Kagame: Kwanini nilimkasirikia Kikwete

Kagame: Kwanini nilimkasirikia Kikwete

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
KAMA sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda, Rais Paul Kagame, alifanya mahojiano na jarida la The African Report… Yafuatayo ni mahojiano hayo, neno kwa neno.

The Africa Report (AR): Miaka ishirini baada ya mauaji ya kimbari, unadhani dunia sasa imeelewa haswa nini kilitokea au kilisababisha kutokea yaliyotokea?
362_kagame2.jpg



Paul Kagame (PK): Kwa bahati mbaya, jibu ni hapana. Taswira iliyoko nje ni ile kwamba mauaji ya kimbari ni kama yalianguka tu kutoka angani. Bila ya sababu au madhara. Hakuna anayepaswa kuwajibika na pia kuna hali ya kutaka kuonyesha kwamba tukio lenyewe limekuzwa tu. Kwa kweli inasikitisha sana.

AR: Je, kutokueleweka huku kwa tukio hili kumesababishwa na ukweli kwamba waliohusika ni watu waliokuwa wakiishi katika jamii moja – jambo ambalo ni la kipekee katika dunia ya sasa?

PK: Kweli kabisa. Kilichotokea ni tofauti na kile ambacho kimetokea kwa watu wengine. Hii limesababisha kuwapo kwa matukio mahususi ambayo wakati mwingine ni muhimu kuyaeleza.
Hata kama kuna watu wanataka jambo hili lifanywe kama mwiko kulizungumzia, hatupaswi kusahau namna baadhi ya mataifa ya magharibi yalivyochangia kwa kilichotokea –si kwa sababu za kihistoria pekee lakini kutokana na kile kilichotokea wakati wa mauaji hayo ya kimbari.

Leo, ni mataifa hayahaya ya magharibi ambayo ndiyo yanahubiri kuhusu masuala ya utawala bora na demokrasia.

Wangependa Wanyarwanda waendelee kuishi kana kwamba hakuna kilichotokea; jambo ambalo lina faida kwao kwa vile linamaanisha watu wangesahau kuhusu kuhusika kwao kwenye mauaji hayo.

Chukulia mfano wa Ufaransa. Miaka 20 baada ya mauaji ya kimbari, jambo pekee wanalodai kujutia ni kwamba hawakufanya vya kutosha kuzuia mauaji yale yasiendelee. Japo huo ni ukweli, unaficha ukweli mwingine mkubwa zaidi kuhusu namna Ufaransa na Ubelgiji zilivyoshiriki katika kuandaa mazingira ya mauaji hayo na namna pia Ufaransa ilivyoshiriki kabisa katika mauaji hayo.

AR: Unalaumu hizi nchi kwa kupanga mauaji au kwa kushiriki katika tukio hilo?

PK: Vyote ! Uliza waathirika wa mauaji ya Bisesero Juni mwaka 1994 na watakueleza nini askari wa Jeshi la Ufaransa walifanya kupitia kile kilichoitwa Opération. Kule Bisesero na katika maeneo ya jirani yaliyotengwa kwa ajili ya Utoaji wa Huduma za Kibinadamu, Wafaransa hawakuwa watazamaji tu bali pia walishiriki katika mauaji hayo.

AR: Sababu nyingine ya kufanya ugumu wa kuelewa kuhusu tukio lenyewe ni ukweli kwamba unaonekana kama kiongozi wa taifa ambaye si wa kawaida. Uko tofauti kidogo. Unafahamu hili?

PK: Sifahamu kabisa. Kama kuna tofauti yoyote, itakuwa ni kwa sababu ya uzoefu nilioupata katika maisha yangu na historia ya kipekee ya taifa langu. Lakini, kama mtu anazungumzia kuhusu maendeleo na utawala, taifa langu lina changamoto zilezile zilizopo katika nchi nyingi za Afrika.

AF: Ingawa mafanikio yako katika maeneo ya kijamii na kiuchumi yamekuwa yakipongezwa, rekodi yako kama mwana demokrasia imekuwa finyu. Unazungumziaje kuhusu hili?

PK: Unamaanisha demokrasia ipi? Kama unamaanisha ile ya nchi za Magharibi ambayo wanatulisha inayoelezea kuwa Demokrasia inatokana na watu na kwa ajili ya watu na inayochagiza Uhuru wa Kujieleza, Kutoa Mawazo na Kuchagua. Cha ajabu, wakati watu wa Rwanda wanapoamua kutumia uhuru wao wa kuchagua; utasikia watu haohao wa magharibi wakilalama; ‘Hapana, mmekosea. Maamuzi yenu si mazuri kwenu.'

Kilicho wazi ni kwamba wenzetu wanataka ufuate aina ya demokrasia wanayoitaka wao na si demokrasia ya kweli. Kuna nchi nyingine za Afrika ambazo zimejaa ukabila, rushwa, wizi na kila aina ya uovu lakini hazisemwi kwa sababu zimeamua kufuata mambo fulani ambayo yanapendwa na mabwana wakubwa.

Hivyo, kama maana ya demokrasia ni kufuata tu maelekezo wanayotaka mabwana wakubwa, basi mimi mtazamo wangu ni tofauti kuhusu demokrasia.

AR: Muda wako wa kuwa madarakani unamalizika mwaka 2017 na Katiba ya Rwanda inakukataza kuwania tena nafasi hiyo. Msimamo wako ukoje kwenye hilo?

PK: Mara zote nimekuwa nikisema nitaiheshimu Katiba. Hata hivyo, napenda kusema kuwa Katiba ni maelezo kuhusu matamanio ya wanancho katika wakati fulani na kwenye muktadha husika.
Duniani kote, iwe katika nchi ambazo demokrasia imekomaa na katika nchi change, sheria za msingi zimekuwa zikibadilishwa, kufanyiwa mapitio na kurekebishwa kutokana na maslahi ya wananchi.

AR: Vipi kuhusu ukomo wa kubaki madarakani.

PK: Kuhusu hilo, kama ilivyo kwenye mengine, sina jibu la moja kwa moja. Sina uamuzi kuhusu hili na mimi si mwandishi wa Katiba. Kwanini watu wamening'ang'ania sana kuhusu jambo hili? Jambo la msingi unalotakiwa kuliweka akilini ni kwamba mimi ninaheshimu Katiba na nitaendelea kuwa hivyo.

AR: Inaonekana hakuna hata Mnyarwanda mmoja anayeamini kwamba utaachia madaraka mwaka 2017?

PK: Unatakiwa kujiuliza je ni kwa sababu wanadhani kwamba ninataka kubaki madarakani au kwa wanataka niendelee kubaki madarakani? Hili ni swali ambalo unatakiwa kuwauliza wananchi. Jambo moja ni lamuhimu sana kulielewa kuhusu mimi; Kama wananchi watawasilisha kwangu mapendekezo yao kuhusu mojawapo ya hilo, ni wazi iitabidi nifanye maamuzi.

AR: Kuna ugumu kidogo kujenga picha yako ukiwa na umri wa miaka 60 na umestaafu ukitazama ng'ombe wako katika ranchi yako iliyopo pembezoni ya Ziwa Muhazi.

PK: Kwanini isiwe hivyo? Mimi naiona hiyo picha. Hilo ni jambo linalowezekana kabisa.

AR: Tangu mauaji ya mwanasiasa wa upinzani, Patrick Karegeya na shambulizi dhidi ya Jenerali Kayumba Nyamwasa nyumbani kwake nchini Afrika Kusini, uhusiano baina ya Rwanda na Afrika Kusini umezorota. Mlikutana na Rais Jacob Zuma mjini Luanda, Angola Machi 25 mwaka huu, mlizungumza nini siku hiyo?

PK: Mazungumzo yetu hayakuzama kwenye mambo hayo ingawa tuligusia kidogo jambo hilo. Msimamo wangu kwenye suala hilo uko wazi; kwamba kupata hifadhi ya kisiasa kwenye nchi ya nje kunamaanisha wajibu wa kukaa kimya na kuacha vitendo vya kichochezi dhidi ya nchi yako.
Hivyo, kimsingi, mimi sina tatizo na watu kupata hifadhi ya kisasa. Tatizo langu liko kwenye uhuru na wakati mwingine msaada wa ngazi za juu ambao watu kama akina Nyamwasa walioko Afrika Kusini wanaupata ili waweze kuhatarisha hali ya Rwanda na kuchochea ugaidi.

AR: Uliomba serikali ya Afrika Kusini iwarejeshe Rwanda Karegeya na Nyamwasa?

PK: Hakika tulifanya hivyo na taarifa za kumbukumbu kuthibitisha hilo tunazo. Watu hawa waliwahi kushitakiwa wakiwa nchini Rwanda na kukutwa na makosa na kuhukumiwa wakiwa hapa.

AR: Lakini Afrika Kusini haina imani na mfumo wenu wa sheria ….

PK: Huo ni upotofu. Afrika Kusini inatakiwa kuwa makini ili isitoe picha kwamba inaelemea upande mmoja katika suala hili. Nina matumaini makubwa kwamba baada ya muda, serikali ya Afrika Kusini itabaini kwamba itapata faida kubwa sana kwa kutusikiliza badala ya kusaidia kuficha maovu ya wakosaji.

AR: Wakati wa kilele cha mgogoro wenu na Afrika Kusini, mlifukuza mabalozi wa pande zote mbili. Je, mtawarudisha?

PK: Tuko katika taratibu za kuwarejesha.

AR: Tangu Zuma awe Rais wa Afrika Kusini, uhusiano wako na taifa hilo umeyumba. Je, hii ni kwa sababu ameamua kuwa rafiki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo ni hasimu wako wa kisiasa?

PK: Siwezi kujibu kwa niaba yake. Lakini jambo moja liko wazi kwangu; Sishauri mtu yeyote aingilie katika mambo yangu ya ndani. Huu ni msimamo wangu na haujalishi ni nchi gani; iwe Afrika Kusini, Tanzania, Ufaransa, au Ubelgiji.

AR: Karegeya, Nyamwasa lakini pia Mwendesha Mashitaka Mkuu wa zamani, Gerald Gahima pamoja na Théogène Rudasingwa walikuwa karibu sana na wewe kabla hamjatofautiana. Huna wasiwasi na watu hawa wanaoondoka wakiwa na siri zako nyingi.

PK: Siri gani? Hawa watu walikuwa na nyadhifa katika Jeshi, Usalama, Mahakama na katika siasa kupitia RPF wakiwa chini yangu. Huwezi kusema hawa walikuwa karibu yangu kwa sababu nilikuwa nao kwenye taasisi moja. Wamesema kila walilosema, tena kwa muda mrefu, lakini kuna siri gani waliyozungumza zaidi ya upuuzi?
Wakati tulipokuwa tukifanya kazi pamoja, hawakuwahi kupinga lolote nililopendekeza. Walianza kutofautiana name baada ya kuondolewa kwenye nyadhifa zao.

AR: Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania alikumbana na hasira zako wakati alipopendekeza ukutane kwa mazungumzo na wapinzani wako wakiwamo wale wa FDLR. Hukubaliani na mawazo hayo?

PK: Kitu nisichokubaliana nacho ni kuingiliwa. Haikubaliki kwamba Jakaya Kikwete na serikali yake wajihusishe, kwa namna yoyote, na watu waliohusika na mauaji ya kimbari. Sioni sababu yoyote ya mtu kujihusisha nayo.


Chanzo;Raia mwemaraiamwema.co.tz

Pia, soma: Kagame tells Kikwete "I will hit you......"
 
kagame mkurupukaji tu, ni jamii ya akina dr slaa anakurupuka alafu akigundua kafanya fyongo anabuni mpango wa kutafta public sympath
 
Anajifanya hawaoni wapinzani wake wakati wanamsokota
 
Mahojiano


Mwandishi Wetu Kigali, Ruanda Toleo la 362 16 Jul 2014



KAMA sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda, Rais Paul Kagame, alifanya mahojiano na jarida la The African Report… Yafuatayo ni mahojiano hayo, neno kwa neno.

The Africa Report (AR):
Miaka ishirini baada ya mauaji ya kimbari, unadhani dunia sasa imeelewa haswa nini kilitokea au kilisababisha kutokea yaliyotokea?


Paul Kagame (PK)
: Kwa bahati mbaya, jibu ni hapana. Taswira iliyoko nje ni ile kwamba mauaji ya kimbari ni kama yalianguka tu kutoka angani. Bila ya sababu au madhara. Hakuna anayepaswa kuwajibika na pia kuna hali ya kutaka kuonyesha kwamba tukio lenyewe limekuzwa tu. Kwa kweli inasikitisha sana.
Hili jibu halina ukweli wowote ule!! Ukweli ni kwamba, wakati jumuiya ya kimataifa inaamini Rwanda Genocide ambayo Wahutu na Watutsi waliuawa, Kagame na timu yake anataka tuamini ile haikuwa Rwanda Genocide bali Tutsi Genocide ingawaje anafahamu kwamba kulikuwa na Wahutu wenye msimamo wa wastani ambao pia waliuawa!!! Jumuiya ya Kimataifa yenye akili timamu, haiwezi kumu-exclude hata Mhutu mmoja aliyeuawa na badala yake iseme waliouawa ni Watutsi pekee!!!
 
AR:
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania alikumbana na hasira zako wakati alipopendekeza ukutane kwa mazungumzo na wapinzani wako wakiwamo wale wa FDLR. Hukubaliani na mawazo hayo?

PK:
Kitu nisichokubaliana nacho ni kuingiliwa. Haikubaliki kwamba Jakaya Kikwete na serikali yake wajihusishe, kwa namna yoyote, na watu waliohusika na mauaji ya kimbari. Sioni sababu yoyote ya mtu kujihusisha nayo.
Yaani jirani anakushauri fanya mazungumzo na waasi mtu unasema anaingilia kuingiliwa mambo yao!! Yaani amesahau kabisa kwamba michezo yao ya kuhusudu bunduki, Tanzania huwa tunaathirika nayo moja kwa moja...
 
Hapo kwenye suala la DEMOKRASIA amenikosha sana,anasema kama Demokrasia ni kufuata tu yale unayoamriwa na mabwana wakubwa wa Magharibi yeye hayuko tayari kuifuata,Akashangaa unafiki wa Nchi za Magharibi kukaa kimya juu ya nchi zenye rekodi mbaya kuhusu Demokrasia,Haki za Binadamu,Rushwa,Ubadhirifu,nk,Mimi nahisi kama anamaanisha Tanzania vile?
 
Kuhusu kuondoka madarakani, naona Kagame na Mugabe lao moja!
 
Kuna vitu Kagame ananishawishi.
Kama hilo la kutokubali kupangiwa na nchi za magharibi kwa kisingizio cha kinachoitwa 'demokrasia'.
Hapo kwenye suala la DEMOKRASIA amenikosha sana,anasema kama Demokrasia ni kufuata tu yale unayoamriwa na mabwana wakubwa wa Magharibi yeye hayuko tayari kuifuata,Akashangaa unafiki wa Nchi za Magharibi kukaa kimya juu ya nchi zenye rekodi mbaya kuhusu Demokrasia,Haki za Binadamu,Rushwa,Ubadhirifu,nk,Mimi nahisi kama anamaanisha Tanzania vile?
Hiyo ndio kauli ya madikteta wote duniani... ndio defensive mechanism wanayotumia kuhadaa watu! Ingawaje nakubaliana na kauli kwamba demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa ndio demokrasia ya afrika au asia, lakini madikteta wamekuwa wakitumia kauli hii kuhalalisha udikteta wao!! Huwezi kusema kwamna ikiwa XYZ wana makosa basi wapelekwe mahakamani badala ya kuwa-assassinate kisha mtu akajificha kwenye hoja ya kwamba demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa ya africa as if huku kwetu suala la kutafuta haki halina nafasi!! Huwezi kuambiwa tunataka uwazi katika utendaji wa serikali halafu mtu akasema demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa sawa na Africa. Huwezi kuambiwa heshimu katiba, halafu ukasema hiyo ni demokrasia ya magharibi!! Huwezi kuambiwa waache wananchi wawe na uhuru wa kutoa maoni bila kuogopa, halafu ukasema demokrasia ya magharibi na ya africa ni tofauti!! Ma-dikteta wengi, demokrasia ambayo wanai-abuse na kisha kujificha kwenye kichaka cha kusema demokrasia magharibi haiwezi kuwa sawa na Africa or elsewhere inafanana na mifano niliyotoa hapo juu!!

Ni kweli kabisa kwamba zipo demokrasia za kipumbavu kama zile wanazotuambia akina Cameron, kama zile za kuyataka makanisa yetu yaruhusu kutawaza ma-padri mashoga... hili sawa... ya magharibi haiwezi kuwa sawa na africa!! Lakini demokrasia wanazoambiwa watu kama akina Kagame si sawa na hizo ingawaje wakikutana na hizo ndipo huonesha makali yao zaidi ili kuhadaa umma kama alivyofanya Museven!!
 
Hiyo ndio kauli ya madikteta wote duniani... ndio defensive mechanism wanayotumia kuhadaa watu! Ingawaje nakubaliana na kauli kwamba demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa ndio demokrasia ya afrika au asia, lakini madikteta wamekuwa wakitumia kauli hii kuhalalisha udikteta wao!! Huwezi kusema kwamna ikiwa XYZ wana makosa basi wapelekwe mahakamani badala ya kuwa-assassinate kisha mtu akajificha kwenye hoja ya kwamba demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa ya africa as if huku kwetu suala la kutafuta haki halina nafasi!! Huwezi kuambiwa tunataka uwazi katika utendaji wa serikali halafu mtu akasema demokrasia ya magharibi haiwezi kuwa sawa na Africa. Huwezi kuambiwa heshimu katiba, halafu ukasema hiyo ni demokrasia ya magharibi!! Huwezi kuambiwa waache wananchi wawe na uhuru wa kutoa maoni bila kuogopa, halafu ukasema demokrasia ya magharibi na ya africa ni tofauti!! Ma-dikteta wengi, demokrasia ambayo wanai-abuse na kisha kujificha kwenye kichaka cha kusema demokrasia magharibi haiwezi kuwa sawa na Africa or elsewhere inafanana na mifano niliyotoa hapo juu!!

Ni kweli kabisa kwamba zipo demokrasia za kipumbavu kama zile wanazotuambia akina Cameron, kama zile za kuyataka makanisa yetu yaruhusu kutawaza ma-padri mashoga... hili sawa... ya magharibi haiwezi kuwa sawa na africa!! Lakini demokrasia wanazoambiwa watu kama akina Kagame si sawa na hizo ingawaje wakikutana na hizo ndipo huonesha makali yao zaidi ili kuhadaa umma kama alivyofanya Museven!!
Amewahitaji warudi washitakiwe nyir na mabwana Zenu wakubwa mmewakatalia. Alafu bado wanaongea ongea upuuzi . Lazma wauliwe . Yenu APA bongo yamewashinda kutwa kumpangia mambo yake kagame
 
Unatakiwa kuwa mwehu ili kupingana na ukweli ambao Kagame amekuwa akiusimamia siku zote. Swali muhimu ni hili, je wakati wa mauaji ya Rwanda jumuiya ya Kimataifa ilifanya nini kuyakomesha? Hiyo inayoitwa Demokrasia haikuwepo wakati huo? Wakati JK anamshauri Kagame kuzungumza na waasi wauaji, Chama chake Dodoma mpaka leo hakitaki Serikali ya umoja wa Kitaifa Zanzibar! Chama Chake hakitaki mawazo ya Wananchi kwenye Katiba mpya! Inashangaza!
 
Back
Top Bottom