Asabaya
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 1,310
- 418
Hali zenu wana MMU?
Kuna jambo nashindwa kulielewa, mdogo wangu aliolewa na jamaa ambae hata kazi alikua hana tukamsaidia kumpa mtaji mpaka mambo yake yakawa sawa, alipopata vijisenti akamjeuri kupita kiasi, na muchepuko ndio usiseme.
Yote haikutukera, akapata mwanamke ndio jeuri ikazidi, ikafikia mpaka anampiga mdogo wetu. Kwakweli hapo ustahmilivu ulinishinda, nikakwambia mdogo wangu huyu jamaa ni limbukeni na atakutoa roho bora ufanye maarifa uondoke.
Kabla hata hajajipanga kuondoka jamaa alikuja na mwanamke ndani ya nyumba alopewa zawadi mdogo wetu na Dad siku ya harusi, yule jamaa bila kujali alimfukuza mdogo wetu na kumwambia mie nakupa talaka na sitokurudia wewe labda nilale na mamangu.
Basi mdogo wetu amerudi nyumbani tukamuondoa kwenda Arabuni mwenyezi mungu kamjalia amepata mume anaolewa soon inshallah, huyu bwana sasa fimbo ya mungu imempiga huyo mwanamke alomchukua ni wale wanawake wa type za wadada wa kutunzana; sijui leo kuna kigodoro wapi wanakwenda, mara sare imepita, kwa ufupi jamaa hanaa amerudi kuliko alivyokua mwanzo, na mwanamke kamfukuza.
Cha kushangaza bila aibu jana amekuja nyumbani na kilio tulijua amefiwa kwao, tunashuka chini haya alichojia nini, ooh nimekuja kumrudia mke wangu, mimi ilikua sio akili yangu nilirogwa.
Hivi waungwana, kwa makosa aloyafanya huyu bwana anawezaje kuja kusema nataka kumrejea mke wangu? Wenye ujuzi na mambo kama haya ebu watuambie kama mliwahi kupitia wasohaya kama hawa.
Kuna jambo nashindwa kulielewa, mdogo wangu aliolewa na jamaa ambae hata kazi alikua hana tukamsaidia kumpa mtaji mpaka mambo yake yakawa sawa, alipopata vijisenti akamjeuri kupita kiasi, na muchepuko ndio usiseme.
Yote haikutukera, akapata mwanamke ndio jeuri ikazidi, ikafikia mpaka anampiga mdogo wetu. Kwakweli hapo ustahmilivu ulinishinda, nikakwambia mdogo wangu huyu jamaa ni limbukeni na atakutoa roho bora ufanye maarifa uondoke.
Kabla hata hajajipanga kuondoka jamaa alikuja na mwanamke ndani ya nyumba alopewa zawadi mdogo wetu na Dad siku ya harusi, yule jamaa bila kujali alimfukuza mdogo wetu na kumwambia mie nakupa talaka na sitokurudia wewe labda nilale na mamangu.
Basi mdogo wetu amerudi nyumbani tukamuondoa kwenda Arabuni mwenyezi mungu kamjalia amepata mume anaolewa soon inshallah, huyu bwana sasa fimbo ya mungu imempiga huyo mwanamke alomchukua ni wale wanawake wa type za wadada wa kutunzana; sijui leo kuna kigodoro wapi wanakwenda, mara sare imepita, kwa ufupi jamaa hanaa amerudi kuliko alivyokua mwanzo, na mwanamke kamfukuza.
Cha kushangaza bila aibu jana amekuja nyumbani na kilio tulijua amefiwa kwao, tunashuka chini haya alichojia nini, ooh nimekuja kumrudia mke wangu, mimi ilikua sio akili yangu nilirogwa.
Hivi waungwana, kwa makosa aloyafanya huyu bwana anawezaje kuja kusema nataka kumrejea mke wangu? Wenye ujuzi na mambo kama haya ebu watuambie kama mliwahi kupitia wasohaya kama hawa.