Kahama yaangamia kwa Ukimwi

Kahama yaangamia kwa Ukimwi

asante kwa maelezo haya lakini hujagusia suala la kinadada bikra kuwa nadra, vile vile kina kaka wasio na uzoefu.

Swali lako limejibika katika paragragh zifuatazo

Boyfriend & Girlfriend mahusiano yanaanza kabla hawajajua ulimwengu ukoje na bado wananukia maziwa ya utotoni, je hayo yatawafikisha kunako ndoa au ni mfumo wa kuiga tamaduni nyingine ambazo wazazi wetu hawakuzoea?

Eti siku hizi lazima watu wafanye majaribio kwanza, na wakijaribiana na kuchokana nini kitaendelea? Katika kujaribiana na kuzoeana hatima yake ni kutwishana mimba baadaye kuchokana hatima yake kila mmoja na njia yake huku hakuna uhakika kama walikuwa makini kujiangalia kiafya. Na mapokea kwa waafrika wengi msichana kisha zaa soko la kuolewa huwa adimu kidogo, bora ajenge njia ya kujitegemea mwenyewe.

Kwa mfumo wa bf na gf ubikira wa msichana na mvulana kutokuwa na mahusiano ya ngono yatakwepeka vipi? Unategemea kumpata msichana mwenye mahusiano ya ngono na vijana wangali teenage kubaki bikira? Unatazamia kijana aliyekwisha zoea kucheza na vimwana bila utaratibu mradi ua linachanua na kuvutia kila nyuki hutua na kufyonza utomvu wake atatulia ukubwani na mwandani wake?
 
Ukimwi upoooo,tuwe makini wana JF.tupime kwanza, tuwe waaminifu.
 
Na hivi vikao vya kujuana wanamitandao hapana budi kuwa makini maana kujuana isiwe nongwa ya kujuana kwa undani zaidi kwa wenye jinsia tofauti hadi kufikia hatua ya kuwa kitu kimoja bila tahadhari.
 
Kahama yaangamia kwa Ukimwi

Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 22nd April 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0








ASILIMIA 70 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 20 hadi 49 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa wilayani Kahama, mkoani Shinyanga wameambukizwa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, imeelezwa.

Hayo yamesemwa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kahama, Morgan Mwita katika taarifa ya hali ya Ukimwi katika Wilaya ya Kahama mbele ya wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo wakiwemo watendaji wa kata na viongozi wa dini.

Mwita alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo inatisha hasa miongoni mwa vijana ambapo cha mwaka 2009, maambukizi yalikuwa asilimia 7.3, lakini sasa yamefikia asilimia 9.3 hali ambayo ni mbaya.

Alisema wakati wilaya hiyo ina wakazi 815,175, wakazi 85,342 walijitokeza kupima Ukimwi hadi kufikia Desemba mwaka 2010, na 7,913 waligundulika wameambukizwa virusi vya Ukimwi.

Mwita alisema kutoka na maambukizi ya ugonjwa huo kuwa makubwa, changamoto wanayoipata wao kama Wilaya ya Kahama ni pamoja na kuendelea kuelimisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa na ubaguzi kwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi.

Alisema changamoto nyingine ni pamoja na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hasa katika maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajapa elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huo hatari.

Hata hivyo ofisa huyo aliyataka mashirika mbalimbali kuongeza jitihada za kutafuta fedha za kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu na hatarishi hasa katika upande wa lishe, elimu, ujasiriamali na afya.

Tohara kwa wanaume pia ni muhimu huko maana jamaa hawatahiriwi kule
 
Back
Top Bottom