Kama Gwajima Ndiye Mtetezi wa Haki, Basi Fisi Ni Mlinzi wa Kondoo

Kama Gwajima Ndiye Mtetezi wa Haki, Basi Fisi Ni Mlinzi wa Kondoo

Juma Wage

Senior Member
Joined
Sep 8, 2023
Posts
132
Reaction score
279
Katika dunia ya hoja na mantiki, ni kweli kwamba ujumbe ni muhimu kuliko mjumbe. Lakini je, kila mjumbe anastahili jukwaa? Mbona si kila njiwa huleta barua njema; wapo wanaoruka wakiwa wamebeba hadaa na uzushi.

Gwajima ni baba wa ahadi zilizoharibika kabla ya kuzaliwa. Aliwahadaa wananchi wa Kawe kwa ndoto za Birmingham, akawakatia tiketi za meli kutoka Japan ambazo hazikuwahi kutia nanga.

Leo hii anajivika joho la mtetezi wa haki za binadamu? Ni sawa na fisi kujitambulisha kama mchungaji wa kondoo.

Huyu ni yuleyule aliyewahi kudai anaweza kuwafufua Chifupa na Sokoine, kauli iliyovuka mpaka wa hekima na kuingia kwenye ukumbi wa miujiza ya kisiasa isiyo na staha.

Anapotamka sasa kuhusu utekaji na mauaji, haionekani kama sauti ya ujasiri, bali ni sauti ya mtu aliyekata tamaa ya kisiasa akililia jukwaa kwa maneno makali na maigizo.

Hoja yake inaweza kuwa na uzito, lakini ikitolewa na mtu aliyebobea katika uongo, maigizo na usanii wa mimbari, inageuka kuwa mzaha mchafu.

Kwa mtazamo wa wengi, si haki anayoitafuta bali ni umaarufu anaoutafuta kwa hila.
 
Tatizo wabongo wengi wanapenda kuangalia mtoa hoja kuliko hoja.

Gwajima kuna hoja kasema sawa na kuna hoja kakosea, pia kuna hoja zina maswali.

Sasa wabongo hawataki nuance, hawataki kuchambua hoja, wanataka all or nothing at all.

Kukataa hoja muhimu ya Gwajima kwa sababu alitoa ahadi ambazo hajatekeleza ni logical non sequitur fallacy.

Kama katoa ahadi ambazo hajatekeleza mkatae kwenye ubunge huko, lakini haina maana umpinge wakati anakemea utekaji.

Kwani ukikubali hoja fulani za Gwajima lazima ukubali hoja zake zote? Ukikataa hoja zake fulani lazima ukatae hoja zake zote?
 
Anayoyakemea Ni Muhimu Mno Kwa Mustakabali Wa Ustawi Wa Taifa Na Ustawi Wa Wananchi Wote Kiujumla,,Wananchi Wakitendewa Hayo Maovu Anayoyakemea Hata Hao Wa Kuwapeleka Brigihamu,,,Wa Kuwaletea Boti Za Uvuvi,,Wa Kuwajengea Miundombinu Kiujumla Watatoka Wapi???Gentleman...!!:Utu Na Kazi Ndio Tutasonga Mbele Na Wala Si Kazi Na Utu Hatuwezi Kusonga Mbele"###UTUKWANZA###
 
Unataka kusemaje bwana dereva? Wewe ni muajiriwa wa serikali au mwanasiasa? Uko upande wa kushangilia watu kutekwa na kuuwawa, familia yako ikimalizwa bado utabaki huo upande? Acha ubinafsi, Gwaji boy kakemea haijalishi historia yake.
 
Ni wewe tuliyekuwa tukikusubiri au tuendelee kusubiri? Maana kila anayeibuka anashindwa kujenga ushawishi ili aeleweke, zaidi ni kujichanganya tu.

Kama nakumbuka vizuri wakati akiasilisha hoja zake, alitanguliza Utanzania. Hakuwa mbunge, mnec au Askofu, hivyo tulitegemea ujibu hoja zake. Hayo makando mengine yanafahamika lakini, kwanini hamkuyasema wiki iliyopita?

Kwa hiyo, unataka kusema hakukuwa na hoja? Watu hawatekwi?. Mnajaribu kuleta propaganda za kizamani kuwalaghai watu kuwa hata Hitler alivutia maelfu lakini alikuwa muuaji, ili kufifisha hoja na muktadha tofauti na kilichokuwa kinaendelea wakati huo.

Kitu kimoja lazima muelewe, hamwezi kupingana na wakati.
 
Gwajima anaonekana kuwa na changamoto kubwa ya kutojizuia linapokuja suala la dini, jambo ambalo mara kwa mara limeibua hisia kuwa ana msimamo wenye upendeleo na chuki dhidi ya Uislamu. Wapo wanaoamini kuwa hata uhusiano wake baridi na Rais Samia unachochewa zaidi na mitazamo hiyo, kuliko tofauti za kisera au kiuongozi.
 
Gwajima hata angekua mzinzi kwa hili ataonekana shujaa hata kama hupendi.
Roho za watu sio jambo la mchezo. Juma Wage
 
Katika dunia ya hoja na mantiki, ni kweli kwamba ujumbe ni muhimu kuliko mjumbe. Lakini je, kila mjumbe anastahili jukwaa? Mbona si kila njiwa huleta barua njema; wapo wanaoruka wakiwa wamebeba hadaa na uzushi.

Gwajima ni baba wa ahadi zilizoharibika kabla ya kuzaliwa. Aliwahadaa wananchi wa Kawe kwa ndoto za Birmingham, akawakatia tiketi za meli kutoka Japan ambazo hazikuwahi kutia nanga.

Leo hii anajivika joho la mtetezi wa haki za binadamu? Ni sawa na fisi kujitambulisha kama mchungaji wa kondoo.

Huyu ni yuleyule aliyewahi kudai anaweza kuwafufua Chifupa na Sokoine, kauli iliyovuka mpaka wa hekima na kuingia kwenye ukumbi wa miujiza ya kisiasa isiyo na staha.

Anapotamka sasa kuhusu utekaji na mauaji, haionekani kama sauti ya ujasiri, bali ni sauti ya mtu aliyekata tamaa ya kisiasa akililia jukwaa kwa maneno makali na maigizo.

Hoja yake inaweza kuwa na uzito, lakini ikitolewa na mtu aliyebobea katika uongo, maigizo na usanii wa mimbari, inageuka kuwa mzaha mchafu.

Kwa mtazamo wa wengi, si haki anayoitafuta bali ni umaarufu anaoutafuta kwa hila.
Bure kabisa
 
Mbona mmesubiri awakosoe ndio mumpinge
Kumbe nyie mtu akiwalamba lamba mnamfuga
Wanafki wakubwa nyie
 
Back
Top Bottom