Kakobe alitumwa?

Kakobe alitumwa?

Mkatubu kwa mauaji holela mnayofanya, uonevu, kukojolea katiba, ubaguzi n.k. MKATUBU
 
KAKOBE ALITUMWA? MBONA WAPINZANI WAMEFANYA MASHAMBULIZI YAKE DHIDI YA RAIS MAGUFULI KUWA AGENDA ZAO? WAMEKOSA AGENDA ZA KUJISHINDANISHA NA SERIKALI YA CCM KWA WANANCHI?

Tangu Kiongozi wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship(FGBF), Zacharia Kakobe atumie Madhabahu kumshambulia rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. John Pombe Magufuli, Wanasiasa wa Upinzaji wamedandia shutuma za Kakobe na kuzifanya agenda zao kuendeleza kwa kasi ya ajabu porojo za kutaka kuwafanya viziwi na vipofu Watanzania waache kuona na kusikia juhudi za Serikali chini ya Rais Mahiri kabisa, JPM za kuijenga Tanzania mpya na badala yake waamini uzushi, porojo na vimaneno maneno vya hovyo hovyo kwamba rais akatubu, sijui rais hakosolewi na upuuzi mwingi tu.

Kwa jicho la tatu unaweza kuamini kuwa yale hayakuwa maneno ya KAKOBE bali alilipwa na kutumwa kufanyakazi ya wanasiasa ambao kupitia kwa viongozi wa dini aina ya Kakobe wanaweza kupambana na serikali ambayo kimsingi imeonesha kuzikonga nyoyo za wananchi wake kutokana na uchapakazi wake uliotukuka.

Hivi Unawezaje kutofautisha maneno ya Kakobe na porojo za wanasiasa kwamba kuna utawala wa kidikteta, kuminya demokrasia, kutokubali kukosolewa? Hivi hayo madhaifu ya Serikali yanaonekana machoni mwa wana siasa na akina Kakobe? Wanachi wa kawaida ambao kiu yao ya siku nyingi ya kutaka kuona watoto wao wanasoma bure, madawa yanapatikwpana mahospitalini, madini yao, gesi yao, Mafuta yao hayaibiwi na wajanja, Barabara za juu na chini zinajengwa, Reli ya kisasa inajengwa, bei nzuri ya mazao, urasimu katika kupatikana kwa pembejeo na mbolea unatokomezwa, wanafunzi wanapata mikopo kwa wakati , wao hawana macho?

Najiuliza tu:

Kwanini upinzani unajipa kilema cha kujimaliza kwa hoja na mbinu nyepesi nyepesi sana kiasi hiki kupambana na Serikali mahiri kama hii ya awamu ya tano? Uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu wa 2020 upinzani utachomoka kweli kwa hoja za akina Kakobe kweli? Eti serikali haikosoleki, kweli? Mwananchi apigie kura upinzani kwa sababu hiyo tu? Sawa haikosoleki lakini tuna maji, tunapata mbolea kwa bei nafuu na kwa wakati, watoto wetu wanasoma bure na wale wa vyuo vikuu wanapata mikopo kwa wakati, madawa yako hospitalini n.k. Hivi wananchi wakiwapa hizo kama sababu za kumchagua tena JPM mtakuwa na la kuwashawishi tena?

Wapinzani mnapoteza muda kukwapua mashambulizi ya akina kakobe na kuyafanya agenda zenu , mtaumbuka, muwe wabunifu wa hoja nzito za kwenda nazo kwa wananchi siyo hizi za kuwanunua nunua wenye njaa kama akina Kakobe na kuanza kuzikomalia.

Mnachekesha sana. Hivi mnategemea Mshinde uchaguzi kupitia waumini wa Kakobe ambao hata kanisa lake pale Mwenge pamoja na kuwa dogo lililojibananisha pale njiani halijai? BAVICHA mmoja akasema CCM msimpuuze Kakobe ana waumini wapiga kura mil.10. Ujinga mtupu. Watanzania hatujafikia mil.50. Watoto ambao hawajafikia umri wa kupiga kura ndiyo wengi, wanaojiandikisha kupiga kura ni wengi lakini wanaojitokeza kupiga kura hata mil.10 hawafiki. Ina maana wote wanaokwenda kupiga kura wote wanatoka kwa Kakobe? Hizi ni akili za Makarai ya Zege kwelikweli.

Waumini wa Kakobe wenyewe ni kama watu waliokata tamaa ya maisha sijadhani kama wanakuwa na hata wazo la kupiga kura. Ni wale wanaokwenda kuvuliwa mikufu ya dhahabu na Kakobe na kuiuza kwa ajili ya kujipatia fedha huku akiwahadaa kwamba vitu hivyo vya thamani ni chukizo kwa Mungu, hawa watapata muda wa kupiga kura? Ni wale ambao wanaabudu kwa kusikiliza ujumbe wa Mungu wao (KAKOBE) redioni maana akisafiri hakuna ruhusa ya mtu mwingine kuendesha ibada. Hawa wanapiga kura kweli?

Wapinzani jitafakarini sana, waaseni vijana wenu mitandaoni wabuni mbinu mpya za kupambana na serikali ili kupitia kwao siku moja mshike dola. Hamuezi kushika dola kwa Hoja za akina Kakobe.
Nahisi Huu Upumbavu ulio andika ni upumbavu wa mwaka kuwai kuandikwa
 
Mzee kweli kitubio kinamuhusu. Kwa kweli Kakobe kapanikisha watu, naona hata kauli za niombeeni makanisani na miskitini zitapungua sasa!!.

Kama hii track ya kutuba itaendelea mpaka jtatu, lazima mzee wa kutubu anadamkia bandari kwenda kukamata makontena ya magari. ili kuanzisha new kiki.

Ila KUTUBU MUHIMU.
kushtukiza, hivi ile episode ya yule soldier fake wa Lugalo iliishia wapi?
 
Nenda katubu kwamza
Mbonu hii si nyepesi kama uichukuliavyo....huu ni mkono wa Mungu mwenyewe ameshuku kutujibia nakutetea...ninyi niviziwi msiyesikia sasa lazma mtubu....tofauti na hapo Ni Gharika.
 
Pengo ndo alitumw na ccm kwa sababu kaongea km katibu mwenezi wa ccm anayeeneza uchafu lkn BABA ASKOFU KAKOBE kasema ukweli ambao ccm hawataki maana bak yao madarakani ni vyombo vya dola na uvunjifu wa katiba na sheria za nchi
 
20171229_211542.png



20171229_211610.png

A picture speaks a thousand words.
 
Kakobe wala hajaanza leo kuropoka ovyo dhidi ya serikali na mamlaka, hasa baada ya kanisa lake kuingia katika migogoro. Anadhani kuingia siasani kutanusuru jina lake katika dini. Anazidi kupotea na mwisho wake hautakuwa mzuri. Mtaniambia
Tukwambie nini sasa??? Badala useme uliyopanga kumfanyia unakuja na manenoooo
 
Dawa imeingia naona mnahangaika mnashindwa kupinga hoja kwa hoja
 
Mleta uzi ama hujui ulikuwa unaandika nini au basi kuna unachokiwinda kupitia kutubu alikoelekeza Kakobe!
Nchi kuwa huru miaka 50+ maana yake nini? Ni kuwa zile goals walizoset wakati wa kupata uhuru walishazifikia na kuzivuka! Haina maana kuwa miaka ya leo bado tunajadili ukosefu wa dawa, maji, madarasa, barabara na viwanda kwani miaka 25 ilitosha tuwe tunavyo vyote hivi!
Na kwa miaka hii tulitakiwa tuwe tunajadili habari za teknolojia mpya ili tushindane na Korea kaskazini na china!
Kusema kuwa wananchi wanavihitaji hivyo vitu vya kizamani ni kwa kuwa hamkutimiza wajibu wenu kama chamadola kuhakikisha ilani na sera zenu zinatekelezwa sawasawa! Kusema kuwa mnatekeleza hili na lile la miaka 25 nyuma ni kuwadharau wananchi na kuwafanya kama wasioweza kuwaza na kuhoji juu ya kiwango duni cha upatikanaji wa husuma za jamii ilihali wao wanawalipa kodi na bado mnakwenda kukopa na walipaji ni wao lakini huduma hizo zimekuwa kama huruma au zawadi badala ya haki yao!
Msiwafunge mnyororo wa wakati wa ukoloni kuwa ili huduma za jamii zipatikane eneo fulani ni lazima mkoloni awepo eneo hilo! Hii si haki kutumia upatikanaji wa huduma za jamii ili mpate kura zao.
Wapeni wananchi haki yao kwani kodi wanawalipa na hawana haja ya kuwasifu kwa kuwapa haki yao.
 
Ndio ,katumwa na roho mtakatifu. Nikama ilivokuwa kwa Musa na wana wa Israel.
 
Mtoa mada kwanza inabidi uwaombe radhi Wandamba. Unajiita na kujitambulisha kutumia jina la watu makini na watu wanaotafakari kila neno walisemalo. Nawafahamu Wandamba hawawezi kuwa na mawazo kama hayo. Nadhani wewe ni msakatonge na mchumia tumbo kamwe huwezi kubeba jina hilo tukufu la Wandamba. Tafadhali waombe radhi Wandamba. Kama unatafuta U DC basi tumia kanzu nyingine siyo Wandamba ninaowajua Mimi. Aibu yako hiyo.
 
Watu ni wepesi kusaahau
Lowassa amewahi kusema "Ni zamu ya walutheri kutoa Rais." Ukiangalia wengi wanaomlaumu Rais ni waprotestant, na kama ukisikiliza moja ya hotuba ya Kakobe utasikia anasema "Catholic na Anglican." ni imani ya uongo

Je Serikali inawapendelea Wassuni na Wakatoriki??
 
Back
Top Bottom