Tarehe moja mwezi wa Sita mwaka huu, wamasai wa Ngorongoro wameapa kuandamana na kufunga kabisa geti kuu la kuingia hifadhi ya Ngorongoro hivyo kuzuia shughuri yoyote ya utalii kuendelea katika hifadhi hiyo kama serikali haitasikia kilio chao na kutatua tatizo la njaa linalowakabili kutokana na kuzuiwa kulima kilimo cha kujikimu kando ya Hifadhi hiyo.
Hapo kabla Serikali ilipiga marufuku kilimo cha kujikimu kando kando ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa madai kuwa kinaharibu makazi asilia ya wanyama.
Mamia ya wamasai hao walikuwa wamekusanyika wakiwa na viongozi wao wa kijadi na kijamii na kutoa kauli moja.
Waziri wa Maliasili na Utalii Hamis Kagasheki ulipoulizwa kuhusu swala hilo alijibu kwa hasira kwa kusema, vitisho hivyo havimbabaishi na hana mamlaka ya kushughulikia suala hilo kwani linahitaji uteuzi wa mkurugenzi mpya wa Hifadhi hiyo na hiyo ni kazi ya rais.
*SOURCE: Channel Ten
Hapo kabla Serikali ilipiga marufuku kilimo cha kujikimu kando kando ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa madai kuwa kinaharibu makazi asilia ya wanyama.
Mamia ya wamasai hao walikuwa wamekusanyika wakiwa na viongozi wao wa kijadi na kijamii na kutoa kauli moja.
Waziri wa Maliasili na Utalii Hamis Kagasheki ulipoulizwa kuhusu swala hilo alijibu kwa hasira kwa kusema, vitisho hivyo havimbabaishi na hana mamlaka ya kushughulikia suala hilo kwani linahitaji uteuzi wa mkurugenzi mpya wa Hifadhi hiyo na hiyo ni kazi ya rais.
*SOURCE: Channel Ten