WanaJF,
Kwa sasa imedhihirika kuwa Lowassa ni chaguo la wengi kutokana na makundi mbalimbali ya jamii kumuomba agombee nafasi ya urais. Sio wazee, wasio wakina mama, sio mashekhe na wala sio wanafunzi ambao wana kigugumizi juu ya uwezo wa Lowassa.
Kwa kuwa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu kumesikika tetesi juu ya ufisadi wake na juu ya utajiri wake. Je, hao wanaotoa tuhuma hizi ni kwanini wasitandaze ushahidi wao na kumpeleka Mamvi mahakamani? Nadhani hili lingekuwa jambo la busara sana! Maana tulishuhudia wakina Mramba, Mgonja na wengineo wakilambishwa sakafu Mahakamani. Iweje iwe ngumu kwa Mamvi?
Ifike wakati Watanzania tuwe na nguvu na ujasiri wa kudai ushahidi. Yale mazoea ya kuendeshwa kwa hisia na dhana tuachane nayo. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunapingana na siasa za majitaka ambazo zinaelekea kushamili nchini.
Yote kwa yote, Lowassa anakubalika, Watanzania tumpe nafasi.
Kwa sasa imedhihirika kuwa Lowassa ni chaguo la wengi kutokana na makundi mbalimbali ya jamii kumuomba agombee nafasi ya urais. Sio wazee, wasio wakina mama, sio mashekhe na wala sio wanafunzi ambao wana kigugumizi juu ya uwezo wa Lowassa.
Kwa kuwa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu kumesikika tetesi juu ya ufisadi wake na juu ya utajiri wake. Je, hao wanaotoa tuhuma hizi ni kwanini wasitandaze ushahidi wao na kumpeleka Mamvi mahakamani? Nadhani hili lingekuwa jambo la busara sana! Maana tulishuhudia wakina Mramba, Mgonja na wengineo wakilambishwa sakafu Mahakamani. Iweje iwe ngumu kwa Mamvi?
Ifike wakati Watanzania tuwe na nguvu na ujasiri wa kudai ushahidi. Yale mazoea ya kuendeshwa kwa hisia na dhana tuachane nayo. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunapingana na siasa za majitaka ambazo zinaelekea kushamili nchini.
Yote kwa yote, Lowassa anakubalika, Watanzania tumpe nafasi.