Mmmh! Uchafu na fungus ndio zinasababisha harufu ukeni
KUTOA HARUFU MBAYA UKENI.
Kila mwanamke amejaaliwa harufu ya kike inayo vutia na kuhamasisha wanaume kushiriki nae. Japo kuwa wapo wanawake ambao harufu hii hugeuka kero kwa watu wao wa karibu. Zipo sababu nyingi zinazo pelekea hali hii. Baadhi yake ni kama:
1. Kuwa na maambukizi ya magonjwa ya uke: magonjwa haya ni kama kansa ya uke( huu ni ugonjwa mbaya sana, mgonjwa hupata maumivu makali wakati wa kufanya, harufu mbaya sana hutoka, na uke una kuwa kama una waka moto), yeast infection( unakuwa unatoka maji ka maziwa ya mgando), bacterial infection( hii husababishwa na utumiaji wa vyoo usio salama, namna ambavyo unachamba kwani mwanamke yakupasa kuchamba kutoka mbele kwenda nyuma), sti/ std/ uti( haya ni magonjwa ya zinaa na ya njia ya mkojo)
2. Uchafu wa mwili na nguo za ndani: mwanamke yampasa kuwa msafi wa mwili na nguo za ndani. Yampasa mwanamke apende kujisafisha na kubadili nguo za ndani mara kwa mara. Vilevile yampasa aachane na chupi ambazo si za cotton kwani sio nzuri. Aepuke uvaaji wa chupi, taiti na suruali juu kwani anajiweka kwenye risk ya kupata kansa ya uke. Kuna tetesi kwamba taiti hukusanya mafuta ya mapajani na huamia tumboni, na ndio maana wanawake wengi wa siku hizi wana vitambi tofauti na mama zetu wazee wa underskirt.
3. Matumizi ya perfume, lotion, kuogea maji ya moto na vitu vingine ukeni: matumizi ya hivyo vitu huuwa good bacteria wa ukeni na kuziacha sehemu hizo wazi na rahisi kushambuliwa na magonjwa
4. Ngono isio salama: kwa wale wanao liwa kama samaki, wapo kwenye hatari ya kupata hali hii. Mchezo hatari sana na ule wa kutoa kitu kwenye tupu ya nyuma na kuipeleka kwenye tupu ya mbele
5. Kujisafisha kwa kujichokonoa: kujitia ujuzi wa kufanya hivi ni hatari sana. Usifanye kitendo hiki labda ushauriwe na daktari
Chakula: kupendelea kula vyakula vyenye yeast na sukari nyingi hupelekea shida hii kwa kuzalisha yeast mwilini. Vyakula hivi ni kama beer na mikate. Pendelea kula mtindi kwani wenyewe husaidia kuzalisha good bacterias
Kuogelea: kuogelea mara kwa mara si kuzuri kwa mwanamke. Kwani kwa kujiweka muda mrefu kwenye maji alafu ukashindwa kujikausha vizuri utapelekea upatwe na fungus wa uke na uanze kunuka
Pendelea kwenda hospitali pale unapoona haupo sawa. Hii itakusaidia kupata tiba sahihi