Kadi yangu ya CCM niifanye nini?

Yaani hivi vijamaa vinanikera?.....Viswahili sana!....Mbaf...Ndo Makamba kaweka historia ya Katibu Mkuu asiyekuwa na digrii!...

Sometimes, nashindwa kujizuia machozi nikiwakumbuka viongozi mahiri waliowahi kuongoza sekretarieti kuu ya ccm, miongoni mwao kwa uchache wakiwemo Daudi Mwakawago na Philip Mangula. CCM ya leo imepoteza dira, haina mwelekeo wala mvuto kwa wananchi. Kidumu Chama cha Mapinduzi kipi, hiki hiki au kingine? Mangula kama unanisoma tafadhali ingia jamvini JF utupie japo mistari miwili ya kutujenga wanaccm wa ukweli tuliosalia. Jinsi JK anavyoirostisha ccm ni sawa na kundi la kondoo lililokosa mchungaji, ni kama kusema 'mchungaji katokomea kusikojulikana, na kundi la kondoo wake limetawanyika' . Wapi Gama, wapi Tandau, wapi Ali Ameir? Turudishiwe CCM yetu tukomae nayo kivyetuvyetu na mafisadi wote tuwatose!
 

Michelle, naona kama jamaa wa ikulu wamekanusanusa haka kathread, maana kuna dalili za mageuzi makubwa ya uongozi wa juu kwa kuanzia na Makamba kabla ya mwisho wa mwezi huu. JK naye jana kakubali yaishe yacje kumkuta ya misri na algeria, ndio maana karidhia kwa shingo upande DOWANS iclipwe, tusubiri tuone mwisho wa mwezi cmbali. Ila wakigeuka geuka kama vinyonga, cha moto watakiona, wanaccm hatutakaa kimya ng'o!
 
irudishe ulipoitoa
 
"Subira yavuta heri" pia "faida ya mjinga ni kuumia"!
Hayo yote ya wahenga mi nakumbushia tu!
 
bado una kadi ya ccm?
Bado ninayo maana naamini katika mapinduzi ya dhati sambamba na azimio la arusha(misingi ya utu). Kwa sasa silipi ada! Uchaguzi mkuu uliopita sikukipa kura yangu mimi na rafiki zangu maana tunataka mapinduzi yale tuliyolilia na enzi za Mwaaaalimu.
 
Bado ninayo maana naamini katika mapinduzi ya dhati sambamba na azimio la arusha(misingi ya utu). Kwa sasa silipi ada! Uchaguzi mkuu uliopita sikukipa kura yangu mimi na rafiki zangu maana tunataka mapinduzi yale tuliyolilia na enzi za Mwaaaalimu.

kidumu chama cha mapinduzi. Mapinduziiii.........daimaaaaa!
 
kuna umuhimu wa kufanya mapinduzi ndani ya CCM ili wale mafisadi wote waondoke.
 
ichane tu, sio deal tena, ni ishara ya ujinga, ufisadi na ulimbukeni!
 

Hizo kadi zenu ziwekeni kama kumbukumbu (souvenir) siku moja mtasimuila wajukuu zenu na pengine kuwaeleza mlivyoshiriki kulifikisha Taifa hapa lilipo.

Wanachama wa ccm Historia itawahukumu kwani kwa kiasi kikubwa mnawajibika kwa matokeo ya uongozi tulio nao sasa hivi, na pengine kwa asilimia kubwa ndio wamekuwa wanufaika wakubwa wa bakshishi nyakati za chaguzi kupitia takrima, posho za vikao, mikopo ya vikundi na hata pesa za kununulia kura. Uwingi wenu hamjautumia kutuwekea uongozi mzuri bali mmekuwa mkiangalia zaidi mnachopewa wakati ule na baadae kujaribu kutupa lawama kwa wasiohusika.
 


usiitupe, mimi ninayo nilichofanya nimekuwa mwanaharakati imara.Nikifungua droo naitazama na kutokwa machozi.Lakini uwezo wa kufanya jambo sina,kwani tungekuwa na mshikamano tungeandamana wanachama na kudai mabadiliko ya ungozi wa juu wa chama kukinusuru.
 

Acha ujinga kama umekichoka Chama basi rudisha kadi yao na chukua ya chama unachokitaka. Vile vile kuwa na kadi ya chama zaidi ya kimoja sio dhambi wala uvunjifu wa sheria.

fanya maamuzi sahihi na sio kuleta hoja mgando hapo. Kuna wengi wanajiunga na wengi wanajitoa lakini chama kimayea na kuchukua ushindi wa sunami.

Jitoe tu wengine wengi wanataka kuingia.
 
Endelea kulipia kadi yako ili uwe mwanachama hai, nashauri usichoke kutoaushauri wako katika chama chako. si mna vikao kwan vikao vyenu vimekwisha?
 
mAKAMBA POLE SANA MKUU! ILA CCM IMECHOKA MKUU!
 
Unanikumbusha jinsi tulivyokuwa tunabambikiziwa JKT hizo kadi baada ya propganda kali za kada wa chama. That time ilikuwa mkiingia kweye kipindi cha siasa inakuwa mapozeo ya mitulinga jeshini.
 
ihifadhi vizuri siku akukuudhi mtu umfungie kwenye bahasha kama zawadi umpostie
 
wewe nakushauri uhamie chadema
 
Ngoja tuone watakavyofanya DOWANS, ndio kitaeleweka. Maana dado kuna watu wanaleta mchezo.

Hakuna la kusubiri. Wewe utakuwa sikio la kufa lisilosikia dawa. Maovu yaliyofanywa na CCM hayana ata kipimo. Mtu mwenye akili na mcha Mungu awezi kuendelea kuwa CCM. Maovu yanayoendelea ni zaidi ya bln 94 za DOWANS. Kadi chaomeni. Mwombe Mungu akunusuru maana wewe umeshatengenezwa msukule wa CCM. Kwa kifupi wanachama wa CCM wamekuwa kama toilet paper ambayo haina maamuzi kutumika maala pachafu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Mungu nibariki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…