Kahama yaangamia kwa Ukimwi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Kahama yaangamia kwa Ukimwi

Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 22nd April 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0








ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20 hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.

Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kahama, Morgan Mwita katika taarifa ya hali ya Ukimwi katika Wilaya ya Kahama mbele ya wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo wakiwemo watendaji wa kata na viongozi wa dini.

Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.

Alisema wakati wilaya hiyo ina wakazi 815,175, wakazi 85,342 walijitokeza kupima Ukimwi hadi kufikia Desemba mwaka 2010, na 7,913 waligundulika wameambukizwa virusi vya Ukimwi.

Mwita alisema kutoka na maambukizi ya ugonjwa huo kuwa makubwa, changamoto wanayoipata wao kama Wilaya ya Kahama ni pamoja na kuendelea kuelimisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa na ubaguzi kwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi.

Alisema changamoto nyingine ni pamoja na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hasa katika maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajapa elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo hatari.

Hata hivyo ofisa huyo aliyataka mashirika mbalimbali kuongeza jitihada za kutafuta fedha za kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu na hatarishi hasa katika upande wa lishe, elimu, ujasiriamali na afya.
 
Hizi takwimu zinatia shaka...........................kama maambukizi ni 9.3% inakuwaje walioambukizwa wafikie asilimia 70?

Kuna mapungufu makubwa ya uchambuaji wa habari hapa..........................
PHP:
 ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20  hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga  wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.

Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.
 
Kahama yaangamia kwa Ukimwi

Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 22nd April 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0

ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20 hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.

Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kahama, Morgan Mwita katika taarifa ya hali ya Ukimwi katika Wilaya ya Kahama mbele ya wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo wakiwemo watendaji wa kata na viongozi wa dini.

Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.

Alisema wakati wilaya hiyo ina wakazi 815,175, wakazi 85,342 walijitokeza kupima Ukimwi hadi kufikia Desemba mwaka 2010, na 7,913 waligundulika wameambukizwa virusi vya Ukimwi.

Mwita alisema kutoka na maambukizi ya ugonjwa huo kuwa makubwa, changamoto wanayoipata wao kama Wilaya ya Kahama ni pamoja na kuendelea kuelimisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa na ubaguzi kwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi.

Alisema changamoto nyingine ni pamoja na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hasa katika maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajapa elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo hatari.

Hata hivyo ofisa huyo aliyataka mashirika mbalimbali kuongeza jitihada za kutafuta fedha za kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu na hatarishi hasa katika upande wa lishe, elimu, ujasiriamali na afya.


Mkuu, japo % ipo juu, lakini siyo mbaya kama sehemu nyingine. Hebu rejea hii:

Why this age group: 35-39? Pesa? Ushawishi? Ni nini hasa?
.
.
.

Prime Minister Mizengo Pinda released the results from a recent survey carried out by National Bureau of Statistics with assistance from USAID. The survey interviewed and took blood samples from more than 9,000 women aged 15-49 and close to 7,000 men aged 15-49 in all 26 regions of Tanzania. The results indicated a 4.7% HIV prevalence rate among men and a 6.8% rate among women. This is a slight improvement over the 2003-04 survey which found rates of 6.3% and 7.7% respectively.

Iringa recorded the highest rate of 14.7% (previously 13.4%) followed by Dar es Salaam at 8.9% (previously 10.9%), Mbeya at 7.9% (previously 13.5%) and Shinyanga at 7.6% (previously 6.5%). Zanzibar had the lowest prevalence rate at 0.6%. Age-wise, the highest prevalence was among the 35-39 age group (10%).

The survey also collected information on knowledge of HIV, attitudes and behavourial aspects. Over 98% of respondants had heard about HIV/AIDS. 68.6% of women and 76.3% of men knew that condoms can reduce the risk of contracting HIV, while 82% and 86.6% knew that limiting sex to one uninfected partner who has no other partners would reduce the risk. 85% and 89% where aware that abstaining from sexual intercourse is another recognized prevention method.

Source: Tanzanian Affairs » AIDS/HIV & MALARIA STATISTICS
 
mwandishi hakusoma statistics hata kidogo...hakuna hesabu za hivo
 
Hiyo asilimia 70 imetoka wapi? Waliopima 9% positive na hiyo yenyewe hauwezi kuiaply kwa jamii nzima.
 
Hiyo ndio Elimu yetu ya Shule za Kata.Hapo mwandishi hastahili kulaumiwa,kwani huo ndio uelewa wake kwa kuwa ndivyo alivyofundishwa hivyo kuhusu TAKWIMU.Wakulaumiwa hapa ni SERIKALI Kuanzia Shule nyingi za kata bila kujali ubora wa Elimu inayopatikana kwenye shule hizo za KATA.Matokeo yake ndio haya mnayoyaona kwenye "JF".All in all ndugu zangu na hasa vijana.Tuepuke ngono ambazo si salama.Tutumie Kondomu Jamani,sisi ndio nguvu kazi ya TAIFA...
 
Mji wa Kahama ni kambi kubwa ya madereva wa magari makubwa wenye masafa marefu. Uchunguzi wangu unaonyesha mikoa ya Shinyanga na Tabora imeadhiriwa zaidi katika miji ya Kahama na Nzega. Nyumba za wageni zimejaa madereva wa magari makubwa yaendayo pande za Rwanda na Burundi.

Iringa nako hali kama hiyo kwani madereva baada ya kulazimisha malori kupanda mlima Kitonga wanajipumzisha Iringa, na wengine kabla ya kujiandaa kuteremsha mlima Kitonga wanajipumzisha Iringa kwanza.

Waambukizaji wakubwa ni madereva na dada zetu victims wanaotafuta cho chote toka kwa madereva kujikimu kimaisha. Na hawa dada zetu wanawaume au marafiki wengine wanakopandikiza walivyovuna kwa madereva.

Jamani Ukimwi unakwepeka kwa wanaojiamini na kuamua kuaminiana baada ya kujihakikishia usalama wao
 
kuna kampuni ya wiliamson ilitoa magari takribani 30, kuwapeleka wafanya kazi wake kwa babu hii ni ishara tosha kuwa hari huko si shwari...
 
mji wa kahama ni kambi kubwa ya madereva wa magari makubwa wenye masafa marefu. Uchunguzi wangu unaonyesha mikoa ya shinyanga na tabora imeadhiriwa zaidi katika miji ya kahama na nzega. Nyumba za wageni zimejaa madereva wa magari makubwa yaendayo pande za rwanda na burundi.

Iringa nako hali kama hiyo kwani madereva baada ya kulazimisha malori kupanda mlima kitonga wanajipumzisha iringa, na wengine kabla ya kujiandaa kuteremsha mlima kitonga wanajipumzisha iringa kwanza.

waambukizaji wakubwa ni madereva na dada zetu victims wanaotafuta cho chote toka kwa madereva kujikimu kimaisha. Na hawa dada zetu wanawaume au marafiki wengine wanakopandikiza walivyovuna kwa madereva.

jamani ukimwi unakwepeka kwa wanaojiamini na kuamua kuaminiana baada ya kujihakikishia usalama wao
tatizo siyo madereva tu....hakuna sehemu ambao nilisha wahi kufika ambako ngono inafanyika hovyo hovyo kama mbuguni, utakuta vitoto vya darasa la tano vina mimba hapoa kuna maderva gani...
 
Kumpata dada ambaye bikra siku hizi ni chanda cha dhahabu, hali kadhalika kumpata kaka asiyekuwa na uzoefu wa mahusiano ya mapenzi ni imebaki kuwa ndoto ya kufikirika. Masimulizi siku hizi hayakosi kugusa ngono na mbinu za kufanya ngono, hali hiyo huakisi vijana kufanya majaribio ya ngono kwa wajifunzayo kuona na kusikia.

Mfumo wa media nao unachangia maana hata tu taswiraz nyingi zinahamasisha ngonoz, na watu wanafundishana mbinu chafu zenye kuendekeza mambo mabaya kama hayo kwa uwazi, vyombo vya habari na mitandaoni. Kwa mtindo huu ukimwi vigumu kukwepeka.

Hata matumizi ya condom sijui kama yana uzito wa pekee wakati watu wanafanya mengine kupita hata silika ya hayawani wa porini kwa kutumia milango mingine ya maumbile ambayo Mungu hakuiweka kwa makusio hayo.

UCHAFU UCHAFU UCHAFU UNACHEFUA KILA KUKICHA, NA KUAMBIWA UKWELI WANASEMA AJALI KAZINI, SAWA NA KUMPIGIA MBUZI GITAA
 
Kumpata dada ambaye bikra siku hizi ni chanda cha dhahabu, hali kadhalika kumpata kaka asiyekuwa na uzoefu wa mahusiano ya mapenzi ni ndogo. ...

ina maana wengi wa kina dada wanazaliwa bila hiyo na wengi wa kina kaka wanapata uzoefu kabla hawajazaliwa?
 
Huu ugonjwa tusiudharau maana bado unatesa watu wengi....elimu na kubadili tabia ndio njia pekee ya kupunguza maangamizi.Kahama pamechangamka sana...hasa baada ya mgodi wa Buzwagi kusogea pale. kwenye wengi kuna mambo mengi pia
 
tatizo siyo madereva tu....hakuna sehemu ambao nilisha wahi kufika ambako ngono inafanyika hovyo hovyo kama mbuguni, utakuta vitoto vya darasa la tano vina mimba hapoa kuna maderva gani...

Kama unaendesha gari toka Singida ukishaanza kuiacha wilaya ya Iramba na kumaliza mteremko wa mlima Sekenke, kamji kanakofuata endelea hadi Nzega na kisha Kahama ni dhoruba, maana kazi hiyo ni kama ajira ya waliomaliza shule za msingi. Sijajua bado biashara za mikononi kwa vijana wadogo giza likishaingia biashara gani inaendelea, we tulia kidogo maeneo hayo utashtuka, na kama baba mwanao hajakutambua bado utamshtukia, makubwa jamani kinachoendelea duniani hapa.

Happy Pass Over to all
 
ina maana wengi wa kina dada wanazaliwa bila hiyo na wengi wa kina kaka wanapata uzoefu kabla hawajazaliwa?

Boyfriend & Girlfriend mahusiano yanaanza kabla hawajajua ulimwengu ukoje na bado wananukia maziwa ya utotoni, je hayo yatawafikisha kunako ndoa au ni mfumo wa kuiga tamaduni nyingine ambazo wazazi wetu hawakuzoea?

Eti siku hizi lazima watu wafanye majaribio kwanza, na wakijaribiana na kuchokana nini kitaendelea? Katika kujaribiana na kuzoeana hatima yake ni kutwishana mimba baadaye kuchokana hatima yake kila mmoja na njia yake huku hakuna uhakika kama walikuwa makini kujiangalia kiafya. Na mapokea kwa waafrika wengi msichana kisha zaa soko la kuolewa huwa adimu kidogo, bora ajenge njia ya kujitegemea mwenyewe.

Ukimwi unakwepeka kwa wanaojiamini na kuamua kuaminiana baada ya kujihakikishia usalama wao
 
Boyfriend & Girlfriend mahusiano yanaanza kabla hawajajua ulimwengu ukoje na bado wananukia maziwa ya utotoni, je hayo yatawafikisha kunako ndoa au ni mfumo wa kuiga tamaduni nyingine ambazo wazazi wetu hawakuzoea?

Eti siku hizi lazima watu wafanye majaribio kwanza, na wakijaribiana na kuchokana nini kitaendelea? Katika kujaribiana na kuzoeana hatima yake ni kutwishana mimba baadaye kuchokana hatima yake kila mmoja na njia yake huku hakuna uhakika kama walikuwa makini kujiangalia kiafya. Na mapokea kwa waafrika wengi msichana kisha zaa soko la kuolewa huwa adimu kidogo, bora ajenge njia ya kujitegemea mwenyewe.
Ukimwi unakwepeka kwa wanaojiamini na kuamua kuaminiana baada ya kujihakikishia usalama wao

asante kwa maelezo haya lakini hujagusia suala la kinadada bikra kuwa nadra, vile vile kina kaka wasio na uzoefu.
 
Back
Top Bottom