Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

Tatizo la Law School ni mchanganyiko wa factors nyingi zinazoingiliana. Si busara kuchukua sababu moja au mbili tu na kuhitimisha zipo sababu za kimfumo, mitaala ya LST na vyuo vikuu kutoendana, sababu za kijamii ikiwemo rushwa za ngono na nyinginezo, mfumo wa elimu duni kwa ujumla nchini, uwezo wa walimu, ubabe wa kielimu(superiority & negative mindset) kwa walimu na manyanyaso, sababu za kiuchumi, uhaba wa vitendea kazi kwa elimu ya vitendo, mkazo wa nadharia na kuota nafas kido mafunzo ya vitendo, maandalizi hafifu ya wanafunzi kwenye vipindi na psychological feeling kuwa chuo hicho ni vigumu kufaulu hii ni kwa walimu na wanafunzi ndicho kinachozunguka akilini lazima wafelishwe. Teaching methodology and approach haimwandai mwanafunzi na masuala ya kiutawala yakiwemo LST kusajiri wote wanaoomba bila kufanya vetting na upembuzi wa kutosha kuchukua wenye uwezo tu badal

Wanafunzi someni acheni kuingiza siasa.Siasa ikiingizwa hapo matokeo yake tutapata wanasheria watakaokuja kupitisha mikataba ya kuumiza nchi kama ile ya gesi ya mtwara.walimu washikilie hapohapo hakuna cha tume uchwara wala nini.Tumeshuhudia mikataba mingi nchini hii imekuwa ya kipuuzi sana kumbe sababu ni uwezo mdogo wa wanaopata nafasi toka chuoni
Mapesa yamejaa sikia: Hii inapaswa kuwa 100% practical legal training na siyo 50% theoretical (semester 1) kisha 50% legal practical training na mwisho kufanya mtihani wa mwisho wa Theory Paper!! Waliofeli wamefele mtihani wa mwisho uliobase kwenye theory!!

Suluhisho: Semister zote mbili zihusishe field placement maeneo mbali mbali ambako sheria hufanya kazi kwa vitendo kama mahakamani, makampuni ya mawakili, ofisi za mawakili wa serikali, takukuru nk Kuwe na rotations huko na assessment ifanyikie huko na hiyo assessment ifanywe na mawakili na mahakimu walioko huko field na si walimu wa chuo ambao hawana uzoefu wowote wa vitendo wao ni nadharia tu.
 
Prof Costa anawajua wanafunzi wa chuo chake Uwezo wao.

Ukiwauliza wakuu wa chuo,wangependa nyomi Kutoka vyuo vyao wasikwame mbele ya safari bila kujalisha wameiva au la.
 
Kama utaupuuza ukweli kwamba wanafunzi ndiyo wenye shida basi mleta mada una wivu ama chuki binafsi na walimu wa shule ya sheria.

Wanafunzi wanachangia kufeli kwao kwa 75+%. Muda mwingi wanadanga, wanalewa, wanabet, wanawaza ukahaba, n.k.

Hawawezi kuandika sentensi nzuri za kiswahili na hata kiingereza. Unapata wapi ujasiri wa kuwalaumu walimu pekee?
Nafikiri itafika wakati ukweli usemwe. mimi kiasi nakubaliana na walimu wa LST kuwa huenda kushindwa kunachangiwa na kuwachukuwa wanafunzi wa ushindi wa wa chini, lakini haiwezekani wanafunzi wote zaidi ya mia sita walioshindwa walipata ushindi wa D form six. Sanasaana wanafunzi wa ushindi wa D hawafiki 25%. LST ingetaka kutumia ushindi wa chini kama kigezo, basi wangetuambia katika hao zaidi ya 600 ni asili mia ngapi walikuwa na ushindi wa D, hapo mimi ningewaamini.

Nimesikia wakisema kuwa hao wanafunzi hawajui hata kunyoosha senteso. Bila shaka hapa wanaongelea kunyoosha sentoso ya kiingereza. Lakini LST inatakiwa kukumbuka kuwa mahakama zetu ziko katika kuondokana na uenedeshaji wa kesi na uandikaji wa hukumu kwa Kingereza kwenda Kiswahili. Je, LST imefikiria labda kufundisha na kutoa mitihani kwa Kiswahili? Kama wahusika watakuwa wanatumia Kiswahili kuendesha shughuli za kimahakama ikiwa ni pamoja na utetezi, usikiliwaji wa kesi, kwa nini wahangaike kefundisha na kutoa mitihani kwa Kingereza.

Najuwa kutumia Kiswahili kunaweza kupunguza fursa zetu kutumikia mashirika ya kimaitaifa, lakini wapo wenye uwezo wa Kingerezana hao watatuwakilisha kama nchi zingine zisizotumia Kingereza na Kifaransa zinavyofanya
 
Nimesikia wakisema kuwa hao wanafunzi hawajui hata kunyoosha senteso. Bila shaka hapa wanaongelea kunyoosha sentoso ya kiingereza. Lakini LST inatakiwa kukumbuka kuwa mahakama zetu ziko katika kuondokana na uenedeshaji wa kesi na uandikaji wa hukumu kwa Kingereza kwenda Kiswahili. Je, LST imefikiria labda kufundisha na kutoa mitihani kwa Kiswahili? Kama wahusika watakuwa wanatumia Kiswahili kuendesha shughuli za kimahakama ikiwa ni pamoja na utetezi, usikiliwaji wa kesi, kwa nini wahangaike kefundisha na kutoa mitihani kwa Kingereza.
Kiswahili ni kigumu kuliko kiingereza. Angalia hata ktk mada za humu kwenye JF zinazoandikwa kwa kiswahili utaona makosa makubwa Sana.

Neno "ndiyo" wanaandika "ndio"
Neno "hebu" wanaandika "embu"
Neno "yaliyomo" wanaandika "yaliomo"

Hii ni baadhi tu ya mifano ya makosa yanayofanywa wakati wa kuandika ktk kiswahili.
 
Tatizo la Law School si dogo ambalo ati kila Tom, Dick au Harry anaweza kuwa na ufumbuzi au ushauri.

Kwa sampuli hii:

1. Profesa Cyriacus Binamungu (Mzumbe): anasema kuna shida kwa walimu katika taasisi hiyo (LST).

“Wanafunzi wanaandaliwa vizuri (vyuoni) isipokuwa kutakuwa na shida LST, walimu hawazingatii ufundishaji, wanafikiria mishahara, akipokea hajali mwanafunzi kaelewa au la.”

2. Profesa Costa Mahalu, (VC Saut): anasema ni aibu kwa taasisi hiyo kutokana na matokeo hayo, pia inapaswa ijitafakari.

“Haiwezekani wanaofeli mtihani wa uwakili pale LST hawana ujuzi na maarifa katika masomo yao kutoka vyuo walivyosoma. Hapana! Kuna tatizo na lazima utafutwe ufumbuzi,”

Profesa Mahalu anasema matokeo mabaya yanasababishwa na makundi matatu ya walimu wanaowafundisha wanafunzi hao wa uwakili.

(a) Matatizo ya uwezo,
(b) wanaopenda kuogopwa na wanafunzi,
(c) wale wasiotaka mafanikio ya wengine, ambalo ndiyo lililo hatari zaidi.

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

Profesa Mahalu anashauri kulindwa msingi wa kuanzishwa kwa LST ambao ni kutoa elimu kwa vitendo kutoka kwa majaji, mahakimu na mawakili wanaoshughulika na mashauri kila siku mahakamani.

“Maprofesa waliobobea katika nadharia wasipelekwe kuwafundisha wanafunzi pale LST kwa sababu kufanya hivyo ni kukiuka lengo la msingi la kuanzishwa kwa chuo hicho.”

Kabla ya taasisi hiyo, anasema Mahalu mawakili walipata maarifa kwa miezi tisa kutoka kwa mawakili na mahakimu waliopo kazini.

“Taifa lilipata wanasheria na mawakili nguli, nikiwemo mimi, Jaji mkuu mstaafu, Othman Chande na Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda mwaka 1974. Wahadhiri wa LST wajitafakari kwa matokeo haya.”
___________

Watu kama hawa walipaswa kuwamo kwenye tume ya Dr. Ndumbaro.

LST kuna matatizo na walimu yasiyokuwa ya kufumbiwa macho. Fika LST kuutambua ukwasi wa walimu hawa wenye kujiita 'fulani the don.'

Kwa hakika muda wa kuyatanzua makando kando yao ni sasa.

Wameyakoroga wenyewe, hawana budi kuyanywa.

Source:

Profesa Shivji asema tatizo ni mfumo ufaulu mtihani Uanasheria
Hivi ni 'Law School of Tanganyika' au 'Law School of Tanzania'?.
Nadhani tuanzie hapo.
 
Hawa maoni Yao unayasikiliza lkn sion kuyachukua Kama ndo majibu Sahihi, kuna WAtu wanamakasiriko na WAtu wafanyao Kazi LST pia

Ila watu wenye makasiriko na wanafunzi hawapo?

CV ya Prof Mahalu haikuwekwa pale kwa ajali. Huyu anaongea anachokijua.

CV yako Iko wapi ewe Tom, Dick au Harry?

Wewe si kama mrusi wa Buza tu mkuu?
 
Haipo njia nyingine ya kutambua weledi wa mtu isiyoanzia kwenye CV ikafuatiwa na kauli zake na matendo yake.

NIsiache kukwambia Prof Mahalu amemaliza kila kitu kwenye kadhia hii katika namna rahisi na sahihi kwa Kila mtu
Kwani gwiji Pascal Mayalla maoni yake kwenye kadhia hii ni gani?
Mkuu brazaj, kwanza asante kwa hii!.
Pili mimi namkubali sana Prof. Rick Costa Mahalu, toka kitambo!, wakati Mahalu akiwa balozi wetu Italy, mimi nilikuwa Italy nikitafuta maisha!. Maisha yakanigombea nikapata msala fulani, kama sio Prof. Mahalu na ofisa balozi fulani wa ubalozi wetu Italy, Mr. Nchemwa, sijui ningekuwa wapi!.

Prof. Mahalu abarikiwe sana!.
P
 
Ila watu wenye makasiriko na wanafunzi hawapo?

CV ya Prof Mahalu haikuwekwa pale kwa ajali. Huyu anaongea anachokijua.

CV yako Iko wapi ewe Tom, Dick au Harry?

Wewe si kama mrusi wa Buza tu mkuu Naona Uko na supp mwaka wa tano sasa Una makasiriko hta Kwenye comment?? Tuwasikilize WAtu kisa Wana CV kubwa?utaendelea kussup hadi ufikishe Miaka kumi.. hao hao wangekuwa ni sehemu ya LST wasingebadirish chochote au hta kukusaidia ndgu. That's why we need open discussion ila sio kukariri WAtu kisa tu ni wanasheria wa Muda mrefu,?? Na inshu Kama ni CV tuwasikilize hao ambao wanasema Wanafunzi wa siku hiz hamjibiidishi darasani? Au hao wanaowapa Marks sifuri.
 
9 October 2022
Wenzetu wako mbali sana kuhakikisha mambo yanakuwa ya viwango vinavyokybalika toka chini kabisa

National Rounds of the 2022 Schools Moot Court Competition Programme currently underway at the University of Pretoria





Source : Department of Basic Education ZA


13 October 2022

Dar es Salaam, Tanzania

HOJA MEZANI II Wadau wa sheria na ugumu wa shule ya sheria kwa vitendo


Source : azam tv
 
Kwenye maandiahi yako hapa ndiyo unathibitisha uhovyo wa wanafunzi Sasa.

Mwanafunzi wa chuo kikuu anashindwaje kujisimamia Hadi Prof amtake kimapenzi bila ya ridhaa yake na atoe uroda? Huoni kuwa tatizo linaanzia kwa wanafunzi wenyewe?

Mkuu wanafunzi ndiyo hawasomi hivyo wanajiingiza kwenye kununua mitihani kwa kutumia miili yao. Maprofesa wanachofanya ni kutumia tu huo mwanya kama fursa.

Mwanafunzi wa chuo kikuu .mama mtu mzima (miaka 20+ atoe mzigo bila ya ridhaa yake na akae kimya?) Basi wana shida kwenye vichwa vyao.
WENDA umesoma shule za china , Kama sivyo basi wewe sio mtu wakujichanganya, we sema Mie mwanafunzi kumbe wakuta Mie boss wako kila siku twapishana kwenye korido,

Lakini kuwa mwanafunzi sikatai maana elim haina mwisho,

Kaa na jamii ,piga story na jamii utajua mengi Kama sio kujifunza mengi,
 
Nimesikia wakisema kuwa hao wanafunzi hawajui hata kunyoosha senteso. Bila shaka hapa wanaongelea kunyoosha sentoso ya kiingereza. Lakini LST inatakiwa kukumbuka kuwa mahakama zetu ziko katika kuondokana na uenedeshaji wa kesi na uandikaji wa hukumu kwa Kingereza kwenda Kiswahili. Je, LST imefikiria labda kufundisha na kutoa mitihani kwa Kiswahili? Kama wahusika watakuwa wanatumia Kiswahili kuendesha shughuli za kimahakama ikiwa ni pamoja na utetezi, usikiliwaji wa kesi, kwa nini wahangaike kefundisha na kutoa mitihani kwa Kingereza.

Najuwa kutumia Kiswahili kunaweza kupunguza fursa zetu kutumikia mashirika ya kimaitaifa, lakini wapo wenye uwezo wa Kingerezana hao watatuwakilisha kama nchi zingine zisizotumia Kingereza na Kifaransa zinavyofanya

Unaongelea kiingereza? Aliyekuwa waziri wa elimu uliwahi kumsikia akikisokota? Vipi mwendazake hukuwahi kumsikia pia?

Kina Tom, Dick na Harry kukaa kwa kutulia si chaguo baya.
 
-kwa taarifa yako ukisoma hiyo taarifa ya mwqnanchi utagundua kuwa, Prof shivji ameunga mkono hoja za LST,ambazo zilitolewa na Prof Lukumay, kwamba wanafunzi wa law school wana uwezo mdogo kutokana na wengi wao kuwa "half cooked" tokea kwenye degree ya kwanza
- Prof Mahalu, ulitarajia atakubali kwamba SAUT LL.B hawana uwezo?, halafu aliwahi kuwa mkuu wa chuo cha bagamoyo UoB ambacho kilifungiwa na TCU kwa matatizo ya ubora.
-Shivji amesema wanafunzi wana uwezo mdogo sana,
Acheni kumnukuu Shivji out of context:

Prof. Shivji na maoni yake kuhusu kadhia ya Law School

Shivji yuko broader. Education system in Tanzania has collapsed. Humo wapo wote mpaka primary.

Usimuwekee Shivji maneno mdomoni.

Rejea mada kutambua alichosema Mahalu:

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

"Wapenda ngono na wachawi siyo kwenu tu, hata kwetu wapo." --SAM.
 
Wasomi watapeliwa kirahisi, mwanafunzi wa chuo cha elimu asimulia kadhia

NINI KINAFANYA JAMII KUBWA TANZANIA RAHISI KUWAHADAA

Ni elimu isiyo ruhusu wasomi kuhoji



Source: SimuliziNaSauti
 
Acheni kumnukuu Shivji out of context:

Prof. Shivji na maoni yake kuhusu kadhia ya Law School

Shivji yuko broader. Education system in Tanzania has collapsed. Humo wapo wote mpaka primary.

Usimuwekee Shivji maneno mdomoni.

Rejea mada kutambua alichosema Mahalu:

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

"Wapenda ngono na wachawi siyo kwenu tu, hata kwetu wapo." --SAM.
-mkuu hujasoma hiyo habari ukaelewa kwa ufasaha mbona ni lugha rahisi tu sio kama maswali ya LST
-Prof shivji ameunga mkono kikichosemwa na LST kupitia prof lukumay, kwamba tatizo ni vyuo vya sheria LL.B Kwamba hawaandaliwi vizuri, matokeo yake LST wanapokea half cooked students
-tafsiri yake ni kwamba Prof shivji amekubali kwamba tatizo ni vyuo vya LL.B
 
-mkuu hujasoma hiyo habari ukaelewa kwa ufasaha mbona ni lugha rahisi tu sio kama maswali ya LST
-Prof shivji ameunga mkono kikichosemwa na LST kupitia prof lukumay, kwamba tatizo ni vyuo vya sheria LL.B Kwamba hawaandaliwi vizuri, matokeo yake LST wanapokea half cooked students
-tafsiri yake ni kwamba Prof shivji amekubali kwamba tatizo ni vyuo vya LL.B
-mkuu hujasoma hiyo habari ukaelewa kwa ufasaha mbona ni lugha rahisi tu sio kama maswali ya LST
-Prof shivji ameunga mkono kikichosemwa na LST kupitia prof lukumay, kwamba tatizo ni vyuo vya sheria LL.B Kwamba hawaandaliwi vizuri, matokeo yake LST wanapokea half cooked students
-tafsiri yake ni kwamba Prof shivji amekubali kwamba tatizo ni vyuo vya LL.B

Hujamwelewa Shivji. Kumwelewa Shivji si kwa kila Tom.

Shivji ana matatizo na watanzania wote ukiwamo wewe akiambatanisha matatizo hayo na ku collapse kwa educational system.

Matokeo yake ule u arsenal na Man U na umuhimu wa u. Yanga na Simba dhidi ya yenye maslahi zaidi ya nchi.
 
Kwa ujumla UDSM ni chuo cha kidikteta na udikteta huu unasababishwa na ukabila uliokithiri.

Kuna kabila hapo UDSM huwa hawafeli hata kama ni kialaza.

Kingine ngono. Kuna digrii nyingi za mabinti ni za ngono.

Unakuta binti anabakizwa kuwa tutorial asistant na GPA kubwa ila kichwani boga. Anabebwabebwa tu..

Hebu kila chuo kinachofundizha sheria kiwe na law school hapohapo chuoni.

Wana mfumo wa ajabu. Kila chuo kinapaswa kuwa na law school yake. Na jukumu la law school sio kumuandaa mtu kufaulu mtihani wa uwakili. Bar exam has nothing to do with law school. Sio kila law student anataka kufanya bar exam!
 
Wana mfumo wa ajabu. Kila chuo kinapaswa kuwa na law school yake. Na jukumu la law school sio kumuandaa mtu kufaulu mtihani wa uwakili. Bar exam has nothing to do with law school. Sio kila law student anataka kufanya bar exam!
before haijaja law school kulikuwa ba Bar exams
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom