Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Kahama yaangamia kwa Ukimwi
Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 22nd April 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0
ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20 hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.
Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kahama, Morgan Mwita katika taarifa ya hali ya Ukimwi katika Wilaya ya Kahama mbele ya wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo wakiwemo watendaji wa kata na viongozi wa dini.
Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.
Alisema wakati wilaya hiyo ina wakazi 815,175, wakazi 85,342 walijitokeza kupima Ukimwi hadi kufikia Desemba mwaka 2010, na 7,913 waligundulika wameambukizwa virusi vya Ukimwi.
Mwita alisema kutoka na maambukizi ya ugonjwa huo kuwa makubwa, changamoto wanayoipata wao kama Wilaya ya Kahama ni pamoja na kuendelea kuelimisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa na ubaguzi kwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi.
Alisema changamoto nyingine ni pamoja na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hasa katika maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajapa elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo hatari.
Hata hivyo ofisa huyo aliyataka mashirika mbalimbali kuongeza jitihada za kutafuta fedha za kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu na hatarishi hasa katika upande wa lishe, elimu, ujasiriamali na afya.
Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 22nd April 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0
ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20 hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.
Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kahama, Morgan Mwita katika taarifa ya hali ya Ukimwi katika Wilaya ya Kahama mbele ya wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo wakiwemo watendaji wa kata na viongozi wa dini.
Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.
Alisema wakati wilaya hiyo ina wakazi 815,175, wakazi 85,342 walijitokeza kupima Ukimwi hadi kufikia Desemba mwaka 2010, na 7,913 waligundulika wameambukizwa virusi vya Ukimwi.
Mwita alisema kutoka na maambukizi ya ugonjwa huo kuwa makubwa, changamoto wanayoipata wao kama Wilaya ya Kahama ni pamoja na kuendelea kuelimisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa na ubaguzi kwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi.
Alisema changamoto nyingine ni pamoja na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hasa katika maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajapa elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo hatari.
Hata hivyo ofisa huyo aliyataka mashirika mbalimbali kuongeza jitihada za kutafuta fedha za kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu na hatarishi hasa katika upande wa lishe, elimu, ujasiriamali na afya.