Kada mashuhuri wa CCM ajiunga CHADEMA

huyo mroho wa madaraka.. Pokeeni zigo hilo lenye wivu wa madaraka.
Ila mwisho wa siku atarudi CCM.

Gogo wivu,
fanya haraka uje huku kabla majimbo yoote hayajaisha. Huyu si mroho wa madaraka ni mtu aliyeona mbali. 2015 sio mbali, siku hazigandi bali zinayeyuka tu. Utastukia kura hiyooo nawe utakuwa upande wa wale walioambiwa na M/kiti wao kuwa wajiandae kisaikolojia. Wale ambao M/kiti wao aliwaombea huruma kuwa CDM ikichukua madaraka, wawasamehe makosa yao bure ka Mzee Madiba. Tamu hiyo.
Namuunga mkono M/kiti wako, nami namwomba Mh. Mbowe na Dr. Slaa wasirudishe baya kwa baya. Kariib Kamanda umevua gamba vaa Gwanda. Kwetu pazuuuri, nimesha pakumbuka...
 
Yawezekana mfululizo wa habari hizi ukawa wa kufurahisha na kushangiliwa leo. Lakini mbele kidogo uteuzi ndani ya vyama utakapoanza, furaha yote itageuka kuwa majonzi! Uhamiaji wa kasi mida hii ulipaswa kuchukuliwa kama ishara kwa Watendaji wa vyama vya Upinzani kuandaa mfumo bora amabo hautaleta migongano na mitafaruku wakati wa kupitisha wagombea ndani ya chama. Badala yake wanachama, wafuasi, viongozi na watazamaji sote tunashangilia kwa kuangalia mbele badala ya kutazama mbali!

Naomba kurejea huu mchango wangu wa siku za nyuma kwa Bw. Nyami2010:

......
Nina hakika mwaka 2015 ndani ya vyama vya upinzani hakutakuwa na uteuzi kama tulivyozoea huko nyuma bali kutakuwa na uchaguzi. Utakuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana katika baadhi ya majimbo. Hata baadhi ya walio wabunge wa upinzania kwa sasa, 2015 watapingwa ndani ya vyama vyao.

Nimekutana na watu mbalimbali katika nyakati na mazungumzo tofauti tofauti wakiwa tayari wanajitambulisha kama Wabunge wa Majimbo husika kwa kipindi kijacho 2015-2020! Na mara nyingi kama si mara zote hawa "wabunge" wanajinasibu kuupata Ubunge kupitia chama kile kile. Hata wakati mwingine nakutana na watu zaidi ya watatu kwa nyakati tofauti na wote wanajitambulisha ni Wabunge watarajiwa wa eneo lieliele kupitia chama kile kile kwa kipindi kilekile 2015-2020! Unaweza kubashiri toka leo hicho chama kitakuwa na hali ngumu kiasi gani muda ukifika wa kuwapata wagombea.

Rai yangu kwa “wabunge” watarajiwa wanaotangaza nia kuanzia sasa wafikirie upya juu njia sahihi ya kujitambulisha. Wasijiwekee akiba ya msongo pale watakapojikuta safari yao haikuvuka hata mzingiti wa mlango! Nadhani wengi hawako sahihi pale wanapojitangaza kama vile tayari wana tiketi za kuwakilisha vyama vyao. Badala ya kusema “Nitagombea Ubunge XXX 2015 kwa tiketi ya YYY” Labda watakuwa sahihi zaidi wakisema “Nitaomba ridhaa ya chama YYY kugombe Ubunge wa Jimbo XXX mwaka 2015”. Ukilijua hili na kuliweka akilini, itakusaidia pia kujua kwamba vita yako haianzii hatua ya pili bali hatua ya kwanza. Itakupa fursa ya kujijenga mapema na kuweka mkakati wa kushinda kwanza hatua ya awali.

Vinginevyo nawatakia maandalizi mema.
 
Jamaa yupo fit! Nafikiri hii ni kazi nzuri ya mwenezi KAKOKO! bila kumsahau kamanda TALL pale Victoria.
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.

Mapandikizi ya Mbowe hayo! Ameshakatiwa mabaki ya ruzuku, amuongeze nguvu kanda ya magharibi. Ngoja hela iishe utasikia tu.
 
Na bado,utaona mwakani itakavyokuwa.Walikuwa wanasubiri Chadema kusambaratika 2013 lakini mwaka umeisha bila mafanikio huku wakina Nchemba wakiwa wanakaribiwa na tuhuma za kulipua mabomu pale soweto
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.

Njaa inamsumbua. Kwa hiyo hizo kero mbalimbali zinaweza kutatuliwa na Chadema? Toka lini Chadema ikatatua matatizo? Chadema ipo kuleta matatizo sio kuyatatua.
 
huyo mroho wa madaraka.. Pokeeni zigo hilo lenye wivu wa madaraka.
Ila mwisho wa siku atarudi CCM.

Amekimbia kumtoa kafara mwanae kwa lazima kama wanavyofanyiwa wenzake na Mwigulu kama alivyowafanyia wale wa Arusha.
 
Akienda Chadema nako atakutana na haya:
-Pesa ya Sabodo zimepigwa meno
-Wajanja wamekiuzia chama magari mabovu
-Wamejikopesha ruzuku za chama
-Millioni 140 alizokopa Dr. Slaa ziko wapi?
-Chama hakina ofisi ya maana
-Uchaguzi haufanyiki
-Ubaguzi umetapakaa kote.
-Kuna chadema chumbani na chadema sebuleni
 
Njaa inamsumbua. Kwa hiyo hizo kero mbalimbali zinaweza kutatuliwa na Chadema? Toka lini Chadema ikatatua matatizo? Chadema ipo kuleta matatizo sio kuyatatua.

Hahahaha maneno ya mkosaji haya, mpaka mwishoni mwa 2014 ccm mtabaki nyie na wake zenu tu, watanzania watakuwa tayari kwenda kwa wajanja chadema.
 
Hahahaha maneno ya mkosaji haya, mpaka mwishoni mwa 2014 ccm mtabaki nyie na wake zenu tu, watanzania watakuwa tayari kwenda kwa wajanja chadema.

Wake zao ndo tunaanza nao mkuu, watabaki wao tu na pesa walizotuibia.
 
Kada wa CCM jimbo la Ngara, Dr Peter Bujari ametangaza uamuzi wa kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA hivi punde.

Amewaambia wanahabari kuwa CCM imeshindwa kuondoa kero mbalimbali.

Pia amesema amejiunga na CHADEMA kutokana na sera na Uongozi thabiti. na usioyumba wa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Source:Mwananchi Breaking News.

Amejitambua
 
Back
Top Bottom