NGUVUMOJA,
Kama madai ya tetere yana ukweli kuwa Kagame anataka kujenga himaya ya watusi basi nae anataka kuwa kama hao wakubwa wa dunia. Kuna ubaya hapo? Au ya wakubwa tu ndio yawe?
tetere,
Kuwa Kagame ni muuaji, mhalifu madai haya yana ukweli. Lakini kwa sasa ametubu dhambi hizo. Anaelekeza nguvu zake katika kujenga nchi ya Rwanda na kuwainua wanyarwanda. Anatetea maslahi ya nchi yake. Kutofautiana misimamo na nchi zinazoitwa wakubwa wa dunia ndio kisingizio cha kutaka "kumpiga ngwala" na waihujumu Rwanda.
Kasi ya maendeleo ya Rwanda, kanchi kadogo kinawakosesha usingizi baadhi ya watu. Kuna watu wamezoea 10%, pia wapo wanaotaka kuficha udhaifu wa kuongoza nchi zao(uongozi katika nchi zao).
Ukifatilia sana habari za Congo(Zaire) utaona M7 na Kagame walisaidia kumweka Kabila, the father madarakani. Pia kuna ushahidi wa kuwa US na Kabila, mtoto kuhusika katika kifo cha Kabila, the father.
Kwa ufupi, wakubwa wanazichezea nchi zetu vile wanavyopenda na sisi wengine tunawafagilia. Inapasa tubadilike.