kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Viongozi walioteuliwa na Mwenyekiti wa CCM ni ishara kwamba hakuna kiongozi ndani ya chama hicho.
Nianze na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, kwa kipindi chote alichokaa Ruvuma hakuna jambo unaloweza kusema amefanya lakiubunifu na lenye tija kwa mkoa huu. Leo hii unamteua akapange mipango ya chama, means kwa uwezo wake anaenda kukaa ofisi Kama symbol tu huku dola ikiendelea kufanya shughuli za chama. Siamini Kama kwa uwezo alionao anaweza kwa namna yoyote ile kuja na strategy ya kukisaidia chama. Watuhumiwa tu alitamani kuwapiga ngumi,vipi walio kinyume na CCM ataelekeza wapigwe Nini?
Katibu mKuu (chaguo la Mzee Mangula) ambaye pia alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ana madoa mengi kiutawala. Kwanza huyu ameshiriki uchafuzi wa uchaguzi 2020. Amezungukwa na wapigaji akiwemo mwanamtandao (Diwani wa Makongo ) ambaye magazeti siku si nyingi yalidai amekamatwa kwa rushwa na akapigwa kesi ya uhujumu uchumi, siku si nyingi atafutiwa mashtaka. Lakini pia Mali alizonazo na taarifa zake ndani ya chama kwa awamu iliyopita zilitosha kuondolewa kwenye UDC kwa mpango uliokwisha kamilika ukisukwa na mtangulizi wake, kabla yakutiwa nguvuni likatokea tukio la 17/03 na hivyo mambo kuvurugika. Huyu ameshiriki na wakina Nape, Mwigulu na Kinana kudhulumu haki na chaguzi mbalimbali, wamebambikia watu kesi na Hadi Sasa wapo watu wamewekwa ndani kwa njama zake. Je, huyu ndiye mtu wakukabidhiwa chama? Kipi amefanya kipya chakuwekwa pale wakati huu ambao mapambano dhidi ya Rushwa nimakubwa au Ni zama za upigaji zimerejea?Kwamba huyu ndiye mshauri wa Mwenyekiti?
Katibu Mwenezi Wala haina haja yakumjadili kwa sababu tuhuma zake za Rushwa Morogoro zipo wazi na zilitamkwa adharani na Mhe. Rais aliyepita. Kwamba huyu tayari na tuhuma alizokuwa nazo ndiyo anakwenda kuendeleza mapambano dhidi ya Rushwa.?
Katika teuzi za aina hii unapata shida kujua kama kuna viongozi ndani ya CCM au kimebaki chama chakindugu ,kimtandao na kisasi? Kama chama kina viongozi wa aina hii na ni chama dola, serikali itapataje watu wenye ueledi? Kwanini kwa kauli moja tusikubaliane tu kwamba hakuna maendeleo yanayoweza kuletwa na watu wa aina hii?
Nianze na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, kwa kipindi chote alichokaa Ruvuma hakuna jambo unaloweza kusema amefanya lakiubunifu na lenye tija kwa mkoa huu. Leo hii unamteua akapange mipango ya chama, means kwa uwezo wake anaenda kukaa ofisi Kama symbol tu huku dola ikiendelea kufanya shughuli za chama. Siamini Kama kwa uwezo alionao anaweza kwa namna yoyote ile kuja na strategy ya kukisaidia chama. Watuhumiwa tu alitamani kuwapiga ngumi,vipi walio kinyume na CCM ataelekeza wapigwe Nini?
Katibu mKuu (chaguo la Mzee Mangula) ambaye pia alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ana madoa mengi kiutawala. Kwanza huyu ameshiriki uchafuzi wa uchaguzi 2020. Amezungukwa na wapigaji akiwemo mwanamtandao (Diwani wa Makongo ) ambaye magazeti siku si nyingi yalidai amekamatwa kwa rushwa na akapigwa kesi ya uhujumu uchumi, siku si nyingi atafutiwa mashtaka. Lakini pia Mali alizonazo na taarifa zake ndani ya chama kwa awamu iliyopita zilitosha kuondolewa kwenye UDC kwa mpango uliokwisha kamilika ukisukwa na mtangulizi wake, kabla yakutiwa nguvuni likatokea tukio la 17/03 na hivyo mambo kuvurugika. Huyu ameshiriki na wakina Nape, Mwigulu na Kinana kudhulumu haki na chaguzi mbalimbali, wamebambikia watu kesi na Hadi Sasa wapo watu wamewekwa ndani kwa njama zake. Je, huyu ndiye mtu wakukabidhiwa chama? Kipi amefanya kipya chakuwekwa pale wakati huu ambao mapambano dhidi ya Rushwa nimakubwa au Ni zama za upigaji zimerejea?Kwamba huyu ndiye mshauri wa Mwenyekiti?
Katibu Mwenezi Wala haina haja yakumjadili kwa sababu tuhuma zake za Rushwa Morogoro zipo wazi na zilitamkwa adharani na Mhe. Rais aliyepita. Kwamba huyu tayari na tuhuma alizokuwa nazo ndiyo anakwenda kuendeleza mapambano dhidi ya Rushwa.?
Katika teuzi za aina hii unapata shida kujua kama kuna viongozi ndani ya CCM au kimebaki chama chakindugu ,kimtandao na kisasi? Kama chama kina viongozi wa aina hii na ni chama dola, serikali itapataje watu wenye ueledi? Kwanini kwa kauli moja tusikubaliane tu kwamba hakuna maendeleo yanayoweza kuletwa na watu wa aina hii?