Kada mashuhuri wa CCM ajiunga CHADEMA

Akabidhiwe kwenye uongozi wa Jimbo kwa uchunguzi haraka, nina imani kubwa sana na uongozi wa chini wa Chama kuliko makao makuu, makao makuu kumekuwa na bureaucracy ndefu sana katika kuwachukulia wanachama wajinga wajinga hatua za kinidhamu.

Hapa umesema ukweli mkuu,makao makuu wanajivuta sana kutoa maamuzi.
 
mimi sio mwanachama wa CCM ila nalaan na kupinga wanaomuita Dkt Bujari kada wa CCM. na ntaweka sababu
1) huyu jamaa ameanza kufahamika kwenye siasa za Ngara baada ya kutangaza nia ya kugombea ubunge hiyo inaleta picha kwamba alichofuata CCCM ni UBUNGE tu nashukuru watu wa Ngara tulimuelewa
2) chaguzi za ndan ya chama jamaa hajawahi kuchangia chochote na uchaguzi uliopita jamaa alipoombwa mchango alitoa maneno ya kejeli
3) ni mkabila, jamaa alianzisha DIVIDE AND RULE kwa kutaka kutugawa wana Ngara. Hapa Mkazi wa Ngara ataelewa tofauti kdogo iliyopo baina ya Bugufi na Bushubi jamaa alieendeleza kampeni za tumchague WAKWETU
4) baada tu yakupigwa chini kwenye uchaguzi wa ndani ya chama magari yake yalianza kupeperusha bendera za CHADEMA nalazimka kuamini hata huko ndicho anachofuata
kwa taarifa zaid nasikia amekuwa mchungaji na anampango wa kuanzisha kanisa lake pale Rulenge,
Kweli CDM mmepata jembe


Hiyo siasa ya maji taka
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.

Safari ya akhera hiyo inamuadiya masikini Kada
 
Cdm isikimbilie kumpa uongozi kwanza, apewe majukumu ya kuvua watu magamba huko ngara na kagera kiujumla!
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.
Na bado wako wengi wanahamia!
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.

Are u screening these cadres?? we dnt wanna hear u screaming back.. coz even Shibuda was pronounced this much..

However, we suppose to know his personal initiatives and capabilities in building CDM, nt just acceptng, simply ametoka CCM..
 
wapigania tumbo wako chadema eg. Babu Slaa, Mbowe, lEMA, Sugu na jamii ya akina Msigwa

WaTZ wanawafahamu wezi wa rasilimali zao,waliogawana na kupeana viwanda vyetu,ardhi yetu,nyumba zetu za serikali kwa mgongo wa uwekezaji na ubinafsishaji! utakuwa unapoteza muda wako kujaribu kuwapotosha watu walionyang'anywa ardhi/maeneo yao,wanaodhurumiwa haki yao,wahanga wa mabomu ya policcm,wanaokosa elimu bora,walimu wanaotaabika kwa malipo kiduchu,wakulima wanaouza mazao yao kwa bei sawa na kutupa na wanaokopwa mazao yao kama wale wa korosho,vijana waliokosa mikopo huku watoto wa vigogo wakisoma bure n.k! JITAMBUE,UWE MZALENDO KWA KUJIUNGE KWENYE CHAMA CHA UKOMBOZI KWA MSTAKABALI MZURI WA WATOTO WAKO NA WATZ WENZAKO.
 
Karibu CDM kamanda lkn huku ni kazi tu! hivyo umaarufu wako ndani ya CDM siyo chochote bali utathaminika ukiwa msafi na kuchapakazi.
 
Sera ipi hiyo ambayo kaiona sasa na sio kabla?au ana mtambo wa kupikia gongonini?maana hiki ndicho kipya kwa sasa.
nahisi mwenye mtambo uta kuwa wewe usiye ziona sera za cdm unaziona za kubaka watu kwenye operation zaccm tu!
 
Huyu Dr Bujari tumwangalie kwanza ametafuta ubunge kupitia CCM akapigwa chini na kiukweli kupitia ccm hawezi kupata ubunge anachofanya saiv ni kama Gashaza alizunguka badae akaona kuludi ccm mbali nakwamba ni mtu anaependwa sana Ngara binafsi namkubali sasa Dr Bujali ajiandae kupambana na Dr Sebuyoya ila tatzo la wilaya ya Ngara Bado sana watu wengine ukienda Busubi wanajua nyerere ndo raisi
 
nahisi mwenye mtambo uta kuwa wewe usiye ziona sera za cdm unaziona za kubaka watu kwenye operation zaccm tu!

Ingekuwa ni sera zingine si angejiunga muda mrefu uliopita maana zilikuwepo toka 2010,kilicho kipya kwa mwezi huu ni hiki cha gongo,ndio maana nashawishika kuwa labda anaposema sera anamaanisha "gongo".
 
Kwani yeye kaomba uongozi ama ndo kujishtukia? CDM kama chama kinahitaji viongozi na kinahitaji wapiga kura pia na hata mchakato wa kumpa mtu uongozi sidhani kama ni suala la bebabeba tu,ilmradi katiba ipo mimi naamini hata anayetaka kuwa kiongozi atatakiwa kukidhi vigezo kwahiyo nyinyi endeleeni kukaribisha watu mambo ya uongozi ni baadae mda ukifika.
 
Watanzania tuache lawama na tusiwe wavivu wa kufikir.Tanzania ni nchi ya kidemokrasia na hvyo mtu ana haki ya kujiunga chama chochote wakati wowote anaoona unafaa kwake.kwann mnamhisia sababu za kujiunga kwake???halafu hakuna kitu kicchokuwa na changamoto...mbona hamsemi mazur ya CCM mnayaona mabaya tuuuuuu???Achen ushabiki usiyo na tija bwanaaa
 
Back
Top Bottom