Kama tunataka Muungano, lazima Muundo Ubadilishwe

Kama tunataka Muungano, lazima Muundo Ubadilishwe

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,940
Kwa muundo wa Muungano wetu, hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, mkweli wa nafsi na asiye mnafiki, anayeweza kutetea kuwa muundo huu uliopo upo sawa sawa.

Ndiyo maana watu wote maarufu, wenye akili na maadili yasiyotia shaka, bila ya kujali vyama vyao, dini zao au umri wao, hakuna hata mmoja atakuambia kuwa muundo wetu wa Muungano upo vizuri.

Ndiyo maana Kinana alipotaka kuupinga ukweli, alionekana kujidhalilisha zaidi na kuonekana mtu mnafiki na aliyekosa uzalendo, kwa sababu alishindwa kuzijibu hoja za Lisu, Jaji Nyalali, Jaji Warioba, Wabunge G55, akaishia kupiga porojo.

Lisu, kwenye suala la Muungano, alichokisema hazikuwa porojo, hayakuwa majungu bali aliuongea ukweli mtupu. Kwenye ukweli, hata umlete nani, hataweza kuufanya uonekane ni uwongo. Zaidi kitakachotokea ni kumdhalilisha na kumvunjia heshima huyo mtu anayeukana ukweli, kama ilivyotokea kwa Kinana.

Hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, awe CCM, CHADEMA, ACT au asiye na chama, ambaye atasema muundo wa Muungano huu uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar, upo sawa:

Tume ya Warioba ilitamka muundo wa Muungano upo hovyo.

Wabunge 55 wa CCM, walitamka kuwa muundo wa Muungano upo hovyo. Wakaungwa mkono na wabunge wote wa CCM. Serikali ya CCM chini ya Rais Mwinyi ikakubali kuwa muundo wa muungano ni hovyo, ikaridhia iundwe Serikali ya Tanganyika. Nyerere ambaye alikuwa mwenyekiti wa CCM, mtu mmoja tu, akakataa.

Tume ya Jaji Nyalali ilitamka kuwa muundo wa Muungano ni hovyo.

Lisu leo anachokitamka siyo kipya, bali anakazia kinachojulikana na kukubaliwa na wote wenye akili timamu na walio wakweli.

Kwa sasa hakuna mtu hata mmoja mwenye akili timamu anayeweza kusimama hadharani kuwa muundo wa Mungano wetu upo vizuri.

Wananchi tusimame na hawa wenye akili na walio wakweli.

Mimi naamini, kwenye hili, hata Rais Samia, japo hajatoa kauli yoyote hadharani, ataungana na wenye akili kukiri kuwa muundo wa Muungano siyo sawa, unahitaji marekebisho makubwa. Labda anachokosa ni ujasiri wa kunena, hasa kwenye hatua ya sasa.

Nina hakika siku ambayo Samia atasema kuwa, Muungano wetu unahitaji marekebisho, machawa wajinga wote, mtawaona namna watakavyomshangilia na kumsifu.
 
Kwa muundo wa Muungano wetu, hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, mkweli wa nafsi na asiye mnafiki, anayeweza kutetea kuwa muundo huu uliopo upo sawa sawa.

Ndiyo maana watu wote maarufu, wenye akili na maadili yasiyotia shaka, bila ya kujali vyama vyao, dini zao au umri wao, hakuna hata mmoja atakuambia kuwa muundo wetu wa Muungano upo vizuri.

Ndiyo maana Kinana alipotaka kuupinga ukweli, alionekana kujidhalilisha zaidi na kuonekana mtu mnafiki na aliyekosa uzalendo, kwa sababu alishindwa kuzijibu hoja za Lisu, Jaji Nyalali, Jaji Warioba, Wabunge G55, akaishia kupiga porojo.

Lisu, kwenye suala la Muungano, alichokisema hazikuwa porojo, hayakuwa majungu bali aliuongea ukweli mtupu. Kwenye ukweli, hata umlete nani, hataweza kuufanya uonekane ni uwongo. Zaidi kitakachotokea ni kumdhalilisha na kumvunjia heshima huyo mtu anayeukana ukweli, kama ilivyotokea kwa Kinana.

Hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, awe CCM, CHADEMA, ACT au asiye na chama, ambaye atasema muundo wa Muungano huu uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar, upo sawa:

Tume ya Warioba ilitamka muundo wa Muungano upo hovyo.

Wabunge 55 wa CCM, walitamka kuwa muundo wa Muungano upo hovyo. Wakaungwa mkono na wabunge wote wa CCM. Serikali ya CCM chini ya Rais Mwinyi ikakubali kuwa muundo wa muungano ni hovyo, ikaridhia iundwe Serikali ya Tanganyika. Nyerere ambaye alikuwa mwenyekiti wa CCM, mtu mmoja tu, akakataa.

Tume ya Jaji Nyalali ilitamka kuwa muundo wa Muungano ni hovyo.

Lisu leo anachokitamka siyo kipya, bali anakazia kinachojulikana na kukubaliwa na wote wenye akili timamu na walio wakweli.

Kwa sasa hakuna mtu hata mmoja mwenye akili timamu anayeweza kusimama hadharani kuwa muundo wa Mungano wetu upo vizuri.

Wananchi tusimame na hawa wenye akili na walio wakweli.

Mimi naamini, kwenye hili, hata Rais Samia, japo hajatoa kauli yoyote hadharani, ataungana na wenye akili kukiri kuwa muundo wa Muungano siyo sawa, unahitaji marekebisho makubwa. Labda anachokosa ni ujasiri wa kunena, hasa kwenye hatua ya sasa.

Nina hakika siku ambayo Samia atasema kuwa, Muungano wetu unahitaji marekebisho, machawa wajinga wote, mtawaona namna watakavyomshangilia na kumsifu.

Huu ni uvamizi, Wazanzibari hatuutaki tunataka nchi yetu kila mmoja aishi ki vyake tumechoka
 
Muungano tunautaka ila ni kweli kwa mahitaji ya sasa muundo huu haufai kwa wakati huo huu muundo ulikuwa sahihi kabisa na sababu zake na mazingira yake ya wakati huo, ulifaa, kwa sasa haiwezekani.Akina Nape acheni hoja nyepesi oh! tumezaliwa baada ya muungano hatuijui Tanganyika.NI Hoja mufilisi issue ni kero zilzopo na hakuna anayetaka kuuvunja. Ni hofu tu za mabadiliko zinawasumbua lakini sababu zilezile za Kizazi cha sasa kuwa wanajiuliza kwa nini tuteseke na muundo huu wenye ubaguzi kwa pande zote mbili. wenye kunufaika na muundo huu ni wachache mno. wananchi walio wengi wametengwa
 
Hoja zao zina mashiko

Litakuwa jukumu la nani kuendesha gharama za serikali ya tatu ya Muungano?

Je, serikali ya Z'bar wataweza kusimama wenyewe?

Au zigo lote litaiangukia serikali ya Tanganyika?
 
Muungano tunautaka ila ni kweli kwa mahitaji ya sasa muundo huu haufai kwa wakati huo huu muundo ulikuwa sahihi kabisa na sababu zake na mazingira yake ya wakati huo, ulifaa, kwa sasa haiwezekani.Akina Nape acheni hoja nyepesi oh! tumezaliwa baada ya muungano hatuijui Tanganyika.NI Hoja mufilisi issue ni kero zilzopo na hakuna anayetaka kuuvunja. Ni hofu tu za mabadiliko zinawasumbua lakini sababu zilezile za Kizazi cha sasa kuwa wanajiuliza kwa nini tuteseke na muundo huu wenye ubaguzi kwa pande zote mbili. wenye kunufaika na muundo huu ni wachache mno. wananchi walio wengi wametengwa
Kaunganeni na Kagame na yule wa Burundi wanautaka , sisi Wazanzibari tumechoka tuwacheni tupumue tushughulike na Zanzibar yetu
 
Kwa sasa hakuna mtu hata mmoja mwenye akili timamu anayeweza kusimama hadharani kuwa muundo wa Mungano wetu upo vizuri.
Unajuwa kwa nini?
Hata huyo Nyerere unayemsingizia kwamba ni yeye pekee "alikataa", akirudi leo na kukuta huu Muungano ulivyo sasa atakwambia hautaki muungano wenye muundo huo.

Nyerer alipokuwa yungali hai hapakuwepo na " nchi kamili ya Zanzibar,"yenye bendera yake na mipaka yake iliyoainishwa, na mali asili zote zilizomo ndani ya nchi hiyo ikiwa ni mali yake. Zanzibar haikuwa na Katiba yake, na haikuwa na lengo la kujiondoa waziwazi toka kwenye muungano

Ni mambo mangapi yaliyokuwa chini ya muungano, na sasa zinazoitwa "kero" zimeyafikisha wapi mambo hayo!
Hatua hizo zimeimarisha muungano, au zimedhoofisha muungano?

Kwa hiyo, sote tunapolalamikia muungano sasa hivi, ni wazi kabisa ni muundo usiofaa kutokana na juhudi za ziada zinazofanywa na kundi ambalo toka mwanzo halikuutaka muungano..

Lengo la mwanzo la muungano huu halikuwa kuweka vizingiti vya mara kwa mara kwa jina la kero. Hizi kero imekuwa silaha ya kundi ambalo toka mwanzo halikuutaka muungano toka visiwani. CCM ndiyo imekuwa ikitoa rushwa kwa hilo kundi kwa kupitisha hizo kero zao, huku wakijuwa wanauua muungano

Muungano uliokuwepo toka mwanzo uliundwa kwa namna hiyo kwa sababu maalum, na matazamio yake yakiwa kwamba tungefikia mahali, tukaachana na woga tuliokuwa nao mwanzo,na baada ya kila upande kuzoeana kwa kuwa pamoja.

CCM haikuruhusu hilo, badala yake kwa tamaa tu ya kuendelea kukaa madarakani wakaruhusu maadui wa muungano kuuchokonoa na kuulegeza kama ilivyo sasa.

Hapa sitazungumzia tufanye nini sasa. Kama ni kuuvunja, acha uvunjike tu, kwani CCM wameruhusu iwe hivyo.
 
Hoja zao zina mashiko

Litakuwa jukumu la nani kuendesha gharama za serikali ya tatu ya Muungano?

Je, serikali ya Z'bar wataweza kusimama wenyewe?

Au zigo lote litaiangukia serikali ya Tanganyika?
Vunja Muungano ndio utakapo anza kusikia kelele za ajabu sana toka Zanzibar. Si ajabu tukapelekwa hata kwenye mahakama ya dunia kutoa fidia kwa Zanzibar.
Hawa ni watu wetu, ni lazima tuwakumbatie kwa nguvu zote.
Gharama tunazoingia sasa kuwapa huduma, ni kidogo sana kulinganisha na gharama watakazodai wakiachiwa kwenda zao..
Ni muhimu pawepo serikali moja tu basi.
 
Unajuwa kwa nini?
Hata huyo Nyerere unayemsingizia kwamba ni yeye pekee "alikataa", akirudi leo na kukuta huu Muungano ulivyo sasa atakwambia hautaki muungano wenye muundo huo..
Nyerer alipokuwa yungali hai hapakuwepo na " nchi kamili ya Zanzibar,"yenye bendera yake na mipaka yake iliyoainishwa, na mali asili zote zilizomo ndani ya nchi hiyo ikiwa ni mali yake. Zanzibar haikuwa na Katiba yake, na haikuwa na lengo la kujiondoa waziwazi toka kwenye muungano
Ni mambo mangapi yaliyokuwa chini ya muungano, na sasa zinazoitwa "kero" zimeyafikisha wapi mambo hayo!
Hatua hizo zimeimarisha muungano, au zimedhoofisha muungano?

Kwa hiyo, sote tunapolalamikia muungano sasa hivi, ni wazi kabisa ni muundo usiofaa kutokana na juhudi za ziada zinazofanywa na kundi ambalo toka mwanzo halikuutaka muungano..

Lengo la mwanzo la muungano huu halikuwa kuweka vizingiti vya mara kwa mara kwa jina la kero. Hizi kero imekuwa silaha ya kundi ambalo toka mwanzo halikuutaka muungano toka visiwani. CCM ndiyo imekuwa ikitoa rushwa kwa hilo kundi kwa kupitisha hizo kero zao, huku wakijuwa wanauua muungano

Muungano uliokuwepo toka mwanzo uliundwa kwa namna hiyo kwa sababu maalum, na matazamio yake yakiwa kwamba tungefikia mahali, tukaachana na woga tuliokuwa nao mwanzo,na baada ya kila upande kuzoeana kwa kuwa pamoja. CCM haikuruhusu hilo, badala yake kwa tamaa tu ya kuendelea kukaa madarakani wakaruhusu maadui wa muungano kuuchokonoa na kuulegeza kama ilivyo sasa.

Hapa sitazungumzia tufanye nini sasa. Kama ni kuuvunja, acha uvunjike tu, kwani CCM wameruhusu iwe hivyo.

Unalolusema upo sahihi.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa walikubaliana kuwepo na Serikali mbili kuelekea Serikali 1.
 
Muungano tunautaka ila ni kweli kwa mahitaji ya sasa muundo huu haufai kwa wakati huo huu muundo ulikuwa sahihi kabisa na sababu zake na mazingira yake ya wakati ho, ulifaa, kwa sasa haiwezekani.Akina Nape acheni hoja nyepesi oh! tumezaliwa baada ya muungano hatuijui Tanganyika.NI Hoja mufilisi issue ni kero zilzopo na hakuna anayetaka kuuvunja. Ni hofu tu za mabadiliko zinawasumbua lakini sababu zilezile za Kizazi cha sasa kuwa wanajiuliza kwa nini tuteseke na muundo huu wenye ubaguzi kwa pande zote mbili. wenye kunufaika na muundo huu ni wachache mno. wananchi walio wengi wametengwa
Tangu Nape atiishwe na mfumo wa utawala wa Magufuli hajawahi kuwa huru. Alijaribu kujitegemea wakati wa magu. Mwisho tulimwona alivyoacha alichokiamini na akampigia magu magoti na kicheko cha kujipe... Ile picha inamdhalilisha sana ingawa watoto wake wanasoma.
 
Tangu Nape atiishwe na mfumo wa utawala wa Magufuli hajawahi kuwa huru. Alijaribu kujitegemea wakati wa magu. Mwisho tulimwona alivyoacha alichokiamini na akampigia magu magoti na kicheko cha kujipe... Ile picha inamdhalilisha sana ingawa watoto wake wanasoma.
Daniel aliifia Imani

Petro alimkana Yesu
 
Unalolusema upo sahihi.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa walikubaliana kuwepo na Serikali mbili kuelekea Serikali 1.
Sasa iko wapi serikali ya pili. Tanganyika tunalaana ya kukana nchi yetu. Vaa tshirt ya Tanganyika uone kazi. Lakini mwenye nia mbaya ya kutaka kuvunja Muungano ni Samia kwa kuuza vya Tanganyika na kuacha vya Zanzibar kwa mfumo imara wa utawala Samia hakutakiwa kupewa tena nafasi ya kuongoza nchi. Tanganyika tumelaaniwa na Nyerere mungu amuweke kwenye tanuri la moto.
 
Kwa muundo wa Muungano wetu, hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, mkweli wa nafsi na asiye mnafiki, anayeweza kutetea kuwa muundo huu uliopo upo sawa sawa.

Ndiyo maana watu wote maarufu, wenye akili na maadili yasiyotia shaka, bila ya kujali vyama vyao, dini zao au umri wao, hakuna hata mmoja atakuambia kuwa muundo wetu wa Muungano upo vizuri.

Ndiyo maana Kinana alipotaka kuupinga ukweli, alionekana kujidhalilisha zaidi na kuonekana mtu mnafiki na aliyekosa uzalendo, kwa sababu alishindwa kuzijibu hoja za Lisu, Jaji Nyalali, Jaji Warioba, Wabunge G55, akaishia kupiga porojo.

Lisu, kwenye suala la Muungano, alichokisema hazikuwa porojo, hayakuwa majungu bali aliuongea ukweli mtupu. Kwenye ukweli, hata umlete nani, hataweza kuufanya uonekane ni uwongo. Zaidi kitakachotokea ni kumdhalilisha na kumvunjia heshima huyo mtu anayeukana ukweli, kama ilivyotokea kwa Kinana.

Hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, awe CCM, CHADEMA, ACT au asiye na chama, ambaye atasema muundo wa Muungano huu uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar, upo sawa:

Tume ya Warioba ilitamka muundo wa Muungano upo hovyo.

Wabunge 55 wa CCM, walitamka kuwa muundo wa Muungano upo hovyo. Wakaungwa mkono na wabunge wote wa CCM. Serikali ya CCM chini ya Rais Mwinyi ikakubali kuwa muundo wa muungano ni hovyo, ikaridhia iundwe Serikali ya Tanganyika. Nyerere ambaye alikuwa mwenyekiti wa CCM, mtu mmoja tu, akakataa.

Tume ya Jaji Nyalali ilitamka kuwa muundo wa Muungano ni hovyo.

Lisu leo anachokitamka siyo kipya, bali anakazia kinachojulikana na kukubaliwa na wote wenye akili timamu na walio wakweli.

Kwa sasa hakuna mtu hata mmoja mwenye akili timamu anayeweza kusimama hadharani kuwa muundo wa Mungano wetu upo vizuri.

Wananchi tusimame na hawa wenye akili na walio wakweli.

Mimi naamini, kwenye hili, hata Rais Samia, japo hajatoa kauli yoyote hadharani, ataungana na wenye akili kukiri kuwa muundo wa Muungano siyo sawa, unahitaji marekebisho makubwa. Labda anachokosa ni ujasiri wa kunena, hasa kwenye hatua ya sasa.

Nina hakika siku ambayo Samia atasema kuwa, Muungano wetu unahitaji marekebisho, machawa wajinga wote, mtawaona namna watakavyomshangilia na kumsifu.
Hujawahi kuwa na akili. We kajitafutie mlo wako muundo wa muungano unagusa vp maisha. Waasisi wa Taifa la Tanzania walikuwa sahihi kuweka huu muundo. Sababu zimeelezwa vizuri sasa mazuzu km wewe hayawezi kuelewa mpaka yanakufa.
 
Hesabu ya huu muungano ni fupi sana someni HISABATI

Mil.60/mil.
60/1
60 ÷ 1 = 60

Tz = 60mil
Znzb= 1mil
Tanganyika = 0mil
Tng + znzb = Zanz
0 + 1 = 1= (Zanz)
Tanz + zanz
60 + 1 = 61= (Tz) + (Znz)

Kwa Mujibu wa Muungano huu hakuna kitu kinachoitwa Tanganyika ila kuna Tanzania na Zanzbar
 
Vunja Muungano ndio utakapo anza kusikia kelele za ajabu sana toka Zanzibar. Si ajabu tukapelekwa hata kwenye mahakama ya dunia kutoa fidia kwa Zanzibar.
Hawa ni watu wetu, ni lazima tuwakumbatie kwa nguvu zote.
Gharama tunazoingia sasa kuwapa huduma, ni kidogo sana kulinganisha na gharama watakazodai wakiachiwa kwenda zao..
Ni muhimu pawepo serikali moja tu basi.
Si muiweke moja , muone mtavyoongeza dau 😝😝😝 akili ni mali
 
Vunja Muungano ndio utakapo anza kusikia kelele za ajabu sana toka Zanzibar. Si ajabu tukapelekwa hata kwenye mahakama ya dunia kutoa fidia kwa Zanzibar.
Hawa ni watu wetu, ni lazima tuwakumbatie kwa nguvu zote.
Gharama tunazoingia sasa kuwapa huduma, ni kidogo sana kulinganisha na gharama watakazodai wakiachiwa kwenda zao..
Ni muhimu pawepo serikali moja tu basi.
Hakika

Ni vile tu Z'bar wanapenda wawe na raisi ila tungeiga mfumo wa China na Hong Kong

Hong Kong ni special administrative region, hawana raisi, raisi wao ni wa China wao wana Chief Executive Officer of Hong Kong

Masuala ya diplomatic, military and other state-level affairs yako chini ya serikali ya China, Beijing.

Mfumo wa kiungozi wanauita One country, two systems

Why one country two systems?

Hong Kong own governmental system, legal, economic and financial affairs, including trade relations with foreign countries, all of which are independent from those of the mainland China

Hong Kong has multi-party legislatures, legal systems, police forces, separate customs territory, immigration policies, left-hand traffic, official languages, academic and educational systems, representation on certain international bodies and representation in international competitions


Z'bar kusimama kama taifa ni uongo ndio maana bado sehemu nyingi katika international affairs Z'bar huwa inawakilishwa na The United Republic of Tanzania

Mandela aliushangaa sana huu muungano alikuja bara akapigiwa wimbo wa taifa akaenda Z'bar akapigiwa tena wimbo wa taifa. Akauliza nimetembelea nchi 2 tofauti?

Nyerere akabaki na maelezo mengi mzee Mandela hakumwelewa kwa kuwa alikuwa mchizi wake akapotezea
 
Back
Top Bottom