Kadhia ya VODACOM na Utaifa wetu: LUNDENGA Kufungwa Kengele Rasmi

Haya maswalia yanamikataba,hauwezi kukurupuka ukasema naondoa udhamini,unashitakiwa na unashindwa.Pili hela ya udhamini haitolewi siku ya tukio,labda uelewa wako mdogo mkuu
Hapa vodacom wamekosea jamani. Hata hao LINO pia wamekosea kabisa. Unaju hata kama vodacom walitishia kutowapa udhamini basi LINO wao wangeonyesha msimamo wao. Hapa inabidi tuchukue hatua zaidi ikiwa ni pamoja na kutomtambua mshindi wa hilo shindano.

Mimi nitashangaa kabisa eti huyo mlimbwende anajihusisha katika shughuli za kusaidia jamii. Ni jamii ipi hasa anilenga wakati tangu mwanzo hakuwa na huruma kama hiyo? Huyu pia yapaswa tumkatae kwa sauti kuu, tumwambie hatukutambui na pia hatutaki misaada yako. Iweje utukumbuke leo wakati ulitudharau siku tulipopatwa na majonzi makuu ya taifa letu?

Hapa ili vodacom wajisafishe kwa jamii ni lazima wafanye haya mambo yafuatayo
1.Kwanza inatakiwa kuwafukuza kazi wale wahusika wa moja kwa moja na jamii(Mkurugenzi wa mahusiano ya jamii, hapa ni Mwamvita Makamba), pia meneja mahusiano bwana Salumu mwalimu.

2.Wasitishe huduma kwa huyu mshindi wa miss Tanzania kwa kipindi chake choote atakachokuwepo katika taji lake.
3.Wafute udhamini kwa mashindano ya miss Tanzania kuanzia mwakani.
4.Waombe radhi hadharani kwa kitendo chao cha kukosa utu.
5.Wajitathimini upya mahusiano yao na jamiii kwa sasa na penye tatizo walishughulikie mara moja. Hapa waje na sura mpya kabisa kwenye safu ya uongozi na si kuwaona tena Mwamvita Makamba na Salum Mwalimu.

Vodacom chukueni hatua vinginevyo mtaangamia kibiashara. Ninyi ni kampuni achaneni na mambo ya kuwabeba watu waliosababisha muwe katika hili zogo.
 
Mimi binafsi ni mteja wa Vodacom tangu imeanzishwa mpaka sasa,lakini napingana na kilichoendelea jmosi. Sijaona hoja ya kunishawishi kama baadhi yetu humu kwamba Vodacom haina makosa. Na ni matarajio yangu siku chache kuanzia sasa,uongozi wa Vodacom na Lino wataomba msamaha. Kama waliona wasingeweza kuharisha,hapakuwepo sababu ya kuonyesha hiyo show yao Live. Wangeweza kurekodi wakaonyesha baada ya maombolezo. Natarajia kampuni zetu kubwa zitajifunza kutokana na tukio hili, kuajiri watu wenye weledi na wenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa wakati sahihi. Tunajua uzembe wa kwanza ni wa mwenye meli,pili ni watendaji wa serikali za CCM na tatu ni wananchi wenyewe walioshindwa kujitetea. Mapambano hayo ya kuondoa uozo nadhani tutayafanikisha 2015.
 
Mbona CCM walizindua kampeni Igunga tena kwa mbwembwe za hatari lakini hawalaumiwi?
 
Mtu kujaribu kutaka kutetea chochote hapa ni upuuzi mtupu.kampuni ya kishenzi sana hii...wanajeuri coz wanaweza kubadili jina na rangi muda wowote tena kwa kukwepa kodi...Mtu anasema eti uzembe wa SMZ hauwezi kusababishia watu wengine hasara..hivi unatoka chumbani umeshavaa unaratiba ya kwenda kwenye kikao cha harusi,unafika sebuleni unakutana na mtoto kaungua moto jikoni kisa wife alitoka nje mara moja kumwaga takataka, utamuacha mtoto ukaenda zako kwenye harusi halafu baadae ukirudi unamtuhumu wife kuwa mzembe na ndio chanzo cha mtoto kuungua???watu wengine wanafikiria kwa viuno nafikiri
 
Mimi nadhani Zitto alikuwa kidogo hayuko composed au tuseme alikuwa na hasira kiasi fulani wakati anaandika yale maneno kuhusu Vodacom.
Kwa kusambaza ujumbe ule mtandaoni kuwa yeye hatatumia mtandao wa Vodacom siku ile nadhani aliteleza kidogo..! Kibiashara hii kitu haijakaa vizuri kabisa kwa Vodacom kwa mtu mwenye ushawishi kama Zitto kususia huduma zake japo kwa siku moja....! Zitto amesoma biashara kwa hiyo anajua matokeo ya maandishi aliyoyatuma mtandaoni! Ingekuwa kwa wenzetu walioendelea hata yeye mwenyewe angekuwa kwenye kiti moto.
Leo nimemsikia Zitto japo siyo toka mwanzo kwenye radio ya East Africa....sidhani kama ameligusia hili la Vodacom(mliomsikia toka mwanzo mnisahihishe). Lawama zake kwa vyombo vya habari hajazipeleka sana kwa vyombo binafsi vya habari. Anasema vyombo binafsi vinaendeshwa na matangazo kwa hiyo wanakuwa na mipangilio yao fulani....ila lawama kubwa kazipeleka TBC1 kwa sababu ni chombo kinachoendeshwa na kodi zetu sisi wenyewe kwa hiyo walikuwa na jukumu la kutangaza hicho kitu...anataka wa TBC1 wawajibishwe...! mimi najiuliza watawajibishwaje wakati vyombo vya habari vimeshapongezwa kwenye ile hotuba iliyosomwa na luhanjo !!mh
 
Jamani eeeh..!! Hizo zote hapa ni kelele tu. Voda si waandaaji wala wasimamizi wa shindano la mamiss. Wao wametoa pesa za gharama na zawadi kwa washindi kabla hata ya ajali kwa hao waandaaji, sasa hapo kosa lao nini!!!?
 
katika sakata hili la VODACOM sijasikia mtu akigusia suala la vyombo vingine vya habari kama clouds, C2C, EATV, DTV na vinginevyo ambavyo vimekuwa vikiendelea kupiga muziki wa starehe kuwaburudisha watu kama kawaida ingawa serikali imetoa siku 3 za maombolezo tamati yake ikiwa ni leo. hii ina maana vyombo hivi havijaguswa na janga hili, nakumbuka baba wa taifa alipofariki mwaka ule serikali ilitangaza siku 30 za maombolezo hakuna kituo hata kimoja cha redio au televisheni kilichopiga muziki wa burudani isipokuwa nyimbo za maombolezo kwa muda wa siku zote 30, lakini leo siku 3 tu burudani na muziki kama kawaida na hakuna anayeliongelea hili.
<br />
<br />
Mkuu, serikali ya sasa ni legelege zaidi kuliko ile ya wakati ule, ndo maana haiheshimiwi.
 
Mtu kujaribu kutaka kutetea chochote hapa ni upuuzi mtupu.kampuni ya kishenzi sana hii...wanajeuri coz wanaweza kubadili jina na rangi muda wowote tena kwa kukwepa kodi...Mtu anasema eti uzembe wa SMZ hauwezi kusababishia watu wengine hasara..hivi unatoka chumbani umeshavaa unaratiba ya kwenda kwenye kikao cha harusi,unafika sebuleni unakutana na mtoto kaungua moto jikoni kisa wife alitoka nje mara moja kumwaga takataka, utamuacha mtoto ukaenda zako kwenye harusi halafu baadae ukirudi unamtuhumu wife kuwa mzembe na ndio chanzo cha mtoto kuungua???watu wengine wanafikiria kwa viuno nafikiri
Waliochemsha katika hili wameomba msamaha na si Vodacom


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

13 / 09 / 2011


YAH: KUOMBA RADHI KWA NDUGU ZETU WALIOPATWA NA MAAFA YA AJALI YA MELI HUKO ZANZIBAR .

Usiku wa kuamkia jumamosi ya tarehe 10 / 09 2011 tukio kubwa na la huzuni lilitokea huko Zanzibar ambapo wananchi wengi walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa wakati walipopatwa na ajali ya kuzama kwa MELI iliyokuwa ikitoka Unguja kuelekea Pemba . Kwa bahati mbaya siku hiyo ya Jumamosi taaasisi yetu ilikuwa inahitimisha Fainali za Taifa za Mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania 2011.

Kama waandaaji wa Mashindano haya na wenye Mamlaka kamili ya maamuzi juu ya ama kuendelea au la kuahirisha jambo hili, tulipatwa na mshituko mkubwa sana juu ya tukio hilo. Kamati yetu ilikaa na kutakafari katika tukio hilo kwa kuzingatia mambo yafuatayo:-
  • Taarifa kamili ya maafa haya tuliipata rasmi saa tisa na nusu mchana ( 9:30 ) siku ya jumamosi ambayo ilikuwa ni masaa machache kabla ya Fainali za Miss Tanzania kuanza katika ukumbi wa Mlimani City .

  • Wenzetu wa TFF waliendelea na mechi za ligi kuu ikiwemo ya Yanga na Ruvu Shooting.

  • Katika kumbi za starehe ikiwemo mabaa na burudani za muziki wa bendi na kumbi za disco ziliendelea kama kawaida.

  • Muda uliokuwa umebaki kuwakilisha jina la mshiriki wetu kwenye fainali za Miss World zilikuwa zimekwisha hivyo kulikuwa na hatari ya kupoteza nafasi hiyo.

  • Pia tamko rasmi la kusimamisha shughuli zote za burudani lilianza tarehe 11 septemba 2011 kuomboleza Kitaifa maafa hayo.
Hata hivyo kama waandaaji tulifanya shindano tukiwa katika maombolezo kwani kabla ya kuanza shindano Watu wote waliokuwepo ukumbini walisimama kimya kwa dakika moja na hata washiriki walipoingia kwenye jukwaa kwa mara ya kwanza walikuwa wamevaa vitambaa vyeusi katika mikono yao ikiashilia maombolezo. Hali hii imetupa mkanganyiko na kujikuta tukiendelea na mashindano kitu ambacho tunaona tumewakosea Watanzania wenzetu.

Kama Waandaaji tunapenda kusistiza kwamba tunawajibika kwa hayo yaliyotokea na si Taasisi yeyote au Kampuni yeyote na tunaomba ichukuliwe kama ni makosa ya kibinaadamu hasa ukizingatia mazingira magumu tuliyokuwa nayo kwa wakati huo na mkanganyiko wa matukio na taarifa za tatizo hilo.

KUOMBA RADHI

Hata hivyo shughuli hiyo inawezekana imewakwaza watu wengi na kwa sababu hiyo na pia hali halisi ya janga hilo na kwa niaba ya viongozi wenzangu na wadau wa shughuli zetu tunatoa tamko la dhati kwa Familia za ndugu wote walikumbwa na maafa haya, wale wote walionusurika katika ajali hii na Watanzania wote kwa ujumla, kwamba TUNAWAOMBA RADHI KWA MKANGANYIKO ULIOTUTOKEA HADI KUFIKIA HALI HII. Hatuna neno zaidi ya kusema na kusisitiza "TUNAOMBA RADHI"

Mwenyezi MUNGU aziweke roho za marehemu mahali pema peponi,

Amina,


Hashim Lundenga

Mkurugenzi
 
ukisoma kwa makini utaona sio kama alikuwa anataka kuomba radhi,taarifa hii imekaa kiutetezi zaidi na lundenga anajaribu ku-justify ni kwanini waliendelea shindano lao
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

13 / 09 / 2011


YAH: KUOMBA RADHI KWA NDUGU ZETU WALIOPATWA NA MAAFA YA AJALI YA MELI HUKO ZANZIBAR .


Usiku wa kuamkia jumamosi ya tarehe 10 / 09 2011 tukio kubwa na la huzuni lilitokea huko Zanzibar ambapo wananchi wengi walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa wakati walipopatwa na ajali ya kuzama kwa MELI iliyokuwa ikitoka Unguja kuelekea Pemba . Kwa bahati mbaya siku hiyo ya Jumamosi taaasisi yetu ilikuwa inahitimisha Fainali za Taifa za Mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania 2011.

Kama waandaaji wa Mashindano haya na wenye Mamlaka kamili ya maamuzi juu ya ama kuendelea au la kuahirisha jambo hili, tulipatwa na mshituko mkubwa sana juu ya tukio hilo. Kamati yetu ilikaa na kutakafari katika tukio hilo kwa kuzingatia mambo yafuatayo:-
  • Taarifa kamili ya maafa haya tuliipata rasmi saa tisa na nusu mchana ( 9:30 ) siku ya jumamosi ambayo ilikuwa ni masaa machache kabla ya Fainali za Miss Tanzania kuanza katika ukumbi wa Mlimani City .

  • Wenzetu wa TFF waliendelea na mechi za ligi kuu ikiwemo ya Yanga na Ruvu Shooting.

  • Katika kumbi za starehe ikiwemo mabaa na burudani za muziki wa bendi na kumbi za disco ziliendelea kama kawaida.

  • Muda uliokuwa umebaki kuwakilisha jina la mshiriki wetu kwenye fainali za Miss World zilikuwa zimekwisha hivyo kulikuwa na hatari ya kupoteza nafasi hiyo.

  • Pia tamko rasmi la kusimamisha shughuli zote za burudani lilianza tarehe 11 septemba 2011 kuomboleza Kitaifa maafa hayo.
Hata hivyo kama waandaaji tulifanya shindano tukiwa katika maombolezo kwani kabla ya kuanza shindano Watu wote waliokuwepo ukumbini walisimama kimya kwa dakika moja na hata washiriki walipoingia kwenye jukwaa kwa mara ya kwanza walikuwa wamevaa vitambaa vyeusi katika mikono yao ikiashilia maombolezo. Hali hii imetupa mkanganyiko na kujikuta tukiendelea na mashindano kitu ambacho tunaona tumewakosea Watanzania wenzetu.

Kama Waandaaji tunapenda kusistiza kwamba tunawajibika kwa hayo yaliyotokea na si Taasisi yeyote au Kampuni yeyote na tunaomba ichukuliwe kama ni makosa ya kibinaadamu hasa ukizingatia mazingira magumu tuliyokuwa nayo kwa wakati huo na mkanganyiko wa matukio na taarifa za tatizo hilo.

KUOMBA RADHI

Hata hivyo shughuli hiyo inawezekana imewakwaza watu wengi na kwa sababu hiyo na pia hali halisi ya janga hilo na kwa niaba ya viongozi wenzangu na wadau wa shughuli zetu tunatoa tamko la dhati kwa Familia za ndugu wote walikumbwa na maafa haya, wale wote walionusurika katika ajali hii na Watanzania wote kwa ujumla, kwamba TUNAWAOMBA RADHI KWA MKANGANYIKO ULIOTUTOKEA HADI KUFIKIA HALI HII. Hatuna neno zaidi ya kusema na kusisitiza “TUNAOMBA RADHI”

Mwenyezi MUNGU aziweke roho za marehemu mahali pema peponi,

Amina,


Hashim Lundenga

Mkurugenzi


danganya toto hiyo
 
Duuuhhhh, ndugu zangu hata na wewe Mwita25 zaidi ya kuwa vimombo vya kuangusha majengo kumbe hata na busara za kutoa kauli nyoofu nazo zimo???????????

Naoma kwa mfululizo huu wa leo tangu FaizlFoxy hadi wewe hapa, pengine tugemee suprises zaidi toka kwa Kishongo, Omr, na Malaria Sugu humu humu.

Lundega has lost legitimacy to organise Miss Tz event, I think he has to quit to protect his reputation. After all he has served this duty for quite some time now so he probably needs someone to spell him.
 
huyu mzee pumbafu sana..sasa kama bar ilikuwa wazi au tff sijui nini? Pumgwani sana hili zee
 
Ujinga sana, mnajidai kuomba radhi baada ya kustarehe!<br />
Wanapaswa kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu hawa<br />
ili iwe fundisho.
<br />
<br />
MIS TZ HAINA FAIDA YOYE KWA TAIFA
1.IMEJAA RUSHWA
2.WATOTO WALE WANAUZWA KWA MAPEDEJEE .WANAHATARISHA MAISHA YAO WENGI WA MAPEDEJEE WANA MATATIZO YA KIUFUNDI
3.WASHINDI WANAKUWA WA KIMAGUMASHI NA HAWANA VIWANGO VYA KIMATAIFA, HAWANA FAIDA KWA TAIFA ZAID YA KUANGUKIA PUA KILA WANAPOENDA MISS WORLD.WANGELISIMMAMISHA SIKU YA JMO
 
ONE OF MWAMVITA BEST FRIENDs on her FB WALL-''Really watanzania some of us are soooo freaking stupid......Gosh, Mpaka now huko ZNZ hawajajua hata who was the owner of ile meli iliyozama ila wamekazania tu kulaumu why miss tz took place. instead of kuelekeza hasira on why meli yenye uwezo wa kubeba watu 600 ilibeba watu 1000 wao wameng'ang'ana on who was having a jolly good time that day,how the **** is that going to make things better? meli imeondoka bandarini''inaelemea one side kwa mizigo mingi,why not deal na watu waliofanya uzembe.instead stupid politicians wa chadema wamepata opportunity ya ku attack CCM, and waznz wamepata opportunity ya ku question muungano na bara.how unfair is that? DEAL WITH THE REAL ISSUES JAMANI,,MNGEPIGIA KELELE PUBLICLY NA KUDEMAND KUJUA MMILIKI WA MELI ILE MTAISAIDIA ZAIDI ZNZ na sio kuuliza why miss tz went down.septembe . r 11th ilitokea marekani na oscars hazikuwa cancelled ila watz bila majungu hamuoni raha.stupid... ANAENDELEA KUTOA MSISITIZO-''KAMA UNA ANY OPINION YA KISHAMBA YA KUBLAME VODACOM OR MISS TZ DONT COMMENT ON MY STATUS, IF U DONT AGREE WITH WHAT I SAID FEEL FREE TO REMOVE ME FROM YOUR FRIENDS'S LIST....''SASA SIJUI MTU KAMA HUYU ATAMSHAURI NINI MWAMVITA KAMA UUNGWANA KWAKE NI KAULI CHAFU.
Hayo mengine yote sitochangia isipokuwa hilo kwenye nyekundu. Bila ya kuongeza langu ninakuomba ujihabarishe zaidi kuhusu tarehe na mwezi ambapo sherehe za Oscars zinafanyika.
 
Back
Top Bottom