Kama hii tweet ni kweli basi Air Tanzania ni ya kuhurumiwa

Hizi ni changamoto za biashara japokuwa ni ngumu kutoa maamuzi kwa kutumia flight moja.Je ni kila siku hakuna wateja au ni siku hiyo tuu?Na jee ilivyokua inarudi Entebe Kilimanjaro, hali ilikua hivyo hivyo?

Niliwahi kushuhudia Egypt Air Airbus 320 from Cairo to DSM ikiwa na abiria 20.

So hizi ni changamoto na ninaamini wahusika wakiona route hailipi wataifuta au kupunguza idadi ya safari kama KQ walivyofanya route ya NBO to New York.
 
May ni low season.
Hata daladala wakati wa mchana zinakuwa hazina abiria kabisa. Au asubuhi wakati zinatoka city center.
Kama hujui biashara ya daladala ukiona daladala inatoka Kariakoo na abiria 2 inaelekea Tandika unaweza kusema Dar watu wamehama au wanatumia magari binafsi.
Ila yote yawezekana, shirika hili nasikia linajiendesha kwa hasara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…