JUMBA LA DHARAU -SEHEMU YA NNE
Watu walio hukumiwa kunyongwa ni wenye ushauri mzuri na wanabusara sana, nitofauti kabisa na simulizi zilizoko mitaani juu ya wafungwa mbalimbali. Tena leo nataka nikwambia jambo moja, maisha ya gerezani hayatofautiani saba na maisha ya Uraiani kitu pekee kunachotutofautisha ni UHURU. Wafungwa hawana uhuru kama tulionao sisi.huwezi kuaona thamani ya uhuru mpaka huo uhuru utakapo chukuliwa na mamlaka nyingine, ndipo utakapo udai kwa Gharama ya jasho na ikibidi Damu.
Baada ya kupiga michapo na na wafungwa wa KONDEM, tuliagana nao kwa kupeana mikono na kila mmoja kwani huwenda ikawa ndio mwisho wa sisi kuingi katika jengo lile tena katika historia ya maisha yetu labda kama tutahukumiwa kifo. Yule askari akatutoa mpaka nje ya lile jengo, kisha akasema , “MUWE WAANGALIFU VIJANA” ni kweli kabisa maisha ya Jera ni maisha yenye tahadhali kubwa sana kwa kila dakika inayo kufika.
Rafiki yangu Dickson maarufu kama CHEA akaniuliza twende tukapumzike wapi? Nikawaza nikamwambi twende kwenye kibanda cha TV tukaoshe macho. Tulipofika pale tuu. Akaja Askari mmoja akamuita Dickson na kuondoka nae. Nilipata mashaka kidogo hivyo iliniradhamu kuwaangalia muda wote bila kupepesa jicho langu pembeni. Wakafika karibu na maeneo ya utawala wakaa kwenye kingo za kuta ambazo kwa nyuma yake kumepandwa maua. Ni kama watu wanaofahamiana kwani nilimuona Dick akiongea nae kwa furaha bila kuwa na sura ya hofu na mashaka. Lakin bado haikutosha kuamini kwamba amani ilitawala pale walipo. Ilinibidi niondoke kwenye kibanda cha Tv na kutafuta pembe nzuri ambayo itanipa nafasi ya kuwaona bila kukingwa na mtu au kitu chochote ndipo nikaenda kukaa karibu na jengo la Zahanati ya wafungwa.
Pale nilikuwa nimekaa peke yangu lakini baada kama ya dakika kumi alikuja mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya mfungwa lakini mtu Yule alikuwa wa tofauti sana na wafungwa wengine, Sare zake ilikuwa ni safi sana, kuanzi kofia, shati mpaka viatu na usoni alikuwa na amevaa miwani nadhani itakuwa ni ya macho, na mikono alikuwa na kamkoba wa nailoni juu umeandikwa my clear bag, ni mikoba maarufu sana uraiani.ndani ya mkoba ule kulikuwa na nyaraka mbalimbali pamoja na kalamu ya wino na kalamu ya risasi. Huyu mfungwa alikuja kukaa karibu na mimi, na akanisalimia kwa salamu hii,” we mhalifu haujambo “ nikamjibu sijambo lakini mimi sio mharifu, akaniangalia kisha akatabasamu akaniambia kila aliyeingia humu ndani ni mharifu wa makosa mbalimbali kama vile jinai, Mada, uhaini, na ufisadi, akaniuliza kesi yako ni jinai namba ngapi nikamtajia, akaniambia unakataa nini sasa wakati wewe ni mharifu wa kosa la jinai. Hapo niliishiia pozi. Nikamwambia haya bwana nimekusoma vizur
Pamoja nilikuwa na ongea nae lakini nilikuwa na muangalia kwa makini sana kwa sababu sikutaka kumuamini mtu yyote ndani ya jera ile.nilichokigundua kwake ni kwamba kwenye sare yake hakukuwa na namba ya kutoka gerezani kama kwenye sare za wafungwa wengine. Ikanibidi nimuulize “mbona sare yako haina namba ? Yule jamaa akaniangalia tena usoni kisha akanikazia macho na kuniambia “mimi natumikia kifungo cha maisha” hivyo sinto toka gerezani nikiwa hai labda nikiwa maiti, hata nikifa sintaishi uraiani bali nitaenda kuishi maisha mbinguni nako sijui peponi au motoni , akatabasamu tena , hapo nikapata shauku ya kutaka kujua kosa lililomfanya yeye kufungwa maisha hivyo nikamuuliza ulifanya kosa gani, akanijibu niliua watu wawili na hata leo wangekuwa hai ningewaua tena na hata kama siku yamwisho ya hukum mbele ya Mungu nitaonana nao basi Nitawaua kwa mara nyingine, huyu alikwa mfungwa wa ajabu sana ,nikamuuliza kwanini unasema hayo, akaniambia unajua bwana mdogo mimi nilipo maliza chuo kikuu nilikuwa ni wakili wa kujitegeamea , kuna mwanamke mmoja ambae nilikuwa nasoma nae pale chuo kikuu ya Dareslaam mimi nikiwa mwaka wa ne yeye alikuwa mwaka wa kwanza, Yule mwanamke alikuwa anaitwa Joice, nilitokea kumpenda sana, siku mmoja nikakutana nae katika viunga vya chuo, na nikamtongoza kwakweli hakunisumbua sana mwisho tukawa wapenzi baadae nikagundua Yule binti anatoka familia maskini sana hivyo nikajipa jukumu la kumuhudumia kwa kila kitu ikiwemo kumlipia ada ya chuo kwasababu wazazi wangu walikuwa na uwezo kidogo. Hata baada ya mimi kumaliza chuo tuliendea na mahusiano mpaka nikafunga nae pingu za maisha , lakini huwezi kuamini kwamba huyu mwanamke ndio chanzo cha mimi kuwa ndani ya JUMBA hili la DHARAU, Hadithi yake ilinivutia sana na kutaka kujua nni kiliendea,nikamuuliza sasa ikawaje akaniangalia tena kisha akatikisha kichwa ishara ya kusikitika akasema nilizaa na Joyce watoto wawili nilkuwa na furaha na amani, ndipo likanijia wazo la kwenda kuongeza elimu katia ngazi ya shahada ya uzamili chuo kikuu cha Dar eslaam. Ndoa yetu ilidumu kwa muda wa miaka tisa hivi nikawa najipanga kufanya sherehe ya kutimiza miaka kumi ya ndoa yetu ananisimulia Yule mfungwa anaetumikia kifungo cha maisha. Akaendelea.... siku moja nilikuwa natoka mahakamanikuwatetea wateja wangu waliokuwa na kesi mbalimbali, nilipofika nyumbani nikakuta nyumba ipo kimya sana, ambapo si kawaida, na kwa bahati nzuri au mbaya siku hiyo nilikuwa nimeacha gari yangu ofisini sijui ni kitu gani kilinifanya nitembee kwa mguu siku ile. Baada ya kukuta nyumba ipo kimya lakini milango iko wazi nikaingia hadi sebuleni sikukuta mtu nikaenda jikoni pia sikukuta mtu, nikapata wasiwasi maaa nilipo ona mlango wa chumba changu uko wazi kwani chumba changu kilikuwa karibu na jikoni. Basi ikabidi nijisogeze huku nikwa na hofu kwani leo nyumban pako kimya mno , nilipofika mlangoni nilianza kusikia miguno na kelele za mahaba ndipo nilipo ingia chumbani sikuamini macho yangu, nilimkuta Mke wangu akifanya mapenzi na rafiki yangu nilipata hasira sana , Yule jamaa alikuwa amemkunja mke wangu kama kifurushi cha maindi mabichi lakini kwa bahati mbaya hawakuniona maana walizama kwenye adimbwi kubwa la mahaba. Kwanza nikaufunga mlango taratibu bila wao kustuka kisha Nilikwenda kwenye droo la kabti langu, nilipovuta ile droo ndipo wakastuka kwamba ndani kuna mtu lakini tayari nilisha chukua BASTORA yangu kwakweli sikutaka kusikiliza maneno ya mtu ya mtu yeyote wote niliwapiga risasi na wote walikufa palepale mimi nikatoka na kwenda kujisalimisha kituo cha polisi. Baada ya hapo nikahukumiwa kifungo cha maisha. Daa niliumia sana kuona elimu ya Shahada ya Uzamili (Masters ) inatumikia kifungi cha maisha, hivyo ndivyo ilikuwa bwana mdogo , huku akitabasamu nikamuuliza kwa hiyo elimu yako haina kazi tena akasema hapana huwa naitumia nikiwa humu gerezani, huwa nawapa ushauri wa kisheria watu mahabusu na wafungwa walioko humu. Nimeandika rufaa nyingi nikiwa humu na zimewasaidia watu wengi na wengine wameshinda rufaa zao na kuniacha mimi gerezani. Akafungua mkoba wake na akanionyesha vyeti vyake kumbe muda wote anatembea na vyeti vyakekila utakapo muona gerezani.
Pia nae alitaka kujua vp kuhusu mmi kwa nn nimeletwa gerezani kama mahabusu, nikamuelezea kwa kirefu sana. Kwani mkuu wa chuo chenu ana elimu gani nikamjibu ni Profesa, Yule jamaa akasema hakuna profesa mwenye maaamuzi ya kijinga kama hayo., hapo ninyi watawapotezea muda hilo sio kosa la kimfunga mwanachuo kokote duniani hapo watawapotezea muda kisha watasema hawana maslahi na kesi. Dickson akaja nilipo nae akaketi jirani name pia nikamuliza Yule afande alikuwa anakwambia nini akasema Yule afande ni mtu wa Nyumbani bukoba alikuwa anataka nimpatie namba ya baba iliwafanye mpango tupae dhamana si unajua huku atuna ndugu. Hapo matumaini ya kutoka Gerezani yakaaza kuereje, sasa je tulifanikiwa kutoka Gerezana? Endelea kufuatilia simulizi hii ya JUMBA LA DHARAU
na
Rashid Karume
Njombe Imagination of Progressive Technology
S L P 1093
Njombe
0754913924