Naona ingelikuwa ni bora kama na audio ingelifungwa, maake baada ya video kutoka imeonesha dhahiri hata mashairi yaliyoandaliwa yalikuwa na kejeli!
Baada ya Zuchu kutoka kanisani kumsifu bwana anamweleza diamond kuwa
*Eti Amina, dua zimeitikiwa,
Ashtuti, nije kukupa mali yako*
.
Neno "Eti Amina" linaonesha wazi kukejeri kiitikio hicho cha kikatoriki, badala ya kusema "Amina" kaonesha dharau kusema "Eti Amina"
Inaonesha wazi kuwa Zuchu alikuwa kanisani kumkejeli Mungu kwamba alienda kufanya sara ili abariki ngono wanayokwenda kufanya na Nassib! Kilichomaanishwa pale ni kuwa, Diamond kamruhusu Zuchu kwenda kanisani kumwomba Mungu abariki ngono! Ameonesha wazi sehemu pekee ya maombi yao ni Kanisani tena katoriki!
Kwamba, "Dua zimeitikiwa, Ashtuti! Nije kukupa mali yako"
Navyojua kanisa katoriki ni kanisa imara lenye uongozi imara kuanzia chini kwenda juu, nachojiuliza hiyo dili kafanya Diamond na waimba kwaya? Au na makatekista?
Kama na mapadre ama paroko walikuwepo, nahisi pesa zilizomwagika pale ni mamilioni! Hii inaonesha kuwa pesa yaweza fanya kila kitu hapa duniani!
Inasikitisha sana!