Kabla ya kuandamana ni vyema viongozi wetu wakasema walikubaliana nini na Mh Rais?Ni wakati muafaka

Br kinachoendelea n upumbavu na ushenz wa ukawa na ccm tunaposema tuandamane tunakua katka mfumo gan na kwa umoja up ?

Hakuna sababu za msingi za kuandamana ni vyema usiwategemee wana siasa kwa lolote lile!
 
Viongozi wa chadema hawana elimu

Sio kwamba hawana Elimu bali wamesha wageuza wananchi kama wajinga vile wanajua wakisema kuandamana basi wananchi wana fata!
 
Ruttashobolwa;

Hapa ishu siyo kama mimi nataka kuandamana au vipi bali umeleta hoja na tunajadiliana. Ndiyo maana nasema sidhani kama kuna side yoyote tunaoweza kuiamini si Ikulu/CCM, TCD au UKAWA. Lakini kwa kutumia akili yako na mtiririko wa mambo jinsi yanavyokwenda you can simply make decisions on this issue of Katiba! Ndiyo maana nikasema upande utakaoheshimu maoni ya wananchi yaliyokusanywa kitaalamu na kwa mujibu wa sheria na kuwa compresssed kwa mtindo wa Rasimu ya pili ya Katiba chini ya Tume ya Rais iliyoongozwa na Jaji Warioba kiukweli ndiyo upande unaopaswa kuaminiwa na kupewa support na wananchi kwa namna yoyote ile iwe kwa kuandamana au kwa kupaza tu sauti zetu na kwa njia zingine zozote zinazokubalika!!.

BTW, unajicontradict sana kwa namna ulivyoleta uzi wako na na namna unavyo react toka katika mawazo na comments za wachangiaji mbalimbali. Hebu niambie hiyo video ya mazungumzo unayoiomba ni ya nini sasa kama una uhakika kuwa walikubali BMK liendelee hadi tarehe 4/10? Au unalazimisha tu tukuamini wewe na wakati huohuo unaomba video kuonesha kuwa hata wewe hujui lolote kuhusu hayo mazungumzo ila tu kwa sababu Cheyo na TCD amegusa hisia zenu na mnachokitaka na wakati huohuo UKAWA wakatokea kupingana naye? Narudia tena kukuhakikishia kuwa;

Hakuna video au uthibibitisho wowote halisi wa mazungumzo unaoweza kutolewa na Ikulu/CCM yenu,wewe au TCD kwa maana ya Mwenyekiti wake Bwana Mapesa Cheyo kwa sababu moja tu hakuna nia thabiti ya kuukwamua mchakato wa kuandika katiba hii bali kilicho mbele zaidi ya IKULU/CCM ni maslahi ya kisiasa zaidi ambayo yamo katika mchakato huu, kosa dogo tu unamalizwa na opponent kisiasa wako asubuhi tu,wewe na CCM yako mnalijua hili,
that's why you are fighting day and night.........but I am very sorry to tell you that you are losing the battle!.


Na rafiki,nikuambie tu huu mchezo wa kisiasa unaochezwa na Ikulu/CCM kwa msaada wa John Cheyo,Mrema na Fahm Dovutwa Nassoro kwa kivuli cha TCD kila mwenye akili timamu ameshaung'amua!!.. Na I am sory too kukuambia kuwa hata wewe unachokifanya katika social networks kama hii ni kama kuendelea kukolezea ulaghai wa CCM tu. Na kama si mchezo wa kisiasa na kweli hayo mazungumzo chini ya mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi yalikuwa na lengo jema, kwa nini yasingekuwa ya wazi na vyombo vya habari kuruhusiwa kuhudhuria na kuripoti kitakachojiri kuliko ilivyo sasa ambapo tuna lazimishwa kuamini au kutoamini chochote miongoni mwa makundi hasimu ya kisiasa siyoaminiana ya CCM/Ikulu vs TCD vs UKAWA?

Si katiba ni mali ya wananchi, sasa kwa nini mambo yawekwe katika hali ya kifichoficho na kipropaganda zaidi? Kwa sbb hata wewe unachokifanya ni kuendeleza propaganda zilezile chafu za CCM!!..But the fact remains that; ishu hii ya katiba mpya ndiyo itakayoinyonga na kuitupilia mbali CCM tunapoelekea katika uchaguzi wa seriakali za mitaa na uchaguzi mkuu 2015, kama unabisha tunza huu uzi halafu tukumbushane mwaka kesho kuanzia mwezi november!!

Ndiyo maana nakuuliza mnapata wapi ujasiri wa kutuombea Ikulu iweke mazungumzo hayo hadharani halafu yaaminike?
Sababu ya kuiomba hiyo video ni kuondoa unafiki maana with wengine wamesha anza kuamini Ukawa hawakukubali bunge liendelee hadi October 4!
Na swala la maongezi kuwa ya kificho liliombwa na viongozi wa UKAWA waulize!
Ina maana na wewe huamini kama walikubali katiba iliyopo ifanyiwe marekebisho?huamini kuwa walikubali swala la katiba litaendelea baada ya uchaguzi?

Swala la kusema sijui maoni ya wananchi yanatupwa ni inayo jadiliwa si rasimu ya warioba huu ni uongo labda mtwambie zile sura. mbili walizojadili UKAWA zilikuwa kwenye rasimu gani?

Kumbuka bunge limepewa mamlaka ya kubadilisha,kuongeza,kurekebisha chochote kwenye Rasimu na sheria!

Basi tunaweza kukubaliana kuwa hakuna mwenye mamlaka ya kusitisha bunge! Ni vyema tukasubiri hadi October 4 na baadae mchakato wakurekebisha katiba iliyopo!

Kuhusu kuindoa CCM madarakani hizo ni ndoto kabisa na subiri uone dalili za ndoto kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa!
 
Lakini ukae ukijua UKAWA wana imani kabisa na Ikulu ndio maana walikubali mazungumzo nao!

Ndio maana nasema mkanda uwekwe wazi!


Mkuu Rutta,

Usisahau kuwa kile kilikuwa ni kikao kati ya Rais na TCD na sio UKAWA, inabidi utofautishe!
 
Mkuu Rutta,

Usisahau kuwa kile kilikuwa ni kikao kati ya Rais na TCD na sio UKAWA, inabidi utofautishe!

Ukumbuke UKAWA ndio walio pelekea kikao kile na UKAWA ni member wa TCD.
 
Mkuu Rutta,

Hongera sana, kazi ulotumwa na mmeo unaifanya kikamilifu lakini nasikitika kwamba pamoja na michango ya kina unayopatiwa na wachangiaji wenye nia njema na TZ yetu umekuwa mgumu kuelewa na kung'ang'ania ajenda ya huyo mmeo.

Tambua kuwa ipo siku mtayalipa yote haya mnayowafanyia Wa-Tz. Mmelaaniwa nyie!
 
Wanasema ukiwa muongo jifunze kutunza kumbukumbu. Nyie watu ni wanafiki sana. Unasema vyama vya siasa wanachama wake hawazidi 10m hivyo mamlaka ya viongozi wa TCD kuwasemea watanzania 45m wameyatoa wapi???

Hivi nyie mna ugongwa gani? Make majibu yenu hayaeleweki hata mnataka ni. Mlizaliwa kupinga tu???

Hivi nikuulize swali. Hayo maoni ya warioba ya watu elf170ndiyo umeona ni maoni ya watanzania wote kuliko maafikiano ya viongozi wa TCD wanao ongoza watanzania 10m???

Nyie ni wapumbavu sana make hampendi kuelezwa ukweli. Mmebaki na kazi moja tu ya kumsuribia jirani kafanya nini ili mmpingie tu.
Mimi naweza kubishana na Great Thinker na siyo mtu wa Face Book!
 
Sababu ya kuiomba hiyo video ni kuondoa unafiki maana with wengine wamesha anza kuamini Ukawa hawakukubali bunge liendelee hadi October 4!
Na swala la maongezi kuwa ya kificho liliombwa na viongozi wa UKAWA waulize!


Ina maana na wewe huamini kama walikubali katiba iliyopo ifanyiwe marekebisho?huamini kuwa walikubali swala la katiba litaendelea baada ya uchaguzi?


Swala la kusema sijui maoni ya wananchi yanatupwa ni inayo jadiliwa si rasimu ya warioba huu ni uongo labda mtwambie zile sura. mbili walizojadili UKAWA zilikuwa kwenye rasimu gani?

Kumbuka bunge limepewa mamlaka ya kubadilisha,kuongeza,kurekebisha chochote kwenye Rasimu na sheria!

Basi tunaweza kukubaliana kuwa hakuna mwenye mamlaka ya kusitisha bunge! Ni vyema tukasubiri hadi October 4 na baadae mchakato wakurekebisha katiba iliyopo!


Kuhusu kuindoa CCM madarakani hizo ni ndoto kabisa na subiri uone dalili za ndoto kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa!


  1. My question is still unanswered; Unaiamini Ikulu/CCM itakupa hiyo video halisi au sopporting document yoyote ya mazungumzo hayo na bado tukaiamini? Na nani mnafiki hapa kati ya; Ikulu iliyokuwa inajua TCD/UKAWA ni wanafiki na kuamua kufanyia hayo mazungumzo hayo gizani na baadaye waanze kutu - fool kama ilivyo sasa au ni UKAWA halisi kwa akili yako?
  2. Hili la kufanyia marekebisho Katiba ya 1977 ili ku - accomodate mahitaji ya sasa wenye akili tulilisema siku nyingi mara baada ya nyie CCM kudandia kwa nyuma hoja ya kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya mapema mwaka 2011 huku mkijua haikuwa katika mipango yenu ya miaka 5 (ilani yenu ya uchaguzi ya mwaka 2010). Kwa maana hiyo tulijua hamuwezi na mtashindwa tu na ndicho tunachokishuhudia sasa. Kwa hiyo hili Ukawa hata kama walilikubali, sioni ajabu!!.
  3. Likely wewe inaelekea hujui kitu!!...Unatambua kuwa Rasimu ya 2 ilijengwa katika msingi wa Muungano wa Shirikisho la serikali 3 kwa maana ya ile ya Muungano,ya Tanganyika na ya Mapinduzi ya Zanzibar na ambayo kiukweli ndiyo sura halisi ya muungano ambao ni clear na fair kwa nchi zote mbili zilizoungana? Unatambua kuwa hayo ndiyo maoni ya wananchi na yanastahili kuheshimiwa? Nini kinachoendelea Dodoma kwa sasa? Ni wazi Rasimu hii imeshatupwa kule na sasa kinachojadiliwa ni kingne tu, Rasimu ya CCM na wakati huohuo wanakusanya maoni mengine tu kinyume cha sheria kabisa iliyoliweka hilo bunge!!.
  4. Inawezekana BMK lina mamlaka hayo ya kubadilisha na kufanya marekebisho yoyote LAKINI SI KUVUNJAVUNJA MOYO WA RASIMU YA PILI, na hapa ndipo Mgogoro ulipoanzia na kuleta haya ya TCD na Ikulu/CCM kukutana eti kuweka mambo sawa ili mchakato wa kuandika Katiba uendelee na umalizike salama!!.
  5. Acha kutudanganya mwenye mamlaka ya kusitisha BMK kupisha maridhiano yupo tena hata Mwenyekiti mwenyewe Mr Sitta anaweza kufanya hivi na alishawahi kufanya wakati walipopisha Bunge la Kawaida la Bajeti. Wala hili halihitaji kufika hata kwa Rais!!
  6. Kama unafikiri CCM yako iko imara sana kwa sasa,subiri mwakani.Na narudia tena hili ndilo bomu kuu likalowalipua jumlisha vibomu vingine kibao mlivyovitengeneza wenyewe!!..Hata vibaraka wa KANU ya Kenya ya wakati ule walikuwa kama nyie mlivyo wa CCM ya leo, mvinyo uliwalevya ukawachanganya na kudhani kuwa wako salama na wanapendwa kweli watakuwa pale milele, wako wapi sasa? Maandishi ya yako ukutani na hakuna mwenye uwezo wa kuyasoma na kuyatafsiri...........Kalagha bhaho!.
 
Back
Top Bottom