama barabarani kuzunguka redio ama Tv kusikiliza/kuangalia hotuba ya JK ni ishara ya kukubalika JK kwa wananchi' iliniacha hoi.
Kuna makala nyingine uliwalaumu sana baadhi ya waandishi wanaoandika makala zao kwa dhihaka ama kutumia kejeli hasa pale walipokuwa wanamzungumzia JK.
Mimi ninaamini kuwa hukupaswa kuwahukumu waandishi wenzio kwa kuwataka watumie aina fulani ya lugha kwa vile tu walielekea kumkejeli JK.
Kila muandishi ana haki ya kutumia aina yake ya uandishi kufikisha ujumbe wake kwa jamii aliyoilenga ilimradi tu havunji sheria. Mwenye kutumia kejeli na atumie, mwenye kuandika ngonjera na aandike, wa vibonzo achore. wa maigizo na aigize, wa nyimbo na aimbe na wa ngoma acheze ili kuwaelemisha wananchi wetu kuhusu haki yao ya kimsingi ya kumchagua raisi atakayewafaa. Ukiona raisi umpendaye anakejeliwa usikasirike na kuwataka waandishi wenzako kuandika aina ya uandishi unaotaka wewe.

Babadesi,

Nakubaliana na wewe kabisa kwamba Maggid anatakiwa awe mkweli na wasomaji wake kwa kusema wazi kuwa yeye ni mshabiki wa CCM na zaidi JK. Mara nyingi kwenye makala zake anajaribu kuonyesha kama mtu asiyefungamana na upande wowote, lakini ukisugua kidogo tuu chini ya sakafu utaziona rangi zake zote. Ukisoma nakala yake hakuzungumzia kabisa mapungufu ya msingi ya CCM na mbaya zaidi huyu ni mtu anayesafiri kila siku vijijini anaonana matatizo yanayowakabili wananchi.
 
hongera bwana majid ,kwa makala yako nzuri yenye uchambuzi wa kina ,watanzania wengi,
hawataki kupata uchambuzi yakinifu,ccm watashinda ila baada ya ushindi zipo changamoto yafaa wazifanyie kazi,mfano matumizi ya matokeo ya kura za maoni,uteuzi wa watendaji kama makatibu,madc au rc,nk kifupi nimefurahia mada yako
 
magid,
deep down wewe ni CCM,watu wanapenda kusoma makala zako ila unapoelekea sasa utapoteza wapenzi...kuwa mwandishi huru hata kama kuna kitu umepewa na akina rostam
 
Maggid sijui kawaje siku hizi! Naona ana mapenzi binafsi na Kikwete. Fuatilia anachoandika Raia Mwema!
 
Maggid sijui kawaje siku hizi! Naona ana mapenzi binafsi na Kikwete. Fuatilia anachoandika Raia Mwema!

Unajua hawa jamaa, Maggid na pia Ramadhan Semtawa wa Mwananchi, ni vichekesho katika tasnia ya habari. Ukisoma maandiko yao, wana muelekeo wa kuuibeba CCM, na hasa JK. Lakini wamekuwa wepesi wa kutuzuga kwamba hawaegemei upande wowote.

Wandugu nyinyi msitufanye sisi wasomaji kuwa wajinga. Kwanza we Maggid kile kigazeti chako cha Kwanza Jamii kimeishia wapi?
 
Ndugu Zangu,

Kuna mlionielewa nilichoandika, ahsanteni. Kuna ambao pia mmepingana na nilichoandika, ahsanteni pia. Nafikiri ni busara mtu akajibu hoja iliyowasilishwa badala kumshambulia mtoa hoja. Bahati nzuri mimi siogopi kushambuliwa. Nahofia tu kuna wengine wenye kuingiwa hofu hata ya kutoa fikra zao huru kwa hofu ya kushambuliwa. Kumfanya mtu aogope kuandika anachofikiri hata wakati mwingine kuogopa kutumia jina lake halisi ni aina ya ' Ukandamizaji wa kifikra'.

Katika kile nilichoandika na kuchapwa kwenye Raia Mwema, kuna WanaCCM walionijia juu kwa kunitumia sms na hata kunipigia sikmu kwa kuamini nimewabeba CHADEMA na kuna WanaChadema walionijia juu kwa kutumia njia hizo za mawasiliano wakiamini nimewabeba CCM. Kama mwandishi wa makala na mchambuzi hilo kwangu ni jambo jema. Naamini kwa kiasi kikubwa nimefanikiwa kiundishi katika makala husika.

Labda niwahakikishie tu. Nitaendelea kuandika kwa uhuru kabisa kila nitakapokuwa na cha kuandika. Sina cha kuhofia. Na naamini kama mwanadamu sijakamilika. Nitakayoyaandika mengine yana mapungufu, na wataoyapokea maandiko yangu watakuwa na mitazamo tofauti. Na ndiyo demokrasia hiyo. Ndio maisha yalivyo. Ndio maana ya maisha. Tukutane tena.
 
Wana JF naomba nianze kwa kusema kuwa binafsi sina ushabiki wa chama chochote na wala kwenye uchaguzi sitapiga kura.Lakini hilo halinifanyi nishindwe kutoa maoni yangu maana hili ni jukwaa na na kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni ili mradi havunji sheria za JF.Kwa upande wa mada ya Mjengwa mimi binafsi ninampongeza Mjengwa kwa ujasiri aliouonyesha katika kutoa maoni.Wengi humu ndani mmepinga study aliyoifanya lakini ni lazima tukumbuke kuwa kwa mujibu wa kazi yake(maendeleo ya jamii)ana nafasi kubwa zaidi ya kukutana na watanzania wa kawaida kuliko wengi wetu humu hata kama tunaenda vijijini.Amejitahidi kueleza vizuri sana mapungufu aliyoyaona na kwa hilo ninampa pongezi.Tatizo la wengi humu JF ni kwamba hamtaki kuambiwa ukweli na mnafikiria kuwa mnachokijua ninyi basi ndio sahihi.Unapomhukumu Mjengwa Kwa utafiti wake unakuwa umefilisika kimawazo kwa kufikiria kuwa wenye haki ya kufanya utafiti ni Redet,Maprofesa,na watafiti mnaowakubali nyie.Mjengwa kutokana na kazi yake kila siku yuko vijijini na binafsi ninaamini alichokisema maana hata mimi niliweka thread hapa hapa lakini haikupata wachangiaji ila nimekuwa mstari wa mbele kuwakumbusha hilo la wakazi wa vijijini.Nasema hivyo kwa kuwa nami nimeishi vijijini na kujionea kwa macho yangu hali halisi.Ninawaomba msijiliwaze na majimbo mliyoshinda katika baadhi ya vijiji mkafikiri hali ni hiyo nchi nzima.Alichofanya Mjengwa kwa nilivyomuelewa ni kuwakumbusha tu kuwa hali bado si nzuri kwa upande wa wapinzani.mlichotakiwa kufanya ni kuyafanyia kazi mawazo kama haya na sio kumshambulia na kumwita majina mbalimbali.Msidanganyike na idadi ya watu mikutanoni ambao waweza kukuta ni walewale ambao leo wanasikiliza CHADEMA kesho wako kwenye mkutano wa CCM.Na haya yote tunayoyajadili hapa ni watanzania wangapi wana uwezo wa kuyasoma.Chonde chonde jamani jaribuni kuangalia na kukubali kukosolewa wakati bado muda unaruhusu.Fanyieni kazi mawazo yanayowaonyesha udhaifu wenu na sio kujibu kwa kumchambua mtoa hoja nakuonyesha mna uwezo kiasi gani wa kutoa hoja maana wengine mmegraduate kwenye BA in critisism.Kubalini mawazo tofauti ili mjenge, mtashinda vipi wakati kuna watanzania bado wanasema hali yetu ya shida tu hata waje wapinzani na wengine wanasema sisi ni CCM tu kwa kuwa imetupa uhuru(wala hawajui kuwa ni TANU iliyoleta uhuru).Jaribuni kukubaliana na mawazo yanayopinzana nanyi na myafanyie kazi katika kujenga bila ya hilo, tupo hapa na tutawauliza vipi viliendekaje?
 
Jaribuni kukubaliana na mawazo yanayopinzana nanyi na myafanyie kazi katika kujenga bila ya hilo, tupo hapa na tutawauliza vipi viliendekaje?

Kwa hiyo unakubali kuwa hapa JF tupo sisi na ninyi na kwa mantiki hiyo mawazo lazima yatofautiane. Kama ni hivyo kwa nini humshauri na huyo maggid na yeye akubaliane na mawazo yanayopingana na yake ? Anadai kafanya utafiti sawa, sasa anajuaje kama wengine hatuna tafiti zetu zinazoonyesha vinginevyo. Kwa nini maggid na yeye asifanyie kazi mawazo yetu wengine ? Na sisi tuko hapa na tutawauliza vipi viliendekaje Paka mweusi ?
 
Kwa hiyo unakubali kuwa hapa JF tupo sisi na ninyi na kwa mantiki hiyo mawazo lazima yatofautiane. Kama ni hivyo kwa nini humshauri na huyo maggid na yeye akubaliane na mawazo yanayopingana na yake ? Anadai kafanya utafiti sawa, sasa anajuaje kama wengine hatuna tafiti zetu zinazoonyesha vinginevyo. Kwa nini maggid na yeye asifanyie kazi mawazo yetu wengine ? Na sisi tuko hapa na tutawauliza vipi viliendekaje Paka mweusi ?

Mjomba unapitia maoni ya watu au unajibu unapoona umeguswa?Yeye ameshakubali zamani waliotofautiana naye kimawazo tatizo ni ninyi ambao kila kitu mnakijua na hamtaki kukubali kuambiwa hali halisi.Ukumbuke kuwa Mjengwa hana chama cha siasa na wala si mgombea ila ninyi ndio mnaopigia debe chama fulani na hamtaki kuelezwa mapungufu yenu ,wanayoyaona ni wale walio nje.Hivyo basi siwezi kumshauri Mjengwa kwa kuwa naye ni raia kama mimi, ila nyie tutawashuri kwa sababu mna matarajio makubwa sana wakati hali halisi inajieleza tofauti.Si uliona Tanzania ilivyocheza mechi na Brazil ,kuna watanzania waliotamba na kusema lazima tuifunge Brazil utaifunga vipi Brazil wakati maandalizi yako ni madogo?Ndio nyie sasa.Fanyieni kazi maoni ya watu wa kawaida sio mpaka aseme profesa Baregu.Na narudia tena tupo hapa msijekubadilisha Id s tu.Kumradhi mkuu nimefananisha siasa na mpira lakini ndio mfano uliokuwa karibu.
 
Back
Top Bottom