Kaka yangu ameota nimeoa...

Kaka yangu ameota nimeoa...

Wakuu habar za leo.

Kwenye Dunia hii kuna watu ndoto zao huwa za kweli. Anacho ota kinatokea really.

Nina bro wangu yupo kigamboni jana nilienda site kuweka bikoni nikawa nae.

Katika stori za hapa na pale akaniambia dogo nimeota umeowa na ukampa mkeo gari ndogo (sijui aina gani). Usipokuwa makini familia yake itakuteka uishi kwao maana nimeota BABA MKWEO ANAKUBEMBELEZA UKASIMAMIE BIASHARA ZAKE NDOGONDOGO.

Nikamwambia bro hata mchumba sina hayo mambo nimepumzika kwanza. Akacheka na kusema mapenzi yanapumzishwaga?!!? Nikamwambia yeah, nataka nimalize project zangu kwanza then ntaangalia mambo mengine.

NDOTO ALIZOWAHI KUOTA NA ZIKATOKEA NA KUNISIMULIA NI HIZI.

1. Aliwahi kuota polisi wanakuja kijijini kwetu kumkamata jambazi mmoja, asubuhi yake kweli polisi ikaja na jambazi akakamatwa ilikuwa mwaka 2002.

2. Aliota wanawake wawili wamekufa maji ya mtoni (seasonal river) kesho kutwa yake kuna madada mapacha walikuwa wanavuka mto wakapelekwa na kufa tukawaokota mbali na kuzika mwaka 2005.

3. Aliota jamaa mmoja amefilisika pale kijijini, baada miezi kadhaa yule bwana wakamdhulumu msukuma ng'ombe kilichofuata mali iliteketea mpaka jamaa akauza nyumba mwaka 2007.

4. Aliota vurugu kubwa limetokea kwenye sherehe...siku ya nane nane kulikuwa na mechi kijijini pakatokea fujo kuna mchezaji 1 akapigwa akafa.

5. Aliota mwaka flani njaa itaibuka maeneo yetu...mwaka uliofuata watu walikula ugali wa mtama mwekundu njaa ya hatari.

6. Aliota nimepata kazi sehemu ya mbali...akaniambia mwaka uliofuata nikapata kazi hapa dar... (nakumbuka nilimpa zawadi huyu bro)

NB; ndoto nyingi hapendi kusimulia kwa sababu zingine sio nzuri na pengine hisema jambo likishatokea...

(Wakuu hii ni kweli kabisa)

Nawaza hapa huyo nitakae muowa daaah...ina maana inaweza kuwa sitakuwa na choice tena?!
Niache nature ifanye kazi yake?!

Natamani ndoto ya bro ifeli kwa mara ya kwanza aisee.

Ingekuwa wewe ungefanyaje!!??

[Picha ni jana tukiwa site]View attachment 1165162
Oa mkubwa huo ni ujumbe amekufikishia kijanja
 
Unatakiwa uoe,umechelewa sana;pia kaka yako anakipaji ingawa ameshindwa kukitumia vizuri ili awe tajiri-aanzishe sehemu yake ya kuabudu na ajiite nabii...
 
Broo wako mtumie vizuri,

Hao wanaotabiri alafu inakuwa kweli basi huyo broo yuko karibu na Nguvu ambazo hatuzijui,
Kabisa mkuu. Kwa namna hiyo huyo ni mtu makini sana. Watu wa hivyo hata yeye mwenyewe huwa hawafanyi makosa ya kijinga,ksbb anajijua. Huyo hata kujenga ningejenga karibu nae. Kila siku lazima nionane nae. Namweka sawa chochote anachoota kuhusu mimi awe ananishirikisha hata kama ni kibaya ili nijue nijipange vipi
 
Sasa huwezi kumwambia niote...hiyo inamtokea tubhata yeye hana control nayo.
Kumtumia vizuri hamaanishi umwambie akuote No,ila uwe karibu nae tu kwa simu kila siku. Kuna kumwambia kila atakaloota kuhusu wewe akuahirikishe hata kama ni baya,ili ujue ujipange vipi. Halafu kumtumia vizuri kwa kuyatumia kwa usahihi yale aliyokuotea
 
Back
Top Bottom