Kakobe ndio tiba ya umeme tz?

Kadogoo

JF-Expert Member
Feb 26, 2007
2,073
341
Hii Kauli ya Kakobe kuwa ili tatizo la Umeme liishe TZ ni lazima Waziri wa nishati aende kanisani kwa Kakobe kutubu na hakutakuwa na shida ya Umeme tena imekaaje?

Aidha Kakobe huyu kamshambulia Mchungaji mwenzake alieko loliondo kuwa atasababisha Kanisa lake libaki tupu kwa kuwa Watu wengi wanamfuata huko Loliondo kwa ajili ya tiba za maradhi mbalimbali!!!

Jamani huyu Kakobe amechanganyikiwa au nini? kwanini anamwonea wivu Mchungaji wa Loliondo kwa kutibu binaadamu? sasa tumwelewe vipi? hataki wagonjwa wapone kwa kutumia dawa? badala yake anataka wakakeshe Kanisani kwake ili awatibu kwa maombi tu?

gonga hapa usome yote: http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/9891-tiba-ya-loliondo-yamtisha-kakobe
 
unapotaka uishi vizuri hapa dunian ni lazima mtu uwe creative and innovative....kakobe being one of them ameona mambo kidogo yanataka kumuendea kombo sasa na ameona hot issue inayogusa jamii kwa upana wake ni mambo ya umeme na yale yanayoendelea kule loliondo then anajaribu kurusha karata ili labda yeye apate angalau chochote kitu na maisha yasonge,........
 
Alikataa umeme usipipite karibu na kanisa lakini vinginevyo atafanya maombi na umeme hautawaka, tangia mgao uanze hatukumbuki kama serikali ilimkosea Kakobe badala yake tunawasingizia mafisadi. Tafadhali Waziri Ngeleja nenda kaombe radhi; nani ajuaye miujiza ya huyu bwana labda mgawo uataisha?
 
Alikataa umeme usipipite karibu na kanisa lakini vinginevyo atafanya maombi na umeme hautawaka, tangia mgao uanze hatukumbuki kama serikali ilimkosea Kakobe badala yake tunawasingizia mafisadi. Tafadhali Waziri Ngeleja nenda kaombe radhi; nani ajuaye miujiza ya huyu bwana labda mgawo uataisha?
ACHA Kutapatapa na Kakobe wako wewe!!piga kazi!Kakobe ni msanii tu sasa naona anahangaika!wacha na mwenzie atese.
 
Hii Kauli ya Kakobe kuwa ili tatizo la Umeme liishe TZ ni lazima Waziri wa nishati aende kanisani kwa Kakobe kutubu na hakutakuwa na shida ya Umeme tena imekaaje?

Aidha Kakobe huyu kamshambulia Mchungaji mwenzake alieko loliondo kuwa atasababisha Kanisa lake libaki tupu kwa kuwa Watu wengi wanamfuata huko Loliondo kwa ajili ya tiba za maradhi mbalimbali!!!

Jamani huyu Kakobe amechanganyikiwa au nini? kwanini anamwonea wivu Mchungaji wa Loliondo kwa kutibu binaadamu? sasa tumwelewe vipi? hataki wagonjwa wapone kwa kutumia dawa? badala yake anataka wakakeshe Kanisani kwake ili awatibu kwa maombi tu?

gonga hapa usome yote: [URL="http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/9891-tiba-ya-loliondo-yamtisha-kakobe"]http://www.mwananchi.co.tz/habari/-/9891-tiba-ya-loliondo-yamtisha-kakobe[/URL]

zubeda thread yako inamashaka sana! badala ya kutoa ripoti, kinachoonekana utoa mawazo na mtizamo binafsi uliona juu ya Mchungaji Kakobe na inaonyesha una-negative thoughts juu yake sana! Umejitahidi kutumia manenoya kumuonyesha msomaji Mchungaji Kakobe ni mtu wa ajabu na anayoongea ni mambo ya ajabu ajabu pia. Ni maneno ya kutaka kushawishi jamii imuone Mchungaji Kakobe mtu ajabu ajabu ama hasiyefaa ktk jamii....I think this is not fair!
For your information wewe huwezi kujilinganisha na Kakobe ktk fulfillment ya wajibu kila mtu alionao hapa duniani!
 
Zubeda my dear,umewachokoza wafuasi wa kakobe,watakushambulia kama nyuki ohoo..! kakobe kiwango kimeshuka stafu game waache chipukizi babu
 
Zubeda katoa mawazo yake jamani sasa nyie mnachukia nini? Sasa wewe unayesema zubeda anataka kakobe aonekane mtu wa ajabu ajabu toa hoja zako jamvini hapa ili aonekane si wa ajabu sio unalaumu laumu ka Kikwete hapa.
 
zubeda thread yako inamashaka sana! badala ya kutoa ripoti, kinachoonekana utoa mawazo na mtizamo binafsi uliona juu ya Mchungaji Kakobe na inaonyesha una-negative thoughts juu yake sana! Umejitahidi kutumia manenoya kumuonyesha msomaji Mchungaji Kakobe ni mtu wa ajabu na anayoongea ni mambo ya ajabu ajabu pia. Ni maneno ya kutaka kushawishi jamii imuone Mchungaji Kakobe mtu ajabu ajabu ama hasiyefaa ktk jamii....I think this is not fair!
For your information wewe huwezi kujilinganisha na Kakobe ktk fulfillment ya wajibu kila mtu alionao hapa duniani!

Mashaka gani hayo? mimi nimechangia ktk kauli aliyoitoa Kakobe sasa kuna kosa gani? wewe kama unakubaliana na kauli yake si useme? nani kakuzuia? toa mchango wako kumtetea Kakobe na kauli zake tata! halafu wachangiaji watapima mbivu na mbichi!

lakini unajitokeza kutaka kumtetea Kakobe huku unaona aibu kumtetea kwa hoja wazi unabaki kunishambulia mimi ajabu!!!!!
 
zubeda thread yako inamashaka sana! badala ya kutoa ripoti, kinachoonekana utoa mawazo na mtizamo binafsi uliona juu ya Mchungaji Kakobe na inaonyesha una-negative thoughts juu yake sana! Umejitahidi kutumia manenoya kumuonyesha msomaji Mchungaji Kakobe ni mtu wa ajabu na anayoongea ni mambo ya ajabu ajabu pia. Ni maneno ya kutaka kushawishi jamii imuone Mchungaji Kakobe mtu ajabu ajabu ama hasiyefaa ktk jamii....I think this is not fair!
For your information wewe huwezi kujilinganisha na Kakobe ktk fulfillment ya wajibu kila mtu alionao hapa duniani!

Uwe na utamaduni wa kufikiri kabla ya kujibu, pamoja na mawzo yake lakini Zubeda ametoa link kuonesha source ya information yake, sasa unachomshambulia ni nini! by the way ni kweli kakobe amekasirika juu ya uponyaji wa mchungaji wa Loliondo sababu " mapato" ya jumapili hayakuwa mazuri
 
Huyo Jamaa wa loliondo achukue sensa ya wagonjwa wa Ukimwi huko tunaihitaji kwa ajili ya tafiti maana watu walikuwa hawajitokezi kupima na kutangaza matokeo yao, hata Kikwete alitudanganya Dodoma kwenye Uzinduzi wa kampeni za kupima Ukimwi.

Wasiwasi wangu ni kama huyu mzee ni Mganga wa EL kwa ajili ya Uchaguzi 2015; tutakuwa tumeliwa maana wote waliokunywa hayo maji hadi kikwete watakuwa wapiga debe wa EL, au Loliondo siyo U-masaaini?!!
 
Kakobe anachezea imani za watu tu hana lolote! wala hakuna uhusiano kati ya mgao wa umeme na mambo ya kakobe! kwani migao mingapi imetokea hapo siku za nyuma mbona hakuwai kujitokeza! hata hivyo kama yeye ndo anashikilia umeme wetu basi hafai kabisa...afanyiziwe tu! Issue ya Loliondo lazime imguse, kwani mwenzake anapokea TZS 500 tu! yeye amekuwa akipokonya Dhahabu, magari, fedha nyingi, na vingi vya thamani kutoka kwa victims wake...hamjaona tu kuwa kuna mgongano wa kimaslahi! "USINIULIZE KAMA NINA UHAKIKA KWA HAYA TAFADHALI" Wafuasi wake watajibu:rain:
 
Huyo Jamaa wa loliondo achukue sensa ya wagonjwa wa Ukimwi huko tunahiitaji kwa ajili ya tafiti maana watu walikuwa hawajitokezi kupima na kutangaza matokeo yao, hata Kikwete alitudanganya Dodoma kwenye Uzinduzi wa kampeni za kupima Ukimwi.

Wasiwasi wangu ni kama huyu mzee ni Mganga wa EL kwa ajili ya Uchaguzi 2015; tutakuwa tumeliwa maana wote waliokunywa hayo maji hadi kikwete watakuwa wapiga debe wa EL, au Loliondo siyo U-masaaini?!!

Ahahahahahahahahahhahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, mkuu una mawazo kweli loh!!!!!!!!!yaani mbavu sina mwana loh!!!
 
Zubeda katoa mawazo yake jamani sasa nyie mnachukia nini? Sasa wewe unayesema zubeda anataka kakobe aonekane mtu wa ajabu ajabu toa hoja zako jamvini hapa ili aonekane si wa ajabu sio unalaumu laumu ka Kikwete hapa.
source ni Kakobe .soma link aliyoweka hapo juu. Tatizo hatusomi vizuri tunakurupuka tu.
 
Uwe na utamaduni wa kufikiri kabla ya kujibu, pamoja na mawzo yake lakini Zubeda ametoa link kuonesha source ya information yake, sasa unachomshambulia ni nini! by the way ni kweli kakobe amekasirika juu ya uponyaji wa mchungaji wa Loliondo sababu " mapato" ya jumapili hayakuwa mazuri

Ninataka wewe "kilemba" na wengine kujua: kama Mchungaji Kakobe ama mtu yeyeto kaongea jambo, basi at first tueleze amesema nini! Ni makosa na infact ni poor and misleading communication unapoaanza kutoa maelezo kwa kueleza mawazo yako na mtizamo wako. Kwa mtu makini anataka ueleze kwanza ulivyosikia/kilichoongelewa then after unaweza anza kutoa mawazo yako na mtizamo wako.
Sasa ukiangalia zubeda na huyo Mussa Juma wake hakuna anayetuelezi Mchungaji Kakobe alisema nini kuhusiana na hiyo tiba ya lolihondo! Mfano maelezo toka kwa uzitadhi Mussa Juma yanaaza" WAKATI idadi kubwa ya wagonjwa wakionekana kumzidi nguvu mchungaji mstaafu, Ambilikile Mwasapile, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe ameingia hofu ya kupoteza waamini kufuatia taarifa kwamba mchungaji huyo anatibu Ukimwi" Uadishi wa namna hii si kwa watu makini labda kama wewe naripot kwenye magazeti au mambo ya udaku!
 
Mashaka gani hayo? mimi nimechangia ktk kauli aliyoitoa Kakobe sasa kuna kosa gani? wewe kama unakubaliana na kauli yake si useme? nani kakuzuia? toa mchango wako kumtetea Kakobe na kauli zake tata! halafu wachangiaji watapima mbivu na mbichi!

lakini unajitokeza kutaka kumtetea Kakobe huku unaona aibu kumtetea kwa hoja wazi unabaki kunishambulia mimi ajabu!!!!!

Mawazo yako ni sawa na yangu ila kuna wengine yatawakwaza kwa kuwa wana interest na kakobe kwahiyo uwe mvumilivu na mjadala uachwe wazi...............
 
hyo link umeipitia vizuri lakini??? umesoma hadi mwisho au ndo alimradi ubshane tu
Ninataka wewe "kilemba" na wengine kujua: kama Mchungaji Kakobe ama mtu yeyeto kaongea jambo, basi at first tueleze amesema nini! Ni makosa na infact ni poor and misleading communication unapoaanza kutoa maelezo kwa kueleza mawazo yako na mtizamo wako. Kwa mtu makini anataka ueleze kwanza ulivyosikia/kilichoongelewa then after unaweza anza kutoa mawazo yako na mtizamo wako.
Sasa ukiangalia zubeda na huyo Mussa Juma wake hakuna anayetuelezi Mchungaji Kakobe alisema nini kuhusiana na hiyo tiba ya lolihondo! Mfano maelezo toka kwa uzitadhi Mussa Juma yanaaza" WAKATI idadi kubwa ya wagonjwa wakionekana kumzidi nguvu mchungaji mstaafu, Ambilikile Mwasapile, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe ameingia hofu ya kupoteza waamini kufuatia taarifa kwamba mchungaji huyo anatibu Ukimwi" Uadishi wa namna hii si kwa watu makini labda kama wewe naripot kwenye magazeti au mambo ya udaku!
 
Ameona umaarufu wake utashuka dhidi ya mchungaji mstaafu wa Loliondo.
Pole sana Kakobe
 
Back
Top Bottom