Kafulila kuendelea na ubunge

Kafulila kuendelea na ubunge

Mi nasubiri hitimisho la hili jambo,maana sijaelewa kitu ngoja nisubiri tu kitakachokuwa kikiendelea,maana utoaji wa habari wa namna hii bila kuweka mambo kwa upana wake hautupi uwanja mpana wa kujadili
 
poor politic,, angekuwa mbunge wa ccm anamfatafata kafulila hata ni marafiki mgesema mengine, ila kwa kuwa ni zitto mnaona ni sawa, mimi naona mna areji na ccm na sy matatizo yaliyopo nchini mwetu.
 
Ni amri ya Mahakama. Habari ndio hiyo!

SOURCE: http://twitter.com/#!/zittokabwe

===================

Zitto Kabwe


Kafulila kuendelea na Ubunge..... Mahakama Kuu imetoa amri muda mfupi uliopita.

Ataendelea kuwa Mbunge mpaka hapo kesi ya msingi itakapokwisha. Mungu yupo pamoja na wanyonge siku zote.


Naanza na huyu Zitto...huyu jamaa anamaslahi gani na Kafulila? au anataka tuamini kuwa wana agenda ya siri ili kuitawala NCCR? Kwanini Zitto unafanya mambo ya kipumbavu namna hii? unaonyesha kuwa unaagenda kubwa ya siri na tunapaswa kukuchunguza kwa makini...

Kafulila usijidanganye,hakuna sheria inayoweza kuingilia maamuzi ya chama kama yalifanywa chini ya kanuni na taratibu za chama,na wakati mwingine tuwe tunafikiri,hata kama umerudishwa unadhani utafanya kazi kwa ustadi wakati chama kina kinyongo na wewe? kwanini kuendelea kung'ang'ania sehemu ambapo hawakutambui?
 
..wana CDM endeleeni tu kufurahia hili jambo.

..siku mtakapomfukuza ubunge Shibuda halafu mahakama ikalazimishe awe mbunge ndipo mtakapojuta.
 
kafanya jambo la mbolea tafadhali tuambien kesi namba na parties na judge ili tuifuatilie
 
Urafiki wa Zitto na Kafurila unaacha maswali mengi kuliko majibu, sikubaliani kabisa na Uongozi wa James Mbatia lakini ihuyu Kafurila na Zitto ni watu hatari sana kwa afya ya upinzani.
 
Napenda uamuzi wa mahakama kuu.. sasa kijana atulie ajipange vizuri na ajifunze..

kuwa kiongozi wa siasa ni pamoja na kuwaheshimu wenye mamlaka ya juu... so aombe masamaha na atulie..
 
Nchi zinazoendelea kama Tz maamuzi ya mahakama huwa pia yanachagizwa na wanasiasa hasa serikali iliyoko madarakani.
Kuna uwezekano wa mambo matatu kutokana na uamuzi huu:
1. Uamuzi huru wa mahakama kulingana na pingamizi lililowekwa na Kafulila
2. Kutokana na hali mbaya ya kifedha serikali imeamua kutia mkono ili kupiga dana dana kesi hadi ifike 2015.
3. Serikali kuweka mkono kama ilivyojaribu kwa madiwani kule Arusha na kisha kutumia kesi hii ''ku-mblackmail'' Kafulila ili aweze kurudi kwenye mstari na ale kiapo cha utii kwa Mbatia na kumsaidia Mbatia kuhujumu upinzani kama inavyosemwa na wengi kuwa Mbatia ameifanya NCCR kuwa CCM-C.
Kwa vile Kafulila hajawahi kupewa barua rasmi wala NCCR hawajawahi kuiarifu tume ya uchaguzi na msajili wa vyama juu ya uamuzi wao wa kumfuta David, namba 3 naipa uzito zaidi.

Ni mtazamo tu sio lazima uwe sahihi...
 
Potezea mwanangu Kafulila mpaka 2015 karibu na uchaguzi alafu urudi nyumbani kwa sababu hakuna aliyekufukuza.
 
Kafulila rudi kwetu ukavae gwanda, hata mimi naona fahari kuvaa gwanda
 
Nchi zinazoendelea kama Tz maamuzi ya mahakama huwa pia yanachagizwa na wanasiasa hasa serikali iliyoko madarakani.
Kuna uwezekano wa mambo matatu kutokana na uamuzi huu:
1. Uamuzi huru wa mahakama kulingana na pingamizi lililowekwa na Kafulila
2. Kutokana na hali mbaya ya kifedha serikali imeamua kutia mkono ili kupiga dana dana kesi hadi ifike 2015.
3. Serikali kuweka mkono kama ilivyojaribu kwa madiwani kule Arusha na kisha kutumia kesi hii ''ku-mblackmail'' Kafulila ili aweze kurudi kwenye mstari na ale kiapo cha utii kwa Mbatia na kumsaidia Mbatia kuhujumu upinzani kama inavyosemwa na wengi kuwa Mbatia ameifanya NCCR kuwa CCM-C.
Kwa vile Kafulila hajawahi kupewa barua rasmi wala NCCR hawajawahi kuiarifu tume ya uchaguzi na msajili wa vyama juu ya uamuzi wao wa kumfuta David, namba 3 naipa uzito zaidi.

Ni mtazamo tu sio lazima uwe sahihi...

Una akili. Unafaa kuwa kiongozi.

Ningekua mimi serikali ningechukua OPTION number 2.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida zitto, kafulila na wakili wao wanayemtumia kuwatetea na kuua upinzani wanalumiwa na waandishi wa habari kwa kuwapatia taarifa za uongo kuhusu Rulling iliyotolewa na mahakama kuhusu hatma ubunge wa kafulila. Imeelezwa hivyo na wakili wa nccr mageuzi na mtaalamu aliyebobea katika masuala ya sheria Dr. Mvungi ambaye amewapatia nakala ya rulling ya mahakama na kubaini kuwa akina zitto wamewapotosha na hivyo kuandika taarifa zisizokuwa za kweli. Uongo ni mbaya sana, wana nia nzuri kweli hawa?
 
Uongo gani, mbona haueleweki? Tupe hiyo taarifa sahihi basi kama ya kwao ni ya uongo.
 
Ebu tupatie ukweli badala ya kulalama ka mtoto mdogo.
 
Lete taarifa: asubuhi ya leo redio moja imetangaza kuwa Mahakama imetengua uhamuzi uliofikiwa na kamati ya NCCR-mageuzi kwa kumfutia uanachama na ubunge Mh.Kafulila. huo ndo uongo au kuna uongo mwingine?????
 
katika harakati za kabwe kutaka kujisogeza pale magogoni.amejikuta anaangukia pua baada ya kudanganya waandishi nasi wadau hapa jamvini eti kafulila ameruhusiwa na mahakama kuendelea na kazi za kibunge mpaka kesi ya msingi isomwe.Dr mvungi amewahabarisha waandishi ukweli wakabaki wanashangaa na kujiuliza wamfanye ni kabwe kwa kuwadhalili,inshort hakuna taarifa ya mahakama inayosema alivyotuambia kabwe juu za mshirika wake.na kabwe jitazame utashusha heshima yako kwa jamii kwa kutaka umarufu kwa hila
 
Back
Top Bottom