Uchaguzi 2020 Kama Kampeni tumeshazianza kwanini tunawataka TAKUKURU na CCM wawakamate na wawakate Wanaojipitisha wakati hata Sisi wa juu tunaendelea na Kampeni?

Mzukulu

JF-Expert Member
Feb 14, 2020
1,401
2,631
WAZIRI MKUU- HUDUMA YA UMEME KUVIFIKIA VIJIJI VYOTE NCHINI:

Waziri mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli imedhamiria kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote nchini vikiwemo na vijiji 25 vya Wilaya ya Ruangwa ambavyo bado havijafikiwa na umeme.

Kufuatia hatua hiyo, Waziri Mkuu amewataka wananchi walio katika vijiji ambavyo bado havijaunganishiwa nishati ya umeme kufanya maandalizi kwa sababu maeneo mengine tayari wakandarasi wameshapatikana.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Jumanne, Juni 23, alipozungumza na wananchi katika vijiji vya Nanjaru, Nambilanje, Mkaranga, Namichiga na Mbekenyera akiwa kwenye ziara yake ya kikazi wilayani Ruangwa mkoani Lindi.

" Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli anataka kuona kila nyumba ya Mtanzania inawaka umeme na amepunguza gharama za kuunganisha umeme kutoka shilingi 380,000 hadi shilingi 27,000 ili kila mwananchi aweze kumudu gharama hizo. "

Chanzo: Azam TV

Sasa Mzukulu naanza Kuielewa ile Kauli isemayo kuwa Kunya Anye Kuku ila Akinya Bata tu basi Kaharisha. Siku zote Wanafiki huwa hawajifichi.

Kazi ipo mwaka huu.
 
Back
Top Bottom