JUSSA: Mishahara ya Wanasiasa ipunguzwe

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
Mbunge Ismail Jussa ambaye hana muda mrefu bungeni na hajafaidi matunda ya Bunge, ameomba bungeni mishahara ya wanasiasa ipunguzwe kufidia kipato duni cha wafanyakazi wa umma, kauli yake imepingwa vikali na wabunge ambao wako zaidi ya miaka 20 akiwemo na naibu spika Ana Makinda ambaye alimwambia Jussa kama anataka hivyo, basi aanze Jussa kupunguza mshahara wake!! Wadau wa JF mna maoni gani?
 
Ni ngumu sana kupokelewa kwa wazo hilo. ..Kwanza linaonekana kuwa ni wazo la KIUPINZANI zaidi...Lakini pia kushusha mshahara ni kitendo unpractical katika hali ya kawaida, unless kama ni adhabu. Labda kwamba wasiongezwe tena KATIKA MUDA FULANI ujao, ambayo haiko katika discretion yao!...Ila inawezekana kuondoa baadhi ya allowances, not mshahara!...Dawa ni kuwabana mafisadi warudishe hela walizo nazo!
 
Mbunge Ismail Jussa ambaye hana muda mrefu bungeni na hajafaidi matunda ya Bunge, ameomba bungeni mishahara ya wanasiasa ipunguzwe kufidia kipato duni cha wafanyakazi wa umma, kauli yake imepingwa vikali na wabunge ambao wako zaidi ya miaka 20 akiwemo na naibu spika Ana Makinda ambaye alimwambia Jussa kama anataka hivyo, basi aanze Jussa kupunguza mshahara wake!! Wadau wa JF mna maoni gani?
Wafanyakazi na wakulima, hao ndio wabunge wenu mliochagua kutetea maslahi yenu. Habari hiyo hapo inaonyesha kipaumbele chao kipo wapi zaidi. Hata hivyo, uamuzi upo katika mikono yenu wakati wa kupiga kura.
 
Ah!! Temea mate chini. Tusijidanganye kuwa wanasiasa wana chembe ya huruma kwa watu wa kaweaida! Si unamsikia Sitta akimuagiza Mkulo kutatua 'matatizo ya Waheshimiwa Wabunge' eti kwa kipindi cha masaa lakini watumishi tunabaki tukidai kwa miaka.
 
Kila mtu anataka kuwa mwanasisa kwa sababu ya maslahi mazuri zaidi, matokeo yake wataalamu hawaoni haja ya kutumikia jamii katika nyanja zingine zaidi ya siasa inayolipa zaidi.

Vurugu katika kuwania nafasi za kisiasa ni kwa sababu tu ya kipato na wala siyo wito kama wachache wanavyodanganya.

Tunahitaji mfumo ambao kipato kinachotokana na siasa kwa nafasi kama MP, DC, RC, kiwe kidogo kuliko kinchotokana na utaalamu uliobobea ili tupate wanasiasa wa wito na wtaalamu wabaki kwenye fani zao.

Wanasiasa walio wengi sasa hivi ni watu waliojaa tamma, wezi au washirika wao, mafisadi au washirika wao na ni wachache sana unaoweza kuwatenganisha na maovu yanayoangamiza wananchi wa kawaida.

Mfumo wa kisiasa uliopo sasa umewapumbaza wananchi na kujiona kuwa wanyonge wasiostahili maisha mazuri, na bdala yake wao ni watumwa na wapiga debe tu wa wanasisa.

Mifano halisi ya utumwa wa akili na kuwapigia debe wanasisa na familia zao inapatikana humu humu unaposoma posts za wanaJF.

Lazima tujue kwamba mwenye shibe hajui njaa na hivyo kutegemea utetezi kutoka kwa wanaolipwa zaidi ya mara hamsini ya mshahara wa mfanyakazi wa kawaida haiwezekani.

Tunahitaji tujenge jamii ambayo walio wengi ambao siyo wanasiasa na ni wazalishaji wanaweza kuwa na uwiano sawa kimapato na wachache wasio na tija kwa asilimia kubwa (kwa hali halisi ilivyo sasa), ambao ni wanasisa.
 
Anna Makinda! Kashiba sana na keshasahau alikotoka. Ndivyo wanavyo-behave Watanzania wanaopata nafasi, tena za kupewa na wananchi wenzao.

Wakishafika juu na kuanza kufaidi jasho la Watanzania wenzao wanasahau! Halafu hawa hawa akina Makinda ndio waliokuwa wakijipendekeza kwa Mwalimu Nyerere na kumdanganya wako pamoja naye katika kutekeleza siasa ya Ujamaa na Kujitegemea! Ujamaa ni kugawana kile kilichopo kwa viwango ambavyo havipishani sana.

Lakini ndugu yetu Anna Makinda anapata zaidi ya milioni 7 kwa mwezi fedha ambazo wala hazitolei jasho. Anaishi kwenye kasiri lenye ubaridi mwanana, anatembelea gari lenye viyoyozi na wala vumbi halimpati; kazi yake ya Ubunge ni ya msimu tu wakati wote ni starehe mtindo mmoja. Makinda keshasahau 'wahasibu' wenziwe ambao wanaamka saa 11 alfajiri kuwahi daladala kwenda kazini, wakifika kazini wanashinda kutwa nzima bila hata chai wala mlo wa mchana, wanasubiri jioni wakale ugali na dagaa ama mchicha na watoto wao kwa sababu kimshahara wanachopata hakiwapi luxury hiyo.

Anna Makinda na wenziwe wenye kula jasho la wananchi wenzao, asubuhi wanapata heavy breakfast, mchana wanakula msosi heavy na kusaza. Kweli mwenye shibe hamjui mwenye njaa! Lakini, ole wao! Itafika siku wananchi watachoka hapo ndipo watakapoyaona makasiri yao na magari ya viyoyozi yamebadilika yamoto badala ya kuwa baridi! Siku hiyo haiko mbali sana kwa sababu Mwalimu Nyerere alishawaonya na hawakusikia!

Asiyesikia la mkuu huvunjika guu!
 
musidanganyike wabunge wa ccm hawahitaji msaada wa wananchi kura wao wanapewa na tume ya uchaguzi. hawana haja na walalahoi
 
I partly agree kwamba wanasiasa wapunguziwe hiyo mishahara, lakini zoezi lisiishie tu hapo, bali liende kwene fani zote ambazo HAZINA CONTRIBUTION TO HUMANKIND.

Technically hata hiyo kupunguza mshahara tu ni cha mtoto. Wabunge wanakula ela nyingi zaidi kwene posho. (waje wenyewe hapa watuambie wanavoitafuna nchi WITH ZERO OUTPUT). SIASA is fvcking this country not only kwene hiyo mishahara na posho, kuna angle nyingi tu za maamuzi ambapo wanasiasa hujifanya wanajua KILA KITU ati kwa sababu WAMECHAGULIWA KWA KISHINDO.

Cha msingi wandugu ni kuipiga chini SIASA. Tusijidanganye kwamba kuna compromise somewhere at a point of time or/and space ambapo tunaweza ku-optimize.
 
Tunataka aina hii ya wabunge kwani kwa hivi sasa badala ya wabunge kuwa waajiriwa wetu wamekuwa waajiri- 1964 Mwalimu aliona haya na alianza kwa kujipunguzia yeye mwenyewe mshahara na marupurupu na ikaendelea hadi wafanyakazi serikalini na mashirika ya umma.
Kwa kupunguza ulwa kwa waheshimiwa hawa itasaidia kujichuja kwa wengi wao wameingia jumba kuu kwa maslahi yao binafsi na siyo maslahi ya wanaowakilisha.
 
Nchi hii ni ya wanasiasa, siyo ya wananchi. Watanzania tuachane kidogo na hawa wanaisasa wa CCM ili tujaribu wengine angalau kwa miaka mitano tu. CCM wanachukulia kuwa nchi hii ni yao na wanaweza kuifanyia lolote watakalo. Tukishwafundisha wanasiasa hao kuwa nchi siyo yao bali ni yetu, wote wataanza kuwa na adabu. Leo hii wabunge wa CCM wanatumia hela nyingi sana kwenye primaries kuliko kwenye uchaguzi wenyewe kwa vile wanawachukulia wananchi for granted, kuwa akishateuuliwa na CCM basi kapeta
 
Hungary na Spain zimetangaza punguzo la mshahara kwa ajili ya wafanyakazi wa umma kwa ajili ya kukwamua uchumi.

sisi badala ya kupunguziana posho na mishahara kwa kuanzia kwa wanasiasa ndio kwanza posho zinaongezeka......hivi kweli ni haki kwa mbunge kupata allowance ya siku moja ambayo ni zaidi ya mshahara wa mwezi mzima wa mfanyakazi wa umma!?

wabunge wetu hawapo kwa maslahi yetu, wanaganga njaa tu
 
ivi wanaendaga misikitini na makanisani awa wanadamu waso na utu wala haya?
jussa kp t up.thou wat u say z unpractical bt u can pump t again in other way round like kwa miaka mitano awa mabwanyenye wasijiongezee mshahara au posho na baadhio ya posho na feva nyngine wasipate

kp t up!!!!!!!
 
ivi wanaendaga misikitini na makanisani awa wanadamu waso na utu wala haya?
jussa kp t up.thou wat u say z unpractical bt u can pump t again in other way round like kwa miaka mitano awa mabwanyenye wasijiongezee mshahara au posho na baadhio ya posho na feva nyngine wasipate

kp t up!!!!!!!
Wengi wa wanasiasa dini yao kubwa ni siasa na ndiyo maana hawana ethics. Cha msingi ni wananchi [hasa wale wanaowafahamu] kuwafichua. maana these guys kwao anything goes ili mradi waingie kwenye madaraka
 
Huyu angekuwa mbuge wa kuchaguliwa kupitia kwenye jimbo wala asingesema haya, kwani angerudisha vipi mikopo na fadhila za kupata ubunge?
 
Back
Top Bottom