Amewajibishwa Maswi na watendaji wendine wa Tanesco kwa utendaji mbaya wa Wizara ambayo anaiongoza Muhongo. Muhongo yupo kiporo anazunguka kama pia. Sasa wanapoandika waandishi wa Habari wa IPP kwa nini tunakimbilia kusema ni Mengi? Kwani wale waandishi wa IPP hawajui kutafuta habari na kwamba Mengi ndo anawatafutia habari? Kwamba Mengi kakosa Vitalu ndo maana anamshambulia Muhongo? Leteni ushahidi hapa muache hapa. Mimi naamini CAG, PCCB, TRA na Bunge hawakuwa Vihiyo kusema fedha ni za umma kwamba Muhongo awajibishwe. Na basi mtuambie kwamba Mengi aliwahonga CAG, PCCB, TRA na Bunge ili waseme kwamba pesa ni za umma. Muhongo yupo kulinda maslahi ya wakubwa na msimsingizie Mengi, mmeharibu wenyewe. Muhongo must GO.