Kama TBL mapato yanashuka, basi hali ni mbaya

Kama TBL mapato yanashuka, basi hali ni mbaya


Ripoti ya Profit and Loss inayoishia September mwaka huu, inaonyesha kuwa mapato ya TBL yameshuka.

Moderators msihamishe uzi huu:

My take:

Hii ni indicator iliyodhahiri kuwa mtaani hali ni mbaya.
Lakini ifahamike kuwa TBL ni mlipa kodi mkubwa, sasa kama hali yao nao inasuasua je hali ya kiuchumi nchini kwa ujumla ikoje?

Ni muda muafaka sasa serikali kuchukua hatua madhubuti kustabilize uchumi, la sivyo tutakwenda kwenye recession.
Hiyo ni habari nzuri Tanzania inaelekea kuwa nchi ya wapiga kazi sio walevi. Na idadi ya vifo vinavyosababishwa na ulevi vitapungua.
 
ikiyumba TBL maana yake biashara ya rejareja ya bia na vinywaji imeyumba pia.
wakilia TBL maana yake wamelia wamiliki wa baa nchi nzima
wakilia TBL maana yake watumishi wa baa nchi nzima wanalia.

Hata wale wadada pendwa pia

madhara yake yamesambaa nchi nzima kwa kiasi kikubwa.

Sekta ya hotel imelia pia

Naiona nchi kama iko msibani,imefiwa,inaomboleza,wakina mama wanapaza sauti za kilio kwa uchungu mkuu
 
tungeweza kupata data za wanywa mataputapu na gongo bila shaka tungepata picha halisi huenda kutokana na ukata watu wakaenda kunywa hizo
 
Hapo nimeona financing costs zimeongezeka. That means jamaa wametegemea zaidi fedha za mabenki katika ku finance shughuli zao za kibiashara ikiashiria hali sio njema...
 
Mwinyi amsifu magufuli kwa kazi na kasi yake ndani ya mwaka mmoja..

Huu ndo ule unafiki unaozungumzwa..
 
Siku hzi tunakunywa Jibapa. Tukiwa watano tunachanga elfu 2 kila mtu tunavuta jibapa.
Njia mpya ya kubana matumizi.

Hapo bado haujabana matumizi mwenzako nimeamua kutengeneza pombe yangu mwenyewe,natumia malighafi ya nanasi toka shambani kwangu,huko TBL sijui Serengeti hawanioni siku hizi hakuna namna.
 
Mwinyi amsifu magufuli kwa kazi na kasi yake ndani ya mwaka mmoja..

Huu ndo ule unafiki unaozungumzwa..

Sijui kwanini napata hisia Mzee Mwinyi alikwenda Ikulu kulalamika kiwanja chake kimechakachuliwa na wajanja wa mujini ndio maana waziri wa ardhi akaitwa haraka Ikulu.Haya mambo ya kusifu ilikuwa zuga tu.
 
Sijui kwanini napata hisia Mzee Mwinyi alikwenda Ikulu kulalamika kiwanja chake kimechakachuliwa na wajanja wa mujini ndio maana waziri wa ardhi akaitwa haraka Ikulu.Haya mambo ya kusifu ilikuwa zuga tu.
Labda alienda kumuonyesha dereva sehemu za gari zilizoharibika
 
Binafsi sio mtaalamu wa takwimu lakini kusema baa zifunguliwe saa 10 alasiri hadi 6 usiku ulitegemea nini!?
 
Karibuni buguruni kwa mnyamani, huku tunakunywa CHOZI LA KOBOKO! A.K.A CHAN'GAA Mchana kweupee! Hali ngumu, hata mapot! Tuko nao tunaranduka nao murraaa!!
" halooo mama mau , tuongeze pegi moja ya 500"
 
Kwa nchi ambazo azipigi ulabu na bado wanafanya mambo yao vizuri inakaaje mkuu au ndio akili za kushikiwa ndo zimekosa ubunifu mbadala?mbona ile issue ya dengu watu hawajachangamkia mkuu au ndo kusena watu wanataka hela za bure tu?
 
Hiyo ni habari nzuri Tanzania inaelekea kuwa nchi ya wapiga kazi sio walevi. Na idadi ya vifo vinavyosababishwa na ulevi vitapungua.

Hi safi sana maana hata mapato kwa sirikali yanazidi kupungua tu toka B 111 mpaka B 92 na ndo kwanza cd imewekwa kwenye deck picha likianza sijui itakuwaje si bure Sizonje anazidi kuzeeka na kuchakaa dah kweli number don't lie!
 
Kuna dada hapa kwetu ni jirani yangu,alifungua bar kwao,hata miezi6 haijafika biashara imemshida.hakuna wateja
 
Tanzania Distilleries watavuna sana.............maana viroba vinanywewa balaaa namaini yanazidi kuungua
 
Mbele kuna giza totoro, ila tuna vaa miwai ya mbao uku tukijipa moyo kuwa tutaona
 
Back
Top Bottom