Kama kweli serikali ya JPM inataka kuwajua "wasiojulikana" waanze na Musiba. Kama la basi ndio wanaomtuma

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
KAMA ni kweli Serikali ya Rais Magufuli haihusiki na utekaji watu na imedhamiria seriously kutaka kuwajua wanaoitwa "wasiojulikana" ianze kwa kumkamata Syprian Musiba.

Musiba ameweka bayana kuwa ama anahusika au anawafahamu fika watu hao wanaoongozwa na Ibilisi.

Musiba amesema, "sisi kama wanaharakati tunaomuunga mkono na kumtetea Rais Magufuli wote wanaomtukana Rais tutawafuata popote mlipo iwe tweeter, Facebook au Instagram na tukikukamata tutahakikisha unabaki kilema. Wewe Mdude Chadema ninakuonya acha mara moja kumtukana Rais, wewe mtu mmoja ukifa watanzania 54 milioni wakabaki hakuna hasara". Maana ya maneno haya ni kwamba Musibu anajua waliomteka Mdude!

Musiba akijua waliomteka Mdude maana yake anajua waliomshambulia Lissu kwa mabunduki na anajua walipo Ben Saanane na Azory Gwanda maana wote hawa wamepotea kwa tuhuma ya kumtusi Rais jambo ambalo halijathibitishwa na mahakama.

Musiba anasema, "sisi wanaharakati tunaompigania Rais, tutapambana na wewe maana tunaona Polisi kitengo cha Cyber Crime na TCRA wameshindwa kazi". Hiki ni kiburi kilichovuka mawingu kama Musibu na wenzie wana uwezo zaidi ya Jeshi la Polisi linalotengewa fedha za walipakodi na Bunge kutulinda na Mali zetu lakini Musiba anaona wameshindwa kazi. Nani anampa kiburi kijana huyu?

Musiba amefikia hatua hata ya kuwa msemaji wa CCM na kuiamuru CCM wamfukuze uanachama Bernard Membe na iwajadili January Makamba, Hussein Bashe na Nape Nnauye. Musiba ameagiza.

Kana kwamba haitoshi, Musiba amelitaka Bunge kurekebisha Katiba ili muda wa uongozi wa Magufuli urefushwe aongoze miaka 14. Musiba hadi amevaa ujasiri wa kumtukana Membe "pumbavu" halafu anasema Magufuli amerejesha maadili ilhali anatukana watu kama Membe anayestahili kumzaa.

Naona aliamua kujipa mamlaka kusema yote haya lakini nadhani Polisi imepata pakuanzia kujua "wasiojulikana" ambayo ni wazi Musiba ni miongoni mwao! Akamatwe!
#AchaWoga2020
 
Nimekutukana tusi kubwa sana kama we ni mwanaume, blaal Cameroon unanifananisha na nani we mliwa 0713.....unataka niendeleee kukutukana kimoyomoyo
Only certified zombies like you n musiba use your dysfunctional brains to argue like this "Ukiwa mwenye kutzama mbali sana utaona kuwa huyu jamaa ni kichwa lkn ukiendelea kutazama zaidi utazalisha maswali meeengi ikiwa ni pamoja na kutaka kujua mfadhili wake kwenye ziara na makelele anayopiga anakuwa na faida mingi kabisa"
 
Hivi inakuaje mnakuza huyu Musiba kiasi hiki, katika jambo nnachukia nikumsikia mtu mwenye akili akimjadili Musiba, mtu mwenyewe jina la mazishi unamfungulia uzi? Haya ni matumizi mabaya ya Jf
Hapana "Kilemakyaaro" Musiba hatakiwi kuchukuliwa kiwepesi. Tawala zote ovu duniani Zina watetezi wake. Akina Hitler walikuwa na akina Heinrich Himmler, Idd Amin na Malyamungu na Bob Astles.
Nilipoyasikia aina ya maneno aliyokuwa akiambiwa Mdude ndani ya gari la watekaji mara moja hisia zangu zilikimbilia kwa Musiba. Ni aina ya maneno ambayo Musiba amekuwa akiyatumia katika kumtetea Rais Magufuli. Yamkini ndani ya gari Lile Musiba alikuwemo!!!!
 
KAMA ni kweli Serikali ya Rais Magufuli haihusiki na utekaji watu na imedhamiria seriously kutaka kuwajua wanaoitwa "wasiojulikana" ianze kwa kumkamata Syprian Musiba.

Musiba ameweka bayana kuwa ama anahusika au anawafahamu fika watu hao wanaoongozwa na Ibilisi.

Musiba amesema, "sisi kama wanaharakati tunaomuunga mkono na kumtetea Rais Magufuli wote wanaomtukana Rais tutawafuata popote mlipo iwe tweeter, Facebook au Instagram na tukikukamata tutahakikisha unabaki kilema. Wewe Mdude Chadema ninakuonya acha mara moja kumtukana Rais, wewe mtu mmoja ukifa watanzania 54 milioni wakabaki hakuna hasara". Maana ya maneno haya ni kwamba Musibu anajua waliomteka Mdude!

Musiba akijua waliomteka Mdude maana yake anajua waliomshambulia Lissu kwa mabunduki na anajua walipo Ben Saanane na Azory Gwanda maana wote hawa wamepotea kwa tuhuma ya kumtusi Rais jambo ambalo halijathibitishwa na mahakama.

Musiba anasema, "sisi wanaharakati tunaompigania Rais, tutapambana na wewe maana tunaona Polisi kitengo cha Cyber Crime na TCRA wameshindwa kazi". Hiki ni kiburi kilichovuka mawingu kama Musibu na wenzie wana uwezo zaidi ya Jeshi la Polisi linalotengewa fedha za walipakodi na Bunge kutulinda na Mali zetu lakini Musiba anaona wameshindwa kazi. Nani anampa kiburi kijana huyu?

Musiba amefikia hatua hata ya kuwa msemaji wa CCM na kuiamuru CCM wamfukuze uanachama Bernard Membe na iwajadili January Makamba, Hussein Bashe na Nape Nnauye. Musiba ameagiza.

Kana kwamba haitoshi, Musiba amelitaka Bunge kurekebisha Katiba ili muda wa uongozi wa Magufuli urefushwe aongoze miaka 14. Musiba hadi amevaa ujasiri wa kumtukana Membe "pumbavu" halafu anasema Magufuli amerejesha maadili ilhali anatukana watu kama Membe anayestahili kumzaa.

Naona aliamua kujipa mamlaka kusema yote haya lakini nadhani Polisi imepata pakuanzia kujua "wasiojulikana" ambayo ni wazi Musiba ni miongoni mwao! Akamatwe!
#AchaWoga2020
Musiba atadakwa na raia tu , tena adakwa kichovu sana ! wala usihofu mkuu , polisi wako kwa ajili ya kukamata Wana chadema , Nyalandu & co
 
Magufuli anajua kinachoendelea, anawajua wasiojulikana, mfumo wa ku tawala anao utumia ni sawa na mfumo unaotumiwa na Kagame..

Kuna vijana kama 600 walipelekwa Israel kusomea mambo kama yanayotokea Tanzania hivi sasa..

Watanzania tumshukuru sana kuwa huyu jamaa kaingia madarakani kukiwa na nguvu za Mitandao ya kijamii "social Media" la si hivyo wengi wangelipotea bila kujulikana..

Mungu ibariki Tanzania
 
Sijui ni kwanini. Mwanzoni sikuamini huu uzi ila baada ya kufuatilia kwenye mitandao mbambali ya kijamii nikajua kumbe ni kweli Musiba alisema haya maneno. Naona Tanzania tunaeleka pabaya sana kutokana na kauli za Musiba. Hizi kauli zitahifadhiwa na naamini kuna siku hata kama tumekufa Musiba atajibu haya mambo. Kwanini tunakubali mtu mmoja avunje hili Taifa? Serikali na jeshi la Polisi kwanini mkubali kutukanwa na huyu Musiba? Kwani ni nani aliye nyuma yake? Naiona Tanzania yangu ikiangamia kwa kauli za Musiba.
Asubuhi njema.
 
IMG_5795.JPG
 
Back
Top Bottom