JWTZ yakamata maafisa wanne wa Rwanda nchini Congo

JWTZ yakamata maafisa wanne wa Rwanda nchini Congo

ASKARI wa UMoja wa MAtaifa wanaolinda amani nchini KONGO (Monusco) , Wakiongozwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) , wamedai kuwakamata maofisa wanne wa ngazi za juu kabisha Wa Jeshi la RWANDA wakiwa wanawasaidia waasi wa M23. MAAFISA hao wanashikiliwa kwa mahojiano

Habari imeendelea kusema kuwa kukamatwa kwa MAAFISA hao na kusambaratishwa kwa waasi wa M23 kumefanikisha kushinda vita hiyo kwa 95% na kwamba tayari Monusco wanaoongozwa na JWTZ wameanza kufurahia ushindi huo na kwamba sasa hivi wanasubiri tamko kutoka kwa wakuu wao, ili kufahamu kinachofuata baafa ya kufanikisha hatua hiyo.

SOURCE:MTANZANIA.

Kinachofuata ni safari ya Kigali.
Vinginevyo itakuwa ni sawa na kutibu malaria kwa paracetamol.
 
Tehe tehe tehe......inabidi awafungulie 'majenerali' wake aliowaweka kizuizini ili wamsaidie mbinu za kivita......! Maanake kwa Rwanda alizoea kupeleka wapiganaji Congo......ambapo askari anaingia msituni leo akiwa luteni usu then baada ya miezi sita anaibuka akiwa 'Brigedier General'....! Bila shule ya vita huwezi kupiganisha vita..........!

Tulishasema humu kuwa Kagame na kagenge chake cha wahuni ni mzigo wa eneo lote la maziwa makuu...!
 
Hii vita haipaswi kuishia congo. Twende hadi kigali tukamtoe mkondefu masikio punda. Jwtz go go. Huwez kucheza na tz nyani wewe kagame

Mkuu tupo pamoja. kitendo cha kumuua Kamanda wetu kilinisikitisha na kunikera sana.
 
Niliwai kuwaeleza watu humu kuwa, hii Brigedi mpya inayoundwa na Tanzania na Africa Kusini ni moto wa kuotea mbali.
Kwenye masuala ya kijeshi, nchi hii huwa aikurupuki.
 
kamata mwizi.......................................................
 
JWTZ juu kumbe Mwamunyage soo ,yeye ni kimya na kutwanga tu. Naona sijawaona kwenye twiter wakijitapa.
 
Hii vita haipaswi kuishia congo. Twende hadi kigali tukamtoe mkondefu masikio punda. Jwtz go go. Huwez kucheza na tz nyani wewe kagame

Kwakuwa uko nyuma ya keyboard unadhani ni rahisi kiasi hicho kwenda hadi Kigali ndiyo maana unatoa matusi,kwa taarifa yako Wazungu hawawezi kukubali twende Kigali kwani wanajua kule hakuna raslimali za kuchota wakati tunapigana, vita isikie tu na kama JWTZ linashinda huko ni jambo jema, lakini lazima tujiulize haya yote Wazungu wana mikono yao huko ili waendelee kuchota, ukiona ushindi unaanza kupatikana ujue Wazungu wameshachota raslimali za kutosha na muda si mrefu hii vita itaisha. Ni bahati mbaya sana kuona Waafrika tunaendelea kupiganishwa na Wazungu ili wao wajichotoe raslimali na kesho sie tunaenda kuomba kwao.
 
Nadhani jeshi liende hadi kigali make mabasi yanayo tekwa kigoma na Biharamulo ni ya jeshi la kagame. so JWTZ songa mbele kagame katuchosha
 
Nina mbwa wangu nyumbani huwa ni mchokozi mno na kutokana na tabia yake hiyo niliamua kumiita jina la Kagame


Wazo zuri sana! Mbwa koko wote Tz waitwe hivyo.
 
Hii vita haipaswi kuishia congo. Twende hadi kigali tukamtoe mkondefu masikio punda. Jwtz go go. Huwez kucheza na tz nyani wewe kagame

Unapenda Vita ee? Tuko Congo kwa sababu gharama zote za vita zinalipwa na Umoja wa Mataifa, Pia South Africa wamepeleka vifaa vya kisasa, kwa uchumi wetu kaputi tukijifanya kutaka kuingia Rwanda tutarudi mwaka 1980, omba sana vita na Rwanda isitokee, Kagame hana cha kupoteza, anapenda Vita.
 
Mna uhakika gani kuwa hao maofisa ni wanyarwanda?

Hapa hata mimi nachelea kukubali.Hii inawezekana ni propaganda tu..hao M 23 walishajiondoa maeneo ya Goma wakasema ni sehemu ya mbinu (Strategy).Ila kama ni kweli basi gud nyuuz
 
Rwanda haiko kama mnavyojidanganya nyuma ya keyboard, udogo wa nchi sio hoja, refer vita ya Eritrea na Ethiopia, Kagame ana jeshi kubwa na uwezo wa kifedha kuendesha vita, nchi yetu ni Kubwa lakini hatuendi vitani wote, Rwanda ina wanajeshi 61,000 waliofunzwa vizuri, ni upumbavu, narudia tena ni upumbavu wa hali ya juu, kuomba kupigana na Rwanda
 
ASKARI wa UMoja wa MAtaifa wanaolinda amani nchini KONGO (Monusco) , Wakiongozwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) , wamedai kuwakamata maofisa wanne wa ngazi za juu kabisha Wa Jeshi la RWANDA wakiwa wanawasaidia waasi wa M23. MAAFISA hao wanashikiliwa kwa mahojiano

Habari imeendelea kusema kuwa kukamatwa kwa MAAFISA hao na kusambaratishwa kwa waasi wa M23 kumefanikisha kushinda vita hiyo kwa 95% na kwamba tayari Monusco wanaoongozwa na JWTZ wameanza kufurahia ushindi huo na kwamba sasa hivi wanasubiri tamko kutoka kwa wakuu wao, ili kufahamu kinachofuata baafa ya kufanikisha hatua hiyo.

SOURCE:MTANZANIA.

Wanasubiri kuagizwa kuitafuta Kigali
 
Back
Top Bottom